PostGE2025 Serikali itahakikisha miradi yote ya umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima - Chongolo

PostGE2025 Serikali itahakikisha miradi yote ya umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima - Chongolo

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
726
Reaction score
953
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, ametembelea mradi wa Umwagiliaji uliopo wilayani Masasi mkoani Mtwara ikiwa moja ya muendelezo wa ziara kwa Taasisi za Wizara ya kilimo ambapo amewahakikishia wananchi kuwa Serikali itakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima.
IMG-20251212-WA0183.jpg

Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula.

Mhe. Chongolo amesema hayo wakati wa ziara yake katika mradi huo unaotekelezwa eneo la Ndanda, mkoani Mtwara.
IMG-20251212-WA0164.jpg

Mradi huo unahusisha ujenzi wa bwawa la Umwagiliaji na uchimbaji wa mifereji mirefu, na ukikamilika unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakulima 700 kutoka vijiji saba.

“Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula, amesisitiza.
IMG-20251212-WA0182.jpg

Amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa bwawa hilo ambalo litachochea matumaini mapya kwa wakulima wa Mtwara kwa kuwawezesha kulima mazao mbalimbali ikiwemo mboga mboga, mpunga, mahindi na mazao mengineyo.

Ameongeza kuwa ingawa Mtwara inasifika kwa kilimo cha korosho, serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imeanzisha miradi ya Umwagiliaji katika mikoa ya Lindi na Mtwara ili kuhamasisha uzalishaji wa mazao mengine ndani ya mikoa hiyo bila kutegemea mazao kutoka maeneo mengine.
IMG-20251212-WA0186.jpg

Aidha, Mhe. Chongolo ameisihi Tume kusimamia kwa umakini miradi hiyo ili kuhakikisha thamani ya fedha iliyowekezwa inaonekana na wakulima wanapata uzalishaji unaoendana na viwango vinavyotakiwa.
IMG-20251212-WA0161.jpg

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) Bw. Raymond Mndolwa, amesema serikali imewekeza na inaendelea kuwekeza fedha nyingi kuhakikisha wananchi wa Lindi na Mtwara wananufaika na miradi ya Umwagiliaji , hatua ambayo itawawezesha kufanya kilimo cha uhakika bila kutegemea mvua.
IMG-20251212-WA0157.jpg

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainabu Telacky amewataka wananchi kushirikiana na Tume katika kulinda miundombinu na rasilimali zilizowekezwa na serikali kwa kuwa wao ndio wanufaika wakuu wa mradi huo.

Akitoa taarifa ya mradi huo ,Mhandisi Macklera Mrutu kutoka Tume amesema kuna jumla ya miradi 26 ya Umwagiliaji katika mikoa ya Lindi na Mtwara yenye thamani ya shilingi bilioni 23.7 Hadi sasa miradi miwili iliyoanza na Utekelezaji ikiwemo ujenzi wa mabwawa na mifereji mirefu , mifereji ya kati ambapo itachukua hekta zaidi ya 300 na utekelezaji wake umefikia asilimia 27%. mpka sasa.

Aidha akiongea kwa upande wa wakulima Bi. Pili Nampokela, wameishukuru serikali kwa kuwafikishia mradi huo wa Umwagiliaji wakisema utawawezesha kulima mara 3 hadi 4 kwa mwaka,na hivyo kuongeza fursa tofauti tofauti kama kuongezeka kwa ajira, kuimarisha usalama wa chakula na kupunguza utegemezi wa mazao kutoka mikoa mingine.
IMG-20251212-WA0170.jpg
IMG-20251212-WA0169.jpg
IMG-20251212-WA0178.jpg
IMG-20251212-WA0189.jpg
 
Maji ya kunywa tu shida

Ndio mtapata ya kumwagilia

Samia ndio kashindwa Kutoa hata maji miaka 5

Nonsense!!
 
Propaganda.
Maji ya matumizi ya majumbani tu watu wanaokoteza kwa kubahatisha, ya kumwagilia mashamba itawezekana vipi?
 
Chongolo aambiwe hizo program za umwagiliaji zilianza kabla hajawa uvccm mpaka leo kazi ni kutindua udongo tu.

Wakifanikiwa miradi inakaa miaka miwili mitatu inapotea.
 
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, ametembelea mradi wa Umwagiliaji uliopo wilayani Masasi mkoani Mtwara ikiwa moja ya muendelezo wa ziara kwa Taasisi za Wizara ya kilimo ambapo amewahakikishia wananchi kuwa Serikali itakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima.
View attachment 3514874
Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula.

Mhe. Chongolo amesema hayo wakati wa ziara yake katika mradi huo unaotekelezwa eneo la Ndanda, mkoani Mtwara.
View attachment 3514875
Mradi huo unahusisha ujenzi wa bwawa la Umwagiliaji na uchimbaji wa mifereji mirefu, na ukikamilika unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakulima 700 kutoka vijiji saba.

“Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula, amesisitiza.
View attachment 3514877
Amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa bwawa hilo ambalo litachochea matumaini mapya kwa wakulima wa Mtwara kwa kuwawezesha kulima mazao mbalimbali ikiwemo mboga mboga, mpunga, mahindi na mazao mengineyo.

Ameongeza kuwa ingawa Mtwara inasifika kwa kilimo cha korosho, serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imeanzisha miradi ya Umwagiliaji katika mikoa ya Lindi na Mtwara ili kuhamasisha uzalishaji wa mazao mengine ndani ya mikoa hiyo bila kutegemea mazao kutoka maeneo mengine.
View attachment 3514878
Aidha, Mhe. Chongolo ameisihi Tume kusimamia kwa umakini miradi hiyo ili kuhakikisha thamani ya fedha iliyowekezwa inaonekana na wakulima wanapata uzalishaji unaoendana na viwango vinavyotakiwa.
View attachment 3514876
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) Bw. Raymond Mndolwa, amesema serikali imewekeza na inaendelea kuwekeza fedha nyingi kuhakikisha wananchi wa Lindi na Mtwara wananufaika na miradi ya Umwagiliaji , hatua ambayo itawawezesha kufanya kilimo cha uhakika bila kutegemea mvua.
View attachment 3514880
Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainabu Telacky amewataka wananchi kushirikiana na Tume katika kulinda miundombinu na rasilimali zilizowekezwa na serikali kwa kuwa wao ndio wanufaika wakuu wa mradi huo.

Akitoa taarifa ya mradi huo ,Mhandisi Macklera Mrutu kutoka Tume amesema kuna jumla ya miradi 26 ya Umwagiliaji katika mikoa ya Lindi na Mtwara yenye thamani ya shilingi bilioni 23.7 Hadi sasa miradi miwili iliyoanza na Utekelezaji ikiwemo ujenzi wa mabwawa na mifereji mirefu , mifereji ya kati ambapo itachukua hekta zaidi ya 300 na utekelezaji wake umefikia asilimia 27%. mpka sasa.

Aidha akiongea kwa upande wa wakulima Bi. Pili Nampokela, wameishukuru serikali kwa kuwafikishia mradi huo wa Umwagiliaji wakisema utawawezesha kulima mara 3 hadi 4 kwa mwaka,na hivyo kuongeza fursa tofauti tofauti kama kuongezeka kwa ajira, kuimarisha usalama wa chakula na kupunguza utegemezi wa mazao kutoka mikoa mingine.
View attachment 3514879View attachment 3514881View attachment 3514882View attachment 3514883
Bashe anasemaje?
 
Back
Top Bottom