Chief-Mkwawa
Platinum Member
- May 25, 2011
- 32,225
- 44,218
Kwa heshima ya jukwaa hili, na uchangiaji wako, nipe specs zote za motherboard unayoitaka nitakutumia in 3 weeks. Huku kwetu zipo nyingi sana na ndio mchezo wa high school kids.nakumbuka kulikua na thread kama hii nimeitafuta sijaipata, kama ipo mods mtaziunganisha.
muda mrefu nimekuwa nikitafuta madukani vifaa vya computer ambavyo mtu ataweza mwenyewe kutengeneza computer inayokidhi mahitaji yake. vifaa hivyo ni kama
-processor(cpu)
-ram
-graphic processor (gpu)
-hard disk
-motherboard
-power supply
-case
ram, hdd na power supply ni rahisi na vinapatikana maduka mengi, kazi kubwa ikawa ni kupata cpu, case, gpu na motherboard.
watu wengi huwa integrated gpu inayokuja na cpu inatosha na case unaweza tumia hata za computer ya zamani hivyo challenge kubwa ikawa kwenye kupata cpu na motherboards.
baada ya kuhangaika sana nikapata duka la cpu ambalo jamaa alikua hadi na i7 4770 kwa dola 325 pamoja na pentium za g series kwa 50,000 tu. cpu hizi ni za haswell aka 4th generation ndio latest kwa sasa duniani.
motherboard nimetafuta sana nimekosa madukani. motherboard za haswell zinatakiwa ziwe na support ya lga 1150. ikiwa ni h81 itakuwa nzuri zaidi ila ikiwa h85 au z97 pia sio mbaya.
je kuna mtu yoyote aliekumbana na duka linalouza motherboard??
au kuna ambaye kafanikiwa kutengeneza pc kwa kununua vifaa hapa hapa tz?
Kwa heshima ya jukwaa hili, na uchangiaji wako, nipe specs zote za motherboard unayoitaka nitakutumia in 3 weeks. Huku kwetu zipo nyingi sana na ndio mchezo wa high school kids.
Poa, hamna tatizo.kaka lengo ni kuwakomboa watu na zile core 2 duo za mwaka 2006 ambazo desktop zake zinauzwa kwenye asilimia 99 ya maduka ya kwetu.
ingekua vizuri hii assignment kama ingekamilika hapa hapa tanzania ili kila mtu afaidike.
na nashukuru kwa kujali nikiwa na mpango wa kutengeneza nitakutafuta kaka.
Mkuu, hilo duka linalouza hizo processor liko maeneo gani? Nina workstation yangu nataka nibadili Processor.
Kuna jamaa yangu mmoja yeye ukimwambia kununua computer full set anaona kama wamtusi, amekuwa aki build pc zake kwa kuunga unga, parts nyingi amekuwa akipata kariakoo ila ni used ones kuanzia Ram, Processor, Motherboard (dukani), graphics card na PSU, na hivi karibuni amefunga machine ya core i5 third gen 3.4ghz, Ram 8GB DDR3 Graphics card ATI 7.X.X series 2GB, PSU 350W ila parts karibu zote ni used alinunua kwa bei poa tu kasoro motherboard, nitamuuliza upatikanaji wa vitu hivyo kwa faida ya wengi.
Na hii ni windows experience base score ya pc yake
View attachment 238775
Hapa akipata SSD na aki upgrade Graphics card atakuwa gaming rig moja makini sana.
Mkuu, hilo duka linalouza hizo processor liko maeneo gani? Nina workstation yangu nataka nibadili Processor.
Kwa processor za workstation sidhani kama utapata kwa urahisi, workstation nyingi kama sio zote zinatumia processor za Xeon ambazo ni ghali sana kama utapata mpya dukani. Kama ulinunua workstation used kwenye haya maduka yetu bongo ni rahisi kupata spare processor huko kuliko maduka yanayouza pc accessories mpya.
h120 yah kweli hapo ssd na hata gtx 750ti inakuwa machine ya maana.
ila kama ni 3rg generation (ivy bridge) motherboard zake hazitaingiliana na 4th (haswell).
ila pia sio mbaya ukinipatia adress na mi nkatembelea
Haya...karib tenaSijaelewa chochote, napita tu wajameni...
unajua thread ya mwaka gani hii ?Duh NASIKITIKA SANA nyie ndio wadau wakubwa tunaowategemea kwenye jukwaa hili kwa habari PC and computerized technology hii habari ya ku assemble Computer Its very minor Issue kwa materials mnayoyatoa kila siku kwenye michango yenu, Nahisi lazima pana stage mliluka hamkuisoma vizuri au ndio hali ya kujiongeaza tu na kuelelwa vitu vingi through PRACTICAL without relevant Theories, Naomba mniwie radhi kama nitawa kwaza.
Njia bora niliyokuwa naitumia huko nyuma more than ten yrs back ni kuagiza online kila kitu utapata na siku hizi imekuwa rahisi sana kuagiza na kulipa yafuatayo ni baadhi tu ya makampuni nadhani bado yapo :
MAPLIN ELECTRONICS , RS COMPONENTS , CPC Electronics na mengine mengi nikiyakumbuka nitayaongeza
Pia siku hizi kuna ALBABA (sijawahi kuwatumia)
Okay sorry nimekuelewaunajua thread ya mwaka gani hii ?