Pundamilia07
JF-Expert Member
- Oct 29, 2007
- 1,439
- 54
Wadau,
Huyu ofisa aliyekaririwa hapo juu ameongea hayu kama maoni yake binafsi au maoni ya serikali?
Je, ni lini serikali itajitoa katika kufanya biashara? Leo hii bado kuna ofisa wa serikali anaongelea kufufua UDA?
Leo bado kuna ofisa wa serikali bado anaongelea kuleta kampuni kubwa badala ya kuwajengea uwezo wananchi waendelee kutoa huduma kwa maana ya kujijengea uwezo wa kiujasiriamali? Huyu ofisa anakwenda mbali na kuonesha kuwa maamuzi yamekwisha tolewa kuwa kila mwenye gari lake akalikabidhi kwa kampuni kubwa.
Iko haja atuelezee hayo mawazo ameyapata wapi? na pili huenda anamjua huyu mwenye kampuni kubwa, kuna kaharufu hapa?
Sijui kama haya nayo bado yapo hapo Dar. Tulitamba nayo sana wakati wetu, na sidhani kama kweli Dar tuliwahi kuwa na usafri mzuri zaidi ya huu. je vijana wa leo mnayafahamu? tulikuwa tukiyaita kumbakumba
Kumalizia, wanasema kama kila mtu atakuja na nyanya sokoni mnunuzi atakua nani?
Sisi wabongo ndio zetu, utakuta sehemu hapana kitu chochote, ukaja na idea yako ukaanzisha kitu, watu wengine wakiona unapata faida basi wanaanza kile ulichoanza pale pale ulipoanzisha.
Pundamilia we sema tu una magari ya daladala.
Kuna kuikosoa serikali lakini sio kila kitu kinachofanywa na ofisa wa serikali nikibaya.
Mimi nilisomea nje na najua uzuri wa mabasi makubwa kwa ajili yakuwasafirisha abiria.
Hakuna msongamano na mabasi yanakufikisha kwa wakati unaoutaka.
Walioko Europe au Marekani watanifahamu ninachosema.
Kama wewe unataka soko huria basi fanya kama Arriva wanavyofanya Europe.
Tangaza biashara yako kwa serikali ili wakupe kazi, ina maana hio ukivunja masharti ya mkataba kazi anapewa mwengine.
Uwe na mabasi yakuwatosha abiria na yaondoke kwa muda bila kuchelewa.
Huu utitiri wa magari ya abiria ndio hata serikali inashindwa kukontroo magari kwa wingi wake, na ndio maana kila leo ajali za magari ya abiria zinatokea.
Kila mtu akipata vipesa vyake tu anatafuta kigari na dereva na kuweka gari barabarani. wanawekwa madereva ambao hata hawana ujuzi ili mradi tu bosi anapata pesa. Matokeo ajali za kila mara
Hakuna mji wenye kero ya usafiri kama Dar.
Dar hata kama una gari nawataka kwenda kazini lakini kero yake utaiona, foleni kila barabara.
Na siku ukisema utumie daladala kwenda kazini basi ujiandae kwa mambo mengi, foleni, kugombania daladala wakati wa asubuhi, unatoka asubuhi msafi ukirudi nyumbani mchafu.
Kukiwa na shirika moja tu lenye uhakika kusafirisha watu kwenda waendako sijui kama watu wataamua wapande magari yao kwa kila siku.
Kumbuka pia foleni pia inasababishwa na huu mtindo wa kila mtu ambaye ana uwezo anaweka gari lake barabarani.
Soko huria
Liwe shirika moja kubwa hata ni la binafsi ambalo lina magari yakutosha kusafirisha abiria wa Dar.
Liwe linafuata sheria za mkataba kwamba watu wengi wakilalamika kwamba wanachelewa au wanasongamana basi mkataba upewe mtu mwingine.
Hapo tutaifaidi Dar yetu.
Darwin,
Ahsante sana kwa mchango wako mzuri sana. lakini nilikuwa ninataka kukumbusha kuwa wengi wa watanzania ambao wanafanya biashara hasa ndogo-ndogo, ni watu ambao wameweza kujitafutia mitaji kwa nguvu zao wenyewe bila ya kupata msaada wa serikali au mabenki. Sasa basi unapotaka kuwashirikisha katika mipango ya serikali ni vema ukapata maoni yao halisi ili kuweza kuilinda mitaji yao ambayo wameitengeneza kwenye mazingira magumu sana. Serikali inapofikia hatua ya kusema itawaletea makampuni makubwa na wao wapeleke magari yao huko, hivi kweli hii nikauli sahihi?
Kwani nini serikali isiratibu shughuli zao na kuwapa uwezo wa kulinda mitaji yao kwa kuwafanya wao ndiyo wawe wadau wakubwa wa hayo makampuni makubwa?
Tuliangalie hili kwa makini sana kwani tusipoangalia sasa tutarudi hapa baadae kupiga kelele baada yakuona kila shida zetu sisi watanzania ni furaha na faraja za wageni na wenzetu wachache.
Huyu ofisa wa serikali anapofananisha usafiri uliopo Japan na hali itakavyokuwa Dar es Salaam, tunaona ni sawa? Je, anaweza kutuambia miundo mbinu ya Japan ni sawasawa na ya Dar? au atuambie ni katika eneo gani ambalo sisi tunaweza kujivunia kuwa tupo sawasawa na Japan?
Ni vema serikali iwe regulatory hasa na wala sio mfanyabiashara. Reglatory officer anapoongelea kufufua UDA ninabaki hoi kabisa!!!!
Kwani nini serikali isiratibu shughuli zao na kuwapa uwezo wa kulinda mitaji yao kwa kuwafanya wao ndiyo wawe wadau wakubwa wa hayo makampuni makubwa?
Tuliangalie hili kwa makini sana kwani tusipoangalia sasa tutarudi hapa baadae kupiga kelele baada yakuona kila shida zetu sisi watanzania ni furaha na faraja za wageni na wenzetu wachache.
Hapa umeongea la maana, ila kitu kimoja nikwamba Tanzania kinachotukwamisa ni uongozi mbaya na rushwa.
Hao wenye mitaji yao walichotakiwa nikuingia ubia tu na na mashirika makubwa ambayo yana uhakika, kwahio nao watapata faida kwenye biashara zao.
Hata ulaya mabasi ya Eurolines, matrein wanaingia ubia na kampuni nyingine ndogo au watu wenye mitaji midogo ili kufanikisha lengo lao, na watu wanaziona faida.
Kenya airways wana ubia na mashirika mwengi tu tena yanayojulina kama KLM na faida zake wanaziona.
Kitu chochote hata kama kina ukubwa gani, lakini kama hakina uongozi mzuri na kina rushwa basi ujue kwamba hakitadumu.