Sakata la Mwigulu na simu feki

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,072
Waziri wa mambo ya ndani sasa tunaomba uwe mstari wa mbele ktk mapambano ya simu feki!

Watanzania wengi wanatarajia kukosa mawasiliano endapo tcra wataamua kuzima simu zote zilizokuwa feki, na hivyo kuleta usumbufu kwa watz walio wengi!

Sasa kuuza bidhaa feki ni kosa katika nchi hii! Kuzima simu tu haiwezi kutosha kuwa ndio tiba ya bidhaa feki, maana zipo pasi feki, deni, nguo, vitasa etc na waingizaji hawatokoma endapo balaa litawakumba watumiaji tu!

Mh. Waziri ambao vimeo vyetu vitakufa naomba tupe ruhusa kuleta malalamiko yetu vituo vya polisi tukiwa na risiti zetu, lengo ni kuwawajibisha waliouza hizo bidhaa, ili nao waone hadha ya kupoteza pesa!

Kuna maduka unaweza ukakuta ndio waliouza labda high percentage ya feki!
Lkn misingi ya nchi inajengwa kwa kusimamia sheria ambapo kuingiza bidhaa feki ni kosa, na sisi consumers hatujalindwa na serikali yenye vyombo maalum kama tbs ambavyo vinaendeshwa kwa kodi yetu ili kitulinda tusiibiwe kwa kupatiwa bidhaa feki!

Serikali hamkutulinda kusimamia uingizaji wa bidhaa feki, badala ya sisi kuwaadhibu nyinyi, then mnatuhukumu kwa kufunga hadi hivyo vimeo vyenyewe!

Tunaomba mh, waziri wa mambo ya ndani tukupe sakata letu hili la simu feki kama ulivyo simamia sakata la wakulima na wafugaji!

Tunajua una uwezo wa kulisimamia hili!
 
Mawazo na maombi mazuri kwa mtazamo wangu, ila kama yamechelewa hivi kuwasilishwa.

Vitu / vifaa feki nchi hii ni kweli vipo vingi sana, na walaji ni sisi sisi raia wa kawaida, na vinapitia mipakani mwetu, bandarini, viwanja vya ndege, na uzuri vinakatiwa / kulipishwa kodi. Sijajua likini, ngoja tushuhudie.

Nimetaka kuchangia hivyo. Japo tukumbushane. Mawazo mazuri kama haya, tuwe tunayatoa mwanzoni kabisa mwa sakata.

Ahsante!
 
Back
Top Bottom