Kilichomsukuma Raisi Kikwete kuanzisha mchakato wa katiba mpya ni kutoka kwa wapinzani, baadhi ya NGOS, wanaharakati, vyombo vya habari na wengineo. Pamoja na kulikubali hili ilikuwa tuanze na kura ya maoni kuwauliza wananchi kama:
1. Wanahitaji muungano au la
2. Wanahitaji muungano wa serikali ngapi? Moja, mbili, tatu ama vinginevyo
3. Utawala utakuwaje.
Baada ya kupata maoni haya ndio angeunda hiyo tume ya kutunga katiba, tume hii ingekuwa tayari inajua inatunga katiba kwa muundo wa serikali ya aina gani sio ilivyo sasa ambapo tume imetunga rasimu ambayo bado ina utata kuhusu muundo wa muungano na ambapo iko katika muelekeo wa serikali tatu ambapo baadhi ya wadau wanapinga.
Utata mwingine uko katika muundo wa bunge la Katiba. Muundo wa bunge ungeundwa kutokana na matakwa ya wananchi kuliko ilivyo sasa ambapo wengi ni wabunge waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo hawakuchaguliwa kwa madhumuni haya. Naona uchaguzi ungekuwa kwa madhumuni ya kuunda katiba mpya basi wengi wa hawa waliopo sasa wamekosa sifa na wasingechaguliwa, matokeo yake ndio hawa wanaoongoza katika kudai nyongeza ya posho.
NAUNGA MKONO HOJA YA KUWA NA SERIKALI MOJA. Ingawa hili wenzetu wa Zanzibar hawalitaki kwa kuwa baadhi wana uroho wa madaraka wanaona watatupwa nje ya ulingo wa uongozi. Mpaka sasa maendeleo yaliyopo Zanzibar kama ikiwa ni mkoa basi wao wana maendeleo zaidi ya mikoa yote ya bara, kwa hiyo wako katika advantage kuliko kubaki kama nchi. Believe me or not.