Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Gang Chomba upo? Hatimaye ule utabiri kuwa Dogo Geovanni Dos Santos ndiye atakayemrithi Ronaldinho Gaucho umetimia. Dogo huyo ambaya kwa muda mrefu amekuwa akifananishwa na kujifananisha na Ronaldinho jana aliudhihirishia Ulimwengu kuwa yeye ndio Gaucho mpya alipowazungusha Wafaransa huku akiwa amefunga nywele zake kama Dinho. Cha kuvutia zaidi ni kuwa huyu dogo anakaba na kukimbiza kuliko Dinho. Anachotakiwa sasa ni kuongeza tabasamu na kicheko kama Dinho. Naamini mtangazaji wa mechi ya jana, Arsene Wenger, atakuwa ameshaanza taratibu za kumsajili dogo huyu kutoka Galatasaray!