Rorya hatuna mradi wowote wa maji tokea Uhuru

Rorya hatuna mradi wowote wa maji tokea Uhuru

Gor

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,791
Reaction score
850
Unashangaa hapa Tanzania kuna baadhi ya maeneo wanapewa upendeleo wa kila aina ya mradi lakini kwetu huku Rorya mambo tafrani.

Toka nizaliwe miaka 50 hapa Rorya hatuna maji,hatuna barabara ya lami hata mita 1,ardhi yetu haijapimwa pia tumehathirika na wizi wa mifugo hasa ng'ombe uliokuwa unafanywa na wakurya kwa baraka za serikali ya CCM.

Nasema hivyo kwa sababu serikali hii inajua kuwa jamii ya Kiluo ni jamii ya kifugaji,wakulima sasa tutalima vipi wakati hatuna maksai?

Tunachoomba ni FIDIA MAANA KAZI YA SERIKALI NI KUTULINDA PAMOJA NA MALI YETU.Hivyo nasi tunaomba fidia kama wananchi wa kule Manyara ambao mifugo yao ilikufa na riftvalley fever na kufidiwa kwani hata kwetu huku riftvalley iliua sana mifugo lakini hakuna anayetujali.

Nasi tunataka mgawo wa keki ya taifa kama sehemu zingine.Nimesema kama liwalo na lije.
 
Teh! Teh! Teheee ndugu yangu Gor, tatizo ni viongozi mnaowachagua jimboni kwenu, maana utafiti wangu unaonyesha kuwa 95% ya madiwani ni waganga wa kienyeji, Mbunge ni Darasa la saba 7 na hajawahi ongea wala kutoa au kushinikiza hoja yeyote ndani ya Bunge, ila mnaridhika na Tsh.2000/= Anazowagawia. Mnapanda kile mnachovuna.
 
Back
Top Bottom