Nyamtalakyono
JF-Expert Member
- Dec 17, 2015
- 795
- 479
Ndugu zangu na watanzania wenzangu napendwa kutoa masikitiko na kero yangu kwa Serikali kutokana na unyama tunaofanyiwa na makampuni ya ving'amuzi. Kwanza ni pale Kifurushi kinapoisha wanakata local Chanel zote. Pili ni gharama za juu za Vifurushi vyao lakini kibaya zaidi ni tabia yao ambayo ni mbaya ya kupandisha kila mara gharama za vifurushi. Naomba serikali kali isimamie swala hili litafanya watanzania wengi kukosa habari kwa kushindwa gharama wakati ni haki ya kikatiba. TCRA nadhani ni wakati wenu kuwajibika kama EWURA wanavyofanya kwenye mafuta na umeme.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app