Dada yetu
Tamalisa kuna huu utaratibu wa watu kuelekea vyuoni kusomea chochote....yaani akiwa hana loop ni nini cha kufanya baada ya kutoka chuoni!
Kama unapenda utangazaji usisomee Udaktari kisa tu unafaulu Biology na Chemistry darasani. Somea utangazaji. Utafanya vizuri zaidi. Watu wengi waliofanikiwa duniani wamefanya vitu wanavyovipenda!
Kama umesomea fani usiyoipenda kisa tu umeambiwa ina kazi za haraka haraka au ina hela umepotea. Siku ukimaliza kusoma usipate kazi au ukapata kazi lakini isiwe na hela kama ulivyotarajia utapata fadhaa na huenda kuchukia wale waliokushauri!
Kama umesomea kitu usichokipenda achana nacho, fanya kile unachokipenda na kinachokupa amani. Kama umesomea Sheria wakati moyo wako upo kwenye biashara ni ngumu sana kufanikiwa kupitia sheria. Achana na sheria, fanya biashara.