Habari wadau wa JF,
Kuna mdau wa TCRA kanitonya kwamba wametoa order kwa makapuni ya simu kuwawezesha wateja kujua kama NIDA ID yake imetumika kwa zaidi ya namba moja au lah.
Ili kujua unabonyeza *106# kisha usajili wa NIDA (Utaingiza NIDA ID yako), baada ya hapo zitakuja namba zote zilizosajiliwa kwa ID yako ya NIDA. Kama namba haijui siyo yako maana yake wakala (agent) alifanya ujanja kutumia ID yako kusajili line nyingine.
Ukishaona kwenye list namba haijui basi unaenda kwenye shop iliyokaribu nawe unaclaim then Customer care anakuambia uweke finger print kisha hiyo namba inafutwa.
Kutokana na watu wengi kutokuwa na Nida mawakala wengi wanatumia ujanjaujanja wa kusajili line kwa kutumia ID ya mtu mwingine na kuuza hizo line kati ya elfu 5 hadi elfu 20 inategemea watakavyokuona na uhitaji wako.
Mawakala wanafanyaje ujanja? Ukienda kusajili line yako atakwambia uingize kidole baada ya dakika atakwambia network inasumbua hebu ingiza tena basi hapo jua umeumia, ile ya kwanza amesajili line ya mtu mwingine na ya pili anasajili yako, kama haujui hiyo mbinu hauwezi kumstukia maana wapo very smart.
Kwahiyo wote mlionunua line kwa mawakala zilizosajiliwa kwa NIDA mjiandae kisaikolojia.