Ni takribani miezi minane sasa wahitimu wa taaluma ya ualimu wako mitaani. Serikali imekuwa ikitaja kuwa moja ya sababu za kuwa na matokeo mabaya mashuleni ni uhaba wa walimu. Naibu Waziri wa Elimu aliahidi ajira kutangazwa mwezi Januari, 2013. Vivyo hivyo Mkuu wa Kaya JK alisisitiza mwezi huo huo wa Januari. Sasa leo ni Februari, sio Januari tena. Au kuna 'political january'? Je, serikali hii ina mpango wa dhati kweli kuinua kiwango cha elimu nchini? Hivi ni kweli kwamba hii ni serikali makini kama inavyosemwa? Nawakilisha!