Wewe walau unafahamu kinachoendelea.Mo alikuwa hatoi pesa huku akiubana uongozi kwa mikataba yake ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa inamnufaisha yeye. Baada ya kuona hiyo changamoto Mangungu na Try again walikutana na Bakhresa Zanzibar ili wafanye taratibu za kumwondoa mo Kama mwekezaji mpya. Bahati mbaya kwao na nzuri kwa mo alipata habari hivyo mo akaanza kulipa watu waanzishe kuendesha kampeni ya kumwondoa Mangungu na Try again.
Ni muda utaongea.
Subiri wafanikiwe ndio utajua inawezekana au lah!Makolo washapoteana Hadi wajipate miaka kumi tayari,Ila Kuna mahala umetupiga,
1:Tajiri anaishi Uturuki
2:Familia Moja/mtu, au kampuni moja haiwezi Kumiliki Timu zaidi ya moja Ligi moja
Sheria ya FIFA hiyo,Kuna kipindi Redbull Salzburg ya Austria na RB Leipzig ya Ujerumani zilizuiwa kushiriki UEFA coz mmiliki mmoja,waliambiwa wachague timu moja ya kwenda...Subiri wafanikiwe ndio utajua inawezekana au lah!
Nafahamu hilo Mkuu, ila hapa kwetu tunajuana hakuna linaloshindikana.Sheria ya FIFA hiyo,Kuna kipindi Redbull Salzburg ya Austria na RB Leipzig ya Ujerumani zilizuiwa kushiriki UEFA coz mmiliki mmoja,waliambiwa wachague timu moja ya kwenda...
Hapo nimekuelewa,Kuna timu inahusishwa na Waziri wa maokoto Ila kwenye makaratasi hayupo,Ila kambi ya timu tunamuona dailyNafahamu hilo Mkuu, ila hapa kwetu tunajuana hakuna linaloshindikana.
Anaweza kuonekana mmiliki mwingine kwenye makaratasi ila kiuhalisia ni SSB.
Naam, sasa tunaongea lugha moja.Hapo nimekuelewa,Kuna timu inahusishwa na Waziri wa maokoto Ila kwenye makaratasi hayupo,Ila kambi ya timu tunamuona daily
Namkumbuka,,akaondoka Tanzania Ila ujio wake si haba,Kaondoka na Gadiel Michael kamagi now anazima mbavu ya kushoto Ajax Cape Town,na mwalimu yule yule,utanikumbusha jina mkuuNaam, sasa tunaongea lugha moja.
Acha tu kuwa kambi ya timu, hadi anaingilia maamuzi ya benchi la ufundi. Unakumbuka kuna kocha aliondoka akasema anaingiliwa kwenye maamuzi yake ya kupanga kikosi?
View attachment 2966280
Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Mhene ‘Try Again’ dhidi ya ‘Rais wa heshima’ wa Simba Mohamed ‘Mo’ Dewj.
Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.
Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeahaji timu Try Again ambao ulimuelemea!
Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya ‘tajiri’ kujitenga ‘kiaiana’, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikizaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.
Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again ‘kususiwa’ timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!
Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na ‘mbambamba’ S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)
Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.
Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujidhihirisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.
Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato huo uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.
Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…
Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.
Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu ‘nono’ kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.
Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.
Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia ‘janja janja’ kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa ‘kuwachonganisha’ na muewekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mkurugenzi wa bodi ya wawekezaji ambaye alijiengua Nkwabi.
Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ‘ujanja wa mjini’ kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!
Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na ‘connection’ za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao ‘umetiki’.
Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni ‘watoto wa mjini’ Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?
Ni mimi na chanzo changu nyeti,
Nifah.
Hii habari kuna mwamba jana tu kaniambia nikampuuza sijui kama kuna ukweli ila sasa ngoja nichimbe zaidi ipo namna hapa!
Hahahahaha..salute Nifah ..hii unayosema ni jana tu nimegusiwa ..mdada now nitaanzq kukuamini uko vzr una sourceView attachment 2966280
Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Mhene ‘Try Again’ dhidi ya ‘Rais wa heshima’ wa Simba Mohamed ‘Mo’ Dewj.
Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.
Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeahaji timu Try Again ambao ulimuelemea!
Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya ‘tajiri’ kujitenga ‘kiaiana’, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikizaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.
Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again ‘kususiwa’ timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!
Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na ‘mbambamba’ S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)
Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.
Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujidhihirisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.
Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato huo uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.
Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…
Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.
Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu ‘nono’ kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.
Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.
Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia ‘janja janja’ kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa ‘kuwachonganisha’ na muewekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mkurugenzi wa bodi ya wawekezaji ambaye alijiengua Nkwabi.
Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ‘ujanja wa mjini’ kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!
Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na ‘connection’ za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao ‘umetiki’.
Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni ‘watoto wa mjini’ Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?
Ni mimi na chanzo changu nyeti,
Nifah.
Vipi Singida black star na yanga mdhamini kuwa mmiliki hiyo Sheria haihusiki.Sheria ya FIFA hiyo,Kuna kipindi Redbull Salzburg ya Austria na RB Leipzig ya Ujerumani zilizuiwa kushiriki UEFA coz mmiliki mmoja,waliambiwa wachague timu moja ya kwenda...
Umeongea kitu cha msingi sana Mkuu. Wewe fikiria endapo mchakato mpya ukianzishwa Dewj gharama zote alizotumia kuendesha timu atakuwa kapoteza, pesa pekee atakayorudishiwa ni ile aliyotoa kwenye kununua hisa pekee!Hivi sera na Dira ya michezo ya hapa Nchini ni nani anajukumu la kuitunga? nafikiri mkakati uwe kwenye sera ili kupunguza utegemezi kwa mtu na kuziweka hizi timu zetu ktk kujiendesha zeneyewe. Mimi ni mshabiki wa Simba na ni mmoja wa mashabiki nao tegemea Simba kufanya vyema ktk michezo yake lakini kikwazo ni uendeshaji wa Timu inafika mahala huelewi nini kimeikuta timu kiasi cha kukosa mwelekeo.
Ina dalili zote za ukweli. Anyway SSB ni bora mara 100 kuliko MoDewji. Aje tuView attachment 2966280
Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Mhene ‘Try Again’ dhidi ya ‘Rais wa heshima’ wa Simba Mohamed ‘Mo’ Dewj.
Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.
Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeahaji timu Try Again ambao ulimuelemea!
Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya ‘tajiri’ kujitenga ‘kiaiana’, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikizaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.
Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again ‘kususiwa’ timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!
Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na ‘mbambamba’ S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)
Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.
Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujidhihirisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.
Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato huo uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.
Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…
Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.
Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu ‘nono’ kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.
Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.
Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia ‘janja janja’ kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa ‘kuwachonganisha’ na muewekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mkurugenzi wa bodi ya wawekezaji ambaye alijiengua Nkwabi.
Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ‘ujanja wa mjini’ kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!
Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na ‘connection’ za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao ‘umetiki’.
Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni ‘watoto wa mjini’ Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?
Ni mimi na chanzo changu nyeti,
Nifah.
Bado kuna swala la uuzaji wa jezi hauna ukaguzi wowote wala maelezo ya timu inafaidika vipi ktk mauzo hayo. Ujanja huu unatufanya tuwe tegemezi kwa kila nyanja iwe usajili hata uendeshaji wa timu unamtegemea mtu mmoja ambapo ni jambo la hatari sana kwa maendeleo ya timu.Umeongea kitu cha msingi sana Mkuu. Wewe fikiria endapo mchakato mpya ukianzishwa Dewj gharama zote alizotumia kuendesha timu atakuwa kapoteza, pesa pekee atakayorudishiwa ni ile aliyotoa kwenye kununua hisa pekee!
Na taarifa zinadai Mo na kundi lake la Friends of Simba wanatumika kuihujumu timu ndio maana inafanya vibaya.
Kukudanganya vibaya mnooo Mo ndo aliyemteua Try Again hivo akijua anafanya hayo anao uwezo wa kumtoa mda wowote mtu ambae ungesema anafanya zengwe habar yako iwe na maana labda Ngungu boy pole sana aiseHapana Mkuu, hii sio propaganda ni habari ya ukweli kabisa.
Na huyo mtu ambaye ni chanzo changu ni mwanachama hai wa Simba mwenye access na taarifa za ‘ndani’ huko kwenye klabu yao.
KabisaTry again na mo n mtu na mjomba wake hapo no problem hizo n propaganda