ndatama
Member
- Jul 18, 2015
- 10
- 4
Kuelekea Uchaguzi Mkuu, nahisi waigizaji wa filamu za kibongo itabidi wapumzike kwa muda ili tutazame hizi sinema za wanasiasa.
Maigizo ya CHADEMA yanaanza pale walipomuita Lowassa in mwizi, fisadi na ni furaha ya Mungu kumzomea.
Wakaja wakamuhusisha na ACT -Wazalendo, hii ikawa zaidi haswa hadi kumpa udhamini wa ACT -Wazalendo.
Wakaja na habari Zitto kamfuata Lowassa Dodoma kumshawishi ajiunge ACT -Wazalendo, kumbe ni Mbowe na ujumbe wake waliokua Dodoma na Lowassa.
Yapo mengi sana yanayofanywa kisinema na CHADEMA haswa wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Kikubwa Leo ni yule mdhamini mkuu wa ACT -Wazalendo, anayeonekana kuwaacha aliowapa pesa na kujiunga kwa wale waliokuwa wakimtusi. Mbowe, hebu funza vijana zako nidhamu na akiba ya maneno.
Leo wanamlilia Lowassa na wameanza kuutilia shaka uwezo was Slaa. Hawa CHADEMA hii sinema wanayocheza inaudhi; ni ya kinafiki, imejaa usaliti na uasi.
Ndatama Mafuru
Maigizo ya CHADEMA yanaanza pale walipomuita Lowassa in mwizi, fisadi na ni furaha ya Mungu kumzomea.
Wakaja wakamuhusisha na ACT -Wazalendo, hii ikawa zaidi haswa hadi kumpa udhamini wa ACT -Wazalendo.
Wakaja na habari Zitto kamfuata Lowassa Dodoma kumshawishi ajiunge ACT -Wazalendo, kumbe ni Mbowe na ujumbe wake waliokua Dodoma na Lowassa.
Yapo mengi sana yanayofanywa kisinema na CHADEMA haswa wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Kikubwa Leo ni yule mdhamini mkuu wa ACT -Wazalendo, anayeonekana kuwaacha aliowapa pesa na kujiunga kwa wale waliokuwa wakimtusi. Mbowe, hebu funza vijana zako nidhamu na akiba ya maneno.
Leo wanamlilia Lowassa na wameanza kuutilia shaka uwezo was Slaa. Hawa CHADEMA hii sinema wanayocheza inaudhi; ni ya kinafiki, imejaa usaliti na uasi.
Ndatama Mafuru