Sekretarieti ya Ajira Muogopeni Mungu

Sekretarieti ya Ajira Muogopeni Mungu

hekimanyingi

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
679
Reaction score
573
Nasikitika kusema sekretarieti ya ajira imekuwa ni janga la wasaka ajira. Nilikuwa siamini nilipokuwa nikiambiwa na sasa nimekubali kuwa hawa jamaa ni genge tena genge la watu wanaofanya kazi kindugu, kwa rushwa na kwa kujuana. Watoto wa maskini wanapewa kazi za TGS D zile zenye mishahara mirefu wanapewa wanaowajuwa wao. Leo hii sishangai kuona watoto wa maskini wanapangiwa sitimbi yaani mbali na mjini wa vigogo wanawekwa pale magogoni. Yaani inasikitisha sana. Mliibia watu kazi za PPRA mmeiba kazi za AG na sasa juzi mmeiba kazi za GPSA na nyingine nyingi tu, najua keshokutwa mnapanga kugawana kazi za TANROADS Mungu atawalaani. Kama kweli nyie wema mngekuwa mnarudisha karatasi au kutoa nafasi ya mtu kukata rufaa kama msingeumbuka. Nashauri serikali iunde chombo cha kuwasimamia hawa jamaa au kama kipo ujue kimekufa. Pale Chuo cha uhasibu Arusha (IAA) waliita watu kwaajili ya usahili mwezi januari cha kushangaza walikuwa na vijana wao waliosoma pale tayari walikuwa intern na ndiyo waliwapa kazi na wengine watoto wa waalimu wa pale mpaka majina tunayo tukanyamaza sasa mnataka kufanya kama idara za serikali ni mali yenu. Hamna huruma na watoto wa maskini wanaotoka Bukoba, Ukerewe, Rorya, Musoma, Kigoma na Songea? wanaharibu hela mnakuja kuwaonea. Inaudhi sana.
 
mh me siamini kwa sababu mimi pia nimepata barua kuitwa kazin kwa AG na nakuhakikishia simjui mtu wala sikutoa hela tena intavyu niliingia wa kwanza katika panel yangu
 
mbona hiyo imekuwa kawaida kwa hao wanaojiita sekretariet ya ajira. wanatangaza kazi kupumbaza taifa. Mi nimeshuhudia mtu kaajiriwa chuo cha Maji DSM position inatangazwa baadae. Nampigia we vipimo mbona nimeona tangazo la kazi unayofanya wewe? Jibu language ni kwamba acha hayo mambo ya chini ya kapeti. Mda si mrefu ananipa kazi ya kumtengenezea presentation kwa power point nampangia kumbe kashapewa na maswali siku ya interview ye anawatazama kama spea tyre kwa kweli aliponiambia nilikuwa nafanyia interview niliumia sana.
 
Wabongo kwa malalamiko mna PhD za kutosha! Nilifanya PPRA nikakosa ila jamaa yangu kapata! Zamani kabla sijapata kazi kwa kupitia utumishi nilikuwa kama wew ila pale ni full Haki kijana. Wakikuita jiandae darasani maana wanafanya ushindani kwa maswali ya Darasani

Punguza hasira maana wakati wewe unalia wenzako wanacheka kwa kupata kazi bila kuwa na mtu! Muombe Mungu one day will be Yes
 
Ni shida hii hali itaisha lini? Kila siku tumekuwa wasindikizaji tu.
 
Tehhhhhhhhhhhh mi nimelalamika sana ila kwa sasa nimechoka maana hakuna jinsi

acha aliyeshika mpini akukate nao
 
NILIOMBA TANROAD ,transport economist, na TAA, airport opération office , sijuh watu wameishakalia viti maana sijaitwa licha yakuwa na vigezo vyoote.
 
Hili la watt wa maskin kutupiwa TGS D NI KWELI KABISAAAA
UKIONA MASKN KAANGUKIA MISHAHARA MINONO ujue hakukua na mhtaj zaid kwa kund lile la HAVES
 
Hamna huruma na watoto wa maskini wanaotoka Bukoba, Ukerewe, Rorya, Musoma, Kigoma na Songea? wanaharibu hela mnakuja kuwaonea. Inaudhi sana.[/QUOTE]

Mie sikubalini na wewe!! mie niko Ukerewe na mwanangu kapata kazi na wala simjui mtu wala Dar sipajui.
 
Ukiponda kuwa PSRS they are not fair basi acha kuomba kazi za serikalini, maana kwa Imani yangu ndiyo taasisi pekee ambayo wanatumia vigezo vya mtu na kushindanishwa sawa mpaka kupangiwa kituo cha kazi. The rest in kweli bila memo hakuna kitu mfano mzuri TRA na ndugu zake hao.
 
ACHA UJINGA WEWE RIZIKA ATA HICHO KIDOGO UNACHOPATA WEWE, asiye shiba kwa kijiko ata kwa sahani hatashiba.
 
mh me siamini kwa sababu mimi pia nimepata barua kuitwa kazin kwa AG na nakuhakikishia simjui mtu wala sikutoa hela tena intavyu niliingia wa kwanza katika panel yangu

Kweli hyo inawezekana
Bt ktk 20 anatokea km ww 1
...si wengine Mungu tu
 
Nyie mnaobisha Shukuruni Mungu tu kuwa mmepata lkn ukweli utabaki palepale
 
Back
Top Bottom