Herymiller
JF-Expert Member
- Jul 8, 2018
- 613
- 861
STORY: MANOEUVRE (MANUVA)
MTUNZI: HERY_MILLER
SEASON 01E01
Baada ya purukushani na hekaheka za mapumziko ya mwisho wa wiki ndani ya jiji la Dar es salaam hatimaye majogoo yaliwika kuashiria ni siku mpya, ambayo haipendwi kiivyo na asilimia kubwa ya watu inaitwa jumatatu, tukiacha na utani jamani jumatatu inaboa haijalishi we ni nani, una cheo gani, jumapili ulikua kanisani,nyumbani na familia au maeneo ya starehe kama watoto wa mjini wenyewe wanavyosema "kula bata".
Alarm ilisikika masikioni mwa kijana mmoja mtanashati,bila kupoteza muda aliamka kitandani nakuelekea kwenye chumba chake maalumu cha mazoezi,kama kawaida ya vijana wa kileo alichukua simu yake na kupitia maeneo muhimu ku like,comment na kujibu ujumbe wa maandishi katika mitandao ya kijamii facebook,twitter na Instagram.
Mguu wa kiume uliingia ndani ya airmax na kupendeza kiroho mbaya, wakati ule upaja uliojikatakata ulivaliwa na bukta fupi kidogo na kumfanya aonekane shupavu kwa jinsi misuli yake ilivyo inyanyasa bukta ile, kile kifua kilicho jigawa katikati na kujaaliwa misuli iliyo nyumbulika na kutengeneza matuta madogo madogo juu ya tumbo (six packs) ukijumlisha na mbavu nene zilizo beba kifua hicho zilikaa kwenye vest moja maridadi iliyokua na maandishi haya "Chicago bull's "na kuifanya mikono ya yake iweze kuwa huru kufanya shughuli zake kikamilifu.
Aliwasha redio na kucheza mtiririko wa nyimbo zake tano(playlist) ambazo hupenda kazisikiliza akiwa anafanya mazoezi( Lituation-fabulous,Many men-50,like a boy-ciara,Dirty off ur shoulder -jay z,Topback- T.I)
Mashine ya kukimbilia ilisoma kilomita 1.5 ndipo alipohamia kwenye pushup 150 akamalizia na squash 70 kabla ya ya kunyanyua chuma mara 100 kwa mikupuo 10.
Kijasho chembamba kilimchurizika mtoto wakiume taaratibu alielekea bafuni kuoga, kutokana na uzito wa siku ile katika maisha yake ya kazi ilibidi awe nadhifu kuliko kawida, ilikuwa hamna namna ndipo alipoamua chukua suti(black label) iliyotengenezwa na mbunifu nguli wa mitindo ya mavazi hapa mjini kwa sasa @ mtani_ be _spoken, chini alivalia travota ya kisigino kifupi inayofungwa kwa zipu pembeni aliyo inunua pale@born 2 shine, Pete yenye mng'aro hatari wa dhahabu kidoleni ,kidani cha madini ya tanzanite(bleclet) mkono wa kulia wakati mkono wa kushoto uling'arshwa na saa yenye rangi ya dhahabu(g-shok), laiti kama kile kioo kingeweza kusema basi kingeomba msamaha maana taswira ya mtu aliyekua anakitumai alikua amependeza kupita jinsi ambayo naweza kukusimulia.
Alipomaliza kujiandaa aliingia kwenye gari lake tayari kwa kuelekea kazini huku moyo ukimdunda dunda kwa sababu alikua anakwenda kwenye kikao ambacho mawazo yake yeye binafsi yanaweza kuja kuathiri maisha ya watu wanao mzunguka na shirika kwa ujumla.
"Deutsche mark" ni jina la shirika la kimataifa lililo anzishwa nchini ujerumani na kufungua matawi katika nchi mbalimbali ulimwenguni,shirika linajishughulisha na kuhifadhi nyara za kihistoria za utawala wa kijerumani kipindi cha ukoloni na kufanya utafiti wambo ya kale,hayo yote yanafanyika chini ya mwamvuli wa sheria ushirikiano wa kimataifa ya umoja wa mataifa.
Majira ya saa mbili asubuhi ndani ukumbi wa mikutano ya ofisi,watu walianza kuingia na kuchua nafasi zao wakisubiri kinacho endelea, nyuso za sitofahamu na bashasha ziliendelea kukinzana mbele ya mapaji ya nyuso zao hatimaye muda uliwadia mkurugenzi aliingia na kuchukua nafasi yake na kikao kikaanza rasmi.
Baada ya salamu na kila mtu kujitambulisha mkurugenzi alitakiwa kuwasilisha mada ili ijadiliwe na kutafutiwa ufumbuzi
"Kwa majina naitwa Herman muller mkurugenzi wa shirika hili hapa nchini Tanzania, nawaombeni mtege masikio yenu vizuri na mnisikilize sio muishie kunitumbulia macho tu (hahahahahahaha) alicheka kidogo, najua leo nimependeza sana ninawashukuru kwa kunisifia pia asante sana naomba niwasilishe mada kama ifuatavyo……
Baada ya mkutano wa berlin (1884-85) Africa mashariki ilikua chini ya utawala wa wajerumani ilitawaliwa kwa mfumo wa majimbo, kuimarisha mfumo wa utawala kila gavana alipewa jimbo lake la kuliongoza, tukirudi nyuma zaidi kabla ya mkutano wa berln ulifanyika utafiti(survey)kwa ajili ya kukagua na kupima maeneo yenye rasilimali ndani ya afrika ili itengenezwe ramani ambayo ingeonyesha maeneo yote, mipaka na rasilimali zake ndani ya africa. Ramani hyo ilipewa jina la skelett,kila nchi tawala ilipewa skelett yake. Baada ya wajerumani kupewa skelett yao waliamua kupunguza hatari ya kuweka mayai yote katika kapu moja(risk) kwa kutengeneza ramani nyingine ambazo zinaonyesha kila jimbo pekeyake na gavana wa jimbo ndiye aliyepewa mamlaka ya kuilinda na kuhifadhi, ili kuhakikisha siri inaendelea kuwepo wote waliousika kutengeneza ramani za majimbo waliuwa na ramani zikabaki mikononi mwa magavana, ziliandaliwa karatasi maalum za kuchorea ramani kwa ustadi wa hali ya juu waliweza kutengeneza picha ambayo inayesha sura ya gavana wa jimbo husika lakini picha ikielekezwa kwenye mwanga inaonyesha ramani ya jimbo.
Baada ya ujerumani na washirika wake kushindwa katika vita ya kwanza ya dunia makoloni yake yalichukuliwa na waingereza, kila gavana wa kijerumani ambaye hakufanikiwa kuirudisha ramani berln aliificha alipoona panafaa.………
Herman baada ya kumaliza kusoma alichokiandaa alikunywa glasi moja ya maji huku akiwaangalia wafanyakazi wake waliokuwa wanamsikiliza kwa makini, kabla haja endelea mlango ulifunguliwa na aliingia binti mbichiiiiii aliyekuwa amependeza na kuvalia viwalo vya hatari guu la shampeni ndani ya mchuchumio wa rangi nyekundu(high hills),mini sketi nyeusi ilionyesha sentimita kiduchu za upaja mtamu unao anza kuichora figa iliyo unganishwa na nyonga iliyoifanya sketi ivimbe kama mimba ya panya, zigoo sasa kajaaliwaa mashalaaaah lakini sio sana maana sana inaboa,juu alivaa kikoti cha suti za kiofisi ambacho kwa mbele ilivaliwa na skafu kuziba uwazi uliokua unasababisha sehemu kubwa ya utamu wa vifuu vya nazi kuonekana na kuzidisha gharika na kuwatoa udenda vidude, hatua kadhaa za madaha hatimaye mtoto mzuri alikaa kwenye kiti ………
"binti jitambulishe na utueleze kwanini umechelewa kwenye kikao muhimu cha kampuni "Herman akiongea maneno hayo kwa sauti ya ukali kidogo
"kwa majina naitwa gwantwa nyakababi ni mwajiliwa mpya wa shirika hili pia mtaalam wa lugha na alama zinazotumika katika mawasilano ya lugha,naongea kiswahili,kiingereza, kifaransa kijerumani,kirusi na kiitaliano kwa ufasaha, kichina na lugha zingine za mashariki ya mbali nazifahamu lakini sio vizuri sana bado nazifanyia kazi na kuhusu kuchelewa hapa ni katikati ya mji kunafoleni sana naomba msamaha naombeni mnisamehe"
"binti unaitwa gwantwa sio kila sehemu kuna sheria zake hivyo basi tuache tumalizie kikao chetu siku nyingine kukiwa hakuna foleni ukiwahi kufika mapema tutajumuika pamoja"
Kinyonge kabisa binti wa watu alitoka nje ya ukumbi wa mkutano akiwa hana raha hata chembe huku akieleke ofisini kwake kuendele na shughuli zake za kila siku.
"kama tulivyo kubaliana kuwa shirika letu litaendeshwa kwa misingi ya sheria tulizo jiwekea,
Haya tuachana na hayo turudi kwenye mada yetu, kwa gharama yoyote ile inabidi tuzipate hizo ramani(skelett) ilituweze kutimiza malengo tulio jiwekea kila mtu atumie uwezo na nafasi aliyonayo ilituweze kupata taarifa sahihi kabla ya kuanzisha oparesheni(field mission) kutona na unyeti wa suala tunalolifanya kwa sasa wafanyakazi wote ambao wanahusika katika mpango huu hatatumia tena mfumo wa mawasiliano ya kawaida badala yake watatumia mfumo mpya unaoitwa enigma toleo la teknolojia mpya ukiachana na ule ulichakachuliwa na Alan Turing wakati ya vita kuu ya pili ya dunia, hiyo yote ni kwa sababu ya kulinda usalama wetu na sifa ya shirika kwa ujumla naamini kila mtu amenielewa leo sihitaji maswali natoa siku tano tuu natakila mtu awe na majibu yanayo eleweka na ushahidi wa kile anacho kieleza"
Aliongena kiingereza ili kuonyesha msisitizo kidogo kabla hajawarusuhu waende
"our primary target is to secure the skelett and I don't think if we have other alternative than to put all our assets on play..."
asanteni sana kwa kunisikiliza mnaweza kwenda sasa.
………Itaendelea usikose......
MTUNZI: HERY_MILLER
SEASON 01E01
Baada ya purukushani na hekaheka za mapumziko ya mwisho wa wiki ndani ya jiji la Dar es salaam hatimaye majogoo yaliwika kuashiria ni siku mpya, ambayo haipendwi kiivyo na asilimia kubwa ya watu inaitwa jumatatu, tukiacha na utani jamani jumatatu inaboa haijalishi we ni nani, una cheo gani, jumapili ulikua kanisani,nyumbani na familia au maeneo ya starehe kama watoto wa mjini wenyewe wanavyosema "kula bata".
Alarm ilisikika masikioni mwa kijana mmoja mtanashati,bila kupoteza muda aliamka kitandani nakuelekea kwenye chumba chake maalumu cha mazoezi,kama kawaida ya vijana wa kileo alichukua simu yake na kupitia maeneo muhimu ku like,comment na kujibu ujumbe wa maandishi katika mitandao ya kijamii facebook,twitter na Instagram.
Mguu wa kiume uliingia ndani ya airmax na kupendeza kiroho mbaya, wakati ule upaja uliojikatakata ulivaliwa na bukta fupi kidogo na kumfanya aonekane shupavu kwa jinsi misuli yake ilivyo inyanyasa bukta ile, kile kifua kilicho jigawa katikati na kujaaliwa misuli iliyo nyumbulika na kutengeneza matuta madogo madogo juu ya tumbo (six packs) ukijumlisha na mbavu nene zilizo beba kifua hicho zilikaa kwenye vest moja maridadi iliyokua na maandishi haya "Chicago bull's "na kuifanya mikono ya yake iweze kuwa huru kufanya shughuli zake kikamilifu.
Aliwasha redio na kucheza mtiririko wa nyimbo zake tano(playlist) ambazo hupenda kazisikiliza akiwa anafanya mazoezi( Lituation-fabulous,Many men-50,like a boy-ciara,Dirty off ur shoulder -jay z,Topback- T.I)
Mashine ya kukimbilia ilisoma kilomita 1.5 ndipo alipohamia kwenye pushup 150 akamalizia na squash 70 kabla ya ya kunyanyua chuma mara 100 kwa mikupuo 10.
Kijasho chembamba kilimchurizika mtoto wakiume taaratibu alielekea bafuni kuoga, kutokana na uzito wa siku ile katika maisha yake ya kazi ilibidi awe nadhifu kuliko kawida, ilikuwa hamna namna ndipo alipoamua chukua suti(black label) iliyotengenezwa na mbunifu nguli wa mitindo ya mavazi hapa mjini kwa sasa @ mtani_ be _spoken, chini alivalia travota ya kisigino kifupi inayofungwa kwa zipu pembeni aliyo inunua pale@born 2 shine, Pete yenye mng'aro hatari wa dhahabu kidoleni ,kidani cha madini ya tanzanite(bleclet) mkono wa kulia wakati mkono wa kushoto uling'arshwa na saa yenye rangi ya dhahabu(g-shok), laiti kama kile kioo kingeweza kusema basi kingeomba msamaha maana taswira ya mtu aliyekua anakitumai alikua amependeza kupita jinsi ambayo naweza kukusimulia.
Alipomaliza kujiandaa aliingia kwenye gari lake tayari kwa kuelekea kazini huku moyo ukimdunda dunda kwa sababu alikua anakwenda kwenye kikao ambacho mawazo yake yeye binafsi yanaweza kuja kuathiri maisha ya watu wanao mzunguka na shirika kwa ujumla.
"Deutsche mark" ni jina la shirika la kimataifa lililo anzishwa nchini ujerumani na kufungua matawi katika nchi mbalimbali ulimwenguni,shirika linajishughulisha na kuhifadhi nyara za kihistoria za utawala wa kijerumani kipindi cha ukoloni na kufanya utafiti wambo ya kale,hayo yote yanafanyika chini ya mwamvuli wa sheria ushirikiano wa kimataifa ya umoja wa mataifa.
Majira ya saa mbili asubuhi ndani ukumbi wa mikutano ya ofisi,watu walianza kuingia na kuchua nafasi zao wakisubiri kinacho endelea, nyuso za sitofahamu na bashasha ziliendelea kukinzana mbele ya mapaji ya nyuso zao hatimaye muda uliwadia mkurugenzi aliingia na kuchukua nafasi yake na kikao kikaanza rasmi.
Baada ya salamu na kila mtu kujitambulisha mkurugenzi alitakiwa kuwasilisha mada ili ijadiliwe na kutafutiwa ufumbuzi
"Kwa majina naitwa Herman muller mkurugenzi wa shirika hili hapa nchini Tanzania, nawaombeni mtege masikio yenu vizuri na mnisikilize sio muishie kunitumbulia macho tu (hahahahahahaha) alicheka kidogo, najua leo nimependeza sana ninawashukuru kwa kunisifia pia asante sana naomba niwasilishe mada kama ifuatavyo……
Baada ya mkutano wa berlin (1884-85) Africa mashariki ilikua chini ya utawala wa wajerumani ilitawaliwa kwa mfumo wa majimbo, kuimarisha mfumo wa utawala kila gavana alipewa jimbo lake la kuliongoza, tukirudi nyuma zaidi kabla ya mkutano wa berln ulifanyika utafiti(survey)kwa ajili ya kukagua na kupima maeneo yenye rasilimali ndani ya afrika ili itengenezwe ramani ambayo ingeonyesha maeneo yote, mipaka na rasilimali zake ndani ya africa. Ramani hyo ilipewa jina la skelett,kila nchi tawala ilipewa skelett yake. Baada ya wajerumani kupewa skelett yao waliamua kupunguza hatari ya kuweka mayai yote katika kapu moja(risk) kwa kutengeneza ramani nyingine ambazo zinaonyesha kila jimbo pekeyake na gavana wa jimbo ndiye aliyepewa mamlaka ya kuilinda na kuhifadhi, ili kuhakikisha siri inaendelea kuwepo wote waliousika kutengeneza ramani za majimbo waliuwa na ramani zikabaki mikononi mwa magavana, ziliandaliwa karatasi maalum za kuchorea ramani kwa ustadi wa hali ya juu waliweza kutengeneza picha ambayo inayesha sura ya gavana wa jimbo husika lakini picha ikielekezwa kwenye mwanga inaonyesha ramani ya jimbo.
Baada ya ujerumani na washirika wake kushindwa katika vita ya kwanza ya dunia makoloni yake yalichukuliwa na waingereza, kila gavana wa kijerumani ambaye hakufanikiwa kuirudisha ramani berln aliificha alipoona panafaa.………
Herman baada ya kumaliza kusoma alichokiandaa alikunywa glasi moja ya maji huku akiwaangalia wafanyakazi wake waliokuwa wanamsikiliza kwa makini, kabla haja endelea mlango ulifunguliwa na aliingia binti mbichiiiiii aliyekuwa amependeza na kuvalia viwalo vya hatari guu la shampeni ndani ya mchuchumio wa rangi nyekundu(high hills),mini sketi nyeusi ilionyesha sentimita kiduchu za upaja mtamu unao anza kuichora figa iliyo unganishwa na nyonga iliyoifanya sketi ivimbe kama mimba ya panya, zigoo sasa kajaaliwaa mashalaaaah lakini sio sana maana sana inaboa,juu alivaa kikoti cha suti za kiofisi ambacho kwa mbele ilivaliwa na skafu kuziba uwazi uliokua unasababisha sehemu kubwa ya utamu wa vifuu vya nazi kuonekana na kuzidisha gharika na kuwatoa udenda vidude, hatua kadhaa za madaha hatimaye mtoto mzuri alikaa kwenye kiti ………
"binti jitambulishe na utueleze kwanini umechelewa kwenye kikao muhimu cha kampuni "Herman akiongea maneno hayo kwa sauti ya ukali kidogo
"kwa majina naitwa gwantwa nyakababi ni mwajiliwa mpya wa shirika hili pia mtaalam wa lugha na alama zinazotumika katika mawasilano ya lugha,naongea kiswahili,kiingereza, kifaransa kijerumani,kirusi na kiitaliano kwa ufasaha, kichina na lugha zingine za mashariki ya mbali nazifahamu lakini sio vizuri sana bado nazifanyia kazi na kuhusu kuchelewa hapa ni katikati ya mji kunafoleni sana naomba msamaha naombeni mnisamehe"
"binti unaitwa gwantwa sio kila sehemu kuna sheria zake hivyo basi tuache tumalizie kikao chetu siku nyingine kukiwa hakuna foleni ukiwahi kufika mapema tutajumuika pamoja"
Kinyonge kabisa binti wa watu alitoka nje ya ukumbi wa mkutano akiwa hana raha hata chembe huku akieleke ofisini kwake kuendele na shughuli zake za kila siku.
"kama tulivyo kubaliana kuwa shirika letu litaendeshwa kwa misingi ya sheria tulizo jiwekea,
Haya tuachana na hayo turudi kwenye mada yetu, kwa gharama yoyote ile inabidi tuzipate hizo ramani(skelett) ilituweze kutimiza malengo tulio jiwekea kila mtu atumie uwezo na nafasi aliyonayo ilituweze kupata taarifa sahihi kabla ya kuanzisha oparesheni(field mission) kutona na unyeti wa suala tunalolifanya kwa sasa wafanyakazi wote ambao wanahusika katika mpango huu hatatumia tena mfumo wa mawasiliano ya kawaida badala yake watatumia mfumo mpya unaoitwa enigma toleo la teknolojia mpya ukiachana na ule ulichakachuliwa na Alan Turing wakati ya vita kuu ya pili ya dunia, hiyo yote ni kwa sababu ya kulinda usalama wetu na sifa ya shirika kwa ujumla naamini kila mtu amenielewa leo sihitaji maswali natoa siku tano tuu natakila mtu awe na majibu yanayo eleweka na ushahidi wa kile anacho kieleza"
Aliongena kiingereza ili kuonyesha msisitizo kidogo kabla hajawarusuhu waende
"our primary target is to secure the skelett and I don't think if we have other alternative than to put all our assets on play..."
asanteni sana kwa kunisikiliza mnaweza kwenda sasa.
………Itaendelea usikose......