25phiri12
Senior Member
- Jun 19, 2021
- 120
- 93
RIWAYA: Fedha Au Risasi
MTUNZI: Emmanuel Phiri
NAMBA: 0758 195 890
SEHEMU YA 01
Aliamshwa toka usingizini kwa teke kali la mbavuni, akakagumia kwa maumivu makali yaliyosambaa mwili mzima kama siafu ashambuliavyo kitoweo chake. Sauti kali ya kukwaruza ililiteka anga, sauti yake ya asili ilikuwa mbali na yeye baada ya kuipoteza kwa kilio kilichokuwa kikimwandama mara kwa mara ndani ya chumba hicho cha mahabusu. Alijikunja haraka kama nyoka akidhani atapunguza ukali wa maumivu aliyokuwa akipitia lakini ilikuwa sawa na kuchukua maji ndani ya nyumba ya makazi na kuyamwaga bahari ya Hindi. Hakupata nafuu yoyote. Mpigaji hakujali hali yake, alimwagia maji ya baridi huku akiendelea kumshambulia kwa mateke, maneno ya kashfa na matusi yaliyotaja viungo vya mwili wa binadamu, hasa mwanamke.
Mpigaji hakujali alikuwa akimtesa msichana mdogo mwenye umri chini ya miaka kumi na nane. Siyo kwamba hakujua hilo, hapana, bali alikuwa akitekeleza kauli ya mkuu wake wa kazi. Hakuishia hapo, alimshika miguu binti yule akaanza kumburuza sakafuni kama kiroba cha chumvi. Hakujali binti yule alivyokuwa akilalamika kwa maumivu aliyokuwa akipitia. Kwakuwa ulikuwa usiku wa manane wenye giza totoro, binti yule hakufanikiwa kumuona mpigaji bali alitambua uwepo wake kutokana na kipigo alichokuwa akipitia. Mpigaji alimuona binti yule vizuri kwa sababu alikuwa na tochi lenye mwanga mkali uliozidisha mateso kwa mpigwaji.
Binti alibamizwa ukutani, akapasuka usoni, akaongeza idadi ya vidonda mwilini. Madonda yaliyokuwa yameacha kuvuja damu yakaanza kumwaga damu kama awali. Aliendelea kulia kama mtoto mdogo lakini hakuna msaada wowote uliopatikana. Alikuwa mwana kondoo mbele ya simba mwenye njaa. Japokuwa sauti ya kilio chake ilipaa angani na kusambaa eneo kubwa la jengo la polisi lakini hakuna aliyefika angalau kutazama nini kilichokuwa kikiendelea. Binti yule alizidi kujihakikishia kuwa, mateso yake yalikuwa ni mpango wa uongozi wa mkoa wake na baadhi ya viongozi wa juu serikali. Alimsikia mpigaji akimfokea kwa kusema
“Lazima ufie gerezani kahaba wewe, huwezi kumuua ofisa wa polisi alafu ufumbiwe maji”
Yalikuwa ni baadhi ya maneno yaliyomtoka mpigaji. Mpigaji alimpiga binti yule mpaka akachoka, jasho lilimtiririka mithili ya mtu aliyetoka kucheza mpira wa miguu. Alitoka ndani ya chumba cha mahabusu, akafunga vizuri kwa kufuri nzito la chuma kisha akatokomea kusikojulikana. Binti akaendelea kulia kama sehemu ya kuomboleza maumivu. Akajikusanya taratibu na kuelekea kwenye moja ya kona ya chumba kile akajikunyata kama kifaranga kilichokosa mama. Kichwani aliendelea kujiuliza kwanini hapelekwi mahakamani kusomewa shitaka lake?, hakupata jawabu kamili.
Ulikuwa usiku wa siku ya tano tangu aingizwe ndani ya chumba hicho cha mahabusu. Chumba kichafu kilichotapakaa damu kila kona. Harufu za kinyesi na mikojo vilikuwa ndiyo mahala pake. Chumba hicho kilichobanduka sakafu na kuacha mawe nje yakisalimia na kuwatesa watuhumiwa kilikuwa kimening`inizwa minyororo toka darini, minyororo iliyotumika kuwafunga watuhumiwa wa makosa mbalimbali. Kwenye kona moja ya chumba hicho kulikuwa na kiti cha chuma kilichounganishwa na mfumo wa umeme, kiti hicho kilitumika kuwaadhibu wahalifu hasa waliogoma kutoa ushirikiano. Hakika kwa namna chumba kile kilivyokuwa hakikustahili kuwa chumba cha mahabusu bali chumba cha mateso, tena mateso ya magaidi au wahaini wa taifa lao.
Hata hivyo, chumba hicho kilikuwa cha siri na mara nyingi mhalifu aliteswa usiku ili kuondoa uwezekano wa watu wengine kubaini usiri huo. Mahabusu wa vyumba vya jirani walitambua uwepo wa chumba hicho kwa sababu walisikia kila kilichokuwa kikiendelea. Siri ilikuwa wa raia wa nje. Kilikuwa chumba cha mwisho kabisa kati ya vyumba vya mahabusu. Kwa nje kilionekana kama chumba kisichokuwa na matumizi yoyote. Hata sauti ya mateso ikipaa ilikuwa vigumu sana kufikia makazi ya raia kwa sababu kituo hicho cha polisi kilikuwa mbali na kilikuwa na sheria nyingi na ngumu kuruhusu raia kukisogelea. Kilikuwa kituo kilichoogopwa sana mkoani Rwama Mwanzo. Na kilikuwa ni moja ya kituo kilichokuwa na sifa mbaya sana nchini Malosha, lakini hakuna kiongozi aliyekemea suala hilo. Kiliendelea kutoa huduma za mateso kila siku. Hata wale watuhumiwa waliokuwa vyumba vya jirani waliporuhusiwa na kwenda uraiani walisema kuhusu uwepo wa chumba hicho cha mateso lakini hakuna aliyejali.
Machozi yakaendelea kutengeneza mifereji katika mashavu ya binti yule baada ya kukumbuka namna alivyoshuhudia kifo cha baba yake, siku hiyo hiyo ndiyo alikamatwa na kuswekwa mahabusu na kuanza kuteswa kama gaidi aliyekamatwa ikulu. Siku ya kukamatwa kwake alishuhudia namna vijana watatu waliovaa kiraia wakiwa wamefunika sura zao kwa soksi usoni wakimuonesha baba yake kitu kupitia simu iliyokuwa imeshika na kijana aliyekuwa katikati. Hakuweza kubaini ni kitu gani. Kati ya vijana wale watatu, mmoja alikuwa ameshika begi lililokuwa zimefunguliwa zipu na kuonesha kiasi kikubwa cha fedha (dollars). Mwingine alikuwa na bastola ndoto aina ya Beretta 92 akiizungusha kidoleni kwake kama mchezo wa watoto. Wa tatu alikuwa katikati yao na ndiye aliyekuwa mzungumzaji mkuu aliyekuwa akishurutisha jambo kwa ukali sana.
Baba yake alikuwa amepiga magoti akiomba kuachwa huru lakini hakuna aliyemsikiliza. Kipindi hicho binti yake alikuwa nyuma ya mlango akichungulia kupitia tundu la kupitishia funguo. Vijana wale watatu waliona ugumu wa mzee yule kutekeleza hitaji lao. Kijana aliyekuwa katikati ya mwenzake, alianza kutembea kushoto kisha kulia. Akainua kichwa na kukishusha chini. Alikuwa akitafakari kitu cha kufanya. Akafanikiwa kupata jawabu, akarudi mbele ya mzee yule kisha akaongea kwa sauti ya juu
“Plata o Plomo”
Kauli ya kijana yule ilimaanisha kuwa mzee achague kuchukua fedha na kutekeleza hitaji lao kisha aachwe huru au apigwe risasi baada ya kugoma kutimiza matakwa yao. Hakika ilikuwa ni ‘Plata o Plomo’. Kauli ilikuwa tata mbele ya mzee, hakuielewa hata kidogo. Vijana wale walielewa kuwa mzee hakuwaelewa walichomaanisha baada ya kusikia sentensi ile yenye maneno ya asili ya America. Kijana mzungumzaji alifafanua maana ya maneno yake. Akaeleweka kwa asilimia mia, lakini mzee hakuwa tayari kuwa msaliti. Aliongea kwa sauti ya juu kama alivyoulizwa
“Sijawahi kuwa msaliti. Sipo tayari kutimiza upuuzi wenu”
Majibu yake yaliwakera sana watekaji. Kijana aliyekuwa mzungumzaji akampa amri kijana mwenye bastola mkononi afanye kazi ya kuondoa uhai wa mzee. Hazikupita hata sekunde tano, binti aliyekuwa akichungulia mkasa wa baba yake alishuhudia baba yake akiwa marehemu baada ya kupigwa risasi ya kichwa. Bastola iliyotumika kufanya mauaji haikutoa sauti yoyote, ilikuwa imefungwa kizuia sauti. Japokuwa bastola haikuwa sauti lakini binti yule alitoa sauti ya mshituko na hofu nyuma ya mlango. Sauti yake ilisafiri mpaka kwenye masikio ya vijana wale waliomuua baba yake. Wale vijana wakageuka haraka kuangalia sauti ilipotokea.
Kitendo kile kilimuongezea hofu binti yule aliyekuwa amevaa sare za shule na begi mgongoni lenye madaftari na vitabu. Alivua begi akalitupa chini kisha akaanza kutimua mbio kuelekea nje. Alifanikiwa kufika nje ya nyumba yao lakini kabla hajafanikiwa kutoka nje ya geti alisikia mngurumo wa gari nje ya mlango wa geti kisha kimya kikatawala ghafla. Alijua si jambo jema kwake, alihisi kuishiwa nguvu kwa sababu hakujua ni nani aliyesimamisha gari nje ya geti lao. Alihisi labda ni wahalifu wengine. Alipofikiria kurudi nyuma, mwili ukakataa. Akakumbuka namna alivyoshuhudia kifo cha baba yake. Akabaki amesimama kama mlingoti wa umeme huku akitetemeka na kuruhusu haja ndoto kushambulia nguo yake ya ndani.
Kipindi akitafakari jambo la kufanya alishuhudia mlango wa geti ukifunguliwa kisha wakaingia watu watatu wakiwa na silaha za moto mikononi. Hawakutofautiana hata kidogo na wale watu aliowashuhudia wakiondoa maisha ya baba yake kipenzi, nao walikuwa wameziba sura zao kwa soksi nyeusi usoni. Watu wale walipomuona binti yule walinyooshea silaha zao haraka na kumshurutisha kusimama pale pale alipokuwa. Binti yule aliweweseka kwa hofu, akili zikaenda kushoto kisha kulia. Akahisi akishindwa kuhimili mwili wake. Akaanguka chini kama gunia na kupoteza fahamu.
Alishitushwa na kelele za hapa na pale. Alipofumbua macho aligundua yupo sebuleni kwao, maiti ya baba yake ikiwa pembeni. Alizungusha macho na kuona idadi ya polisi sita, alipojaribu kuinuka akashindwa. Aligundua alikuwa amefungwa pingu mikononi. Alihamaki kwa hofu na kutoa kauli aliyoshindwa kuielewa hata yeye. Kauli yake ikayakifikia masikio ya polisi, wakageuka na kumtazama. Walikuwa na sura za hasira na visasi dhidi yake. Mmoja kati ya polisi wale aliongea kwa ukali
“Mtoto mdogo kama wewe unafanya ukatili huu! Sasa utaieleza mamlaka”
Binti yule alishangazwa na kauli ya polisi, alihisi kama alisikia vibaya lakini haikuwa hivyo. Alisikia kwa usahihi kabisa. Sauti ya polisi yule haikuwa ngeni kwake, alihisi ilifanana kabisa na sauti aliyoisikia muda mfupi uliopita. Sauti ya miongoni mwa watu waliomuua baba yake. Sauti iliyomwambia baba yake
“Plata o Plomo” (Pesa au Risasi)
Lakini aliona kitu cha tofauti, vijana waliomuua baba yake walikuwa wamevaa mavazi ya kiraia, vile vile mauaji yalifanyika chumbani kwa baba yake na siyo sebuleni alipokuwa muda huo. Akakumbuka mara ya mwisho alikuwa nje ya nyumba yao akitafuta njia ya kutoa getini kisha akawaona vijana wengine watatu wakiingia, baada ya hapo hakuna alichokumbuka. Alijitazama vizuri akagundua amevaa mavazi ya nyumbani tofauti na alivyokuwa awali na nguo za shule. Akili ikaenda mbali sana, akahisi labda yamepita masaa mengi baada ya kushuhudia kifo cha baba yake lakini alipotazama saa yake ya mkononi ikamuonesha imepita robo saa tangu ashuhudie kifo hicho. Alikumbuka alishuhudia watu watatu wakiondoa maisha ya baba yake kisha akashuhudia watu watatu wakiingia getini, na muda huo alikuwa mbele ya polisi sita. Idadi sawa ya watu aliowaona. Akabaki njia panda. Kichwa kigagoma kufikiria zaidi.
ITAENDELEA
Kitabu cha riwaya ya MATEKA kinapatikana, piga namba 0758 195 890 utumiwe mkoa wowote
MTUNZI: Emmanuel Phiri
NAMBA: 0758 195 890
SEHEMU YA 01
Aliamshwa toka usingizini kwa teke kali la mbavuni, akakagumia kwa maumivu makali yaliyosambaa mwili mzima kama siafu ashambuliavyo kitoweo chake. Sauti kali ya kukwaruza ililiteka anga, sauti yake ya asili ilikuwa mbali na yeye baada ya kuipoteza kwa kilio kilichokuwa kikimwandama mara kwa mara ndani ya chumba hicho cha mahabusu. Alijikunja haraka kama nyoka akidhani atapunguza ukali wa maumivu aliyokuwa akipitia lakini ilikuwa sawa na kuchukua maji ndani ya nyumba ya makazi na kuyamwaga bahari ya Hindi. Hakupata nafuu yoyote. Mpigaji hakujali hali yake, alimwagia maji ya baridi huku akiendelea kumshambulia kwa mateke, maneno ya kashfa na matusi yaliyotaja viungo vya mwili wa binadamu, hasa mwanamke.
Mpigaji hakujali alikuwa akimtesa msichana mdogo mwenye umri chini ya miaka kumi na nane. Siyo kwamba hakujua hilo, hapana, bali alikuwa akitekeleza kauli ya mkuu wake wa kazi. Hakuishia hapo, alimshika miguu binti yule akaanza kumburuza sakafuni kama kiroba cha chumvi. Hakujali binti yule alivyokuwa akilalamika kwa maumivu aliyokuwa akipitia. Kwakuwa ulikuwa usiku wa manane wenye giza totoro, binti yule hakufanikiwa kumuona mpigaji bali alitambua uwepo wake kutokana na kipigo alichokuwa akipitia. Mpigaji alimuona binti yule vizuri kwa sababu alikuwa na tochi lenye mwanga mkali uliozidisha mateso kwa mpigwaji.
Binti alibamizwa ukutani, akapasuka usoni, akaongeza idadi ya vidonda mwilini. Madonda yaliyokuwa yameacha kuvuja damu yakaanza kumwaga damu kama awali. Aliendelea kulia kama mtoto mdogo lakini hakuna msaada wowote uliopatikana. Alikuwa mwana kondoo mbele ya simba mwenye njaa. Japokuwa sauti ya kilio chake ilipaa angani na kusambaa eneo kubwa la jengo la polisi lakini hakuna aliyefika angalau kutazama nini kilichokuwa kikiendelea. Binti yule alizidi kujihakikishia kuwa, mateso yake yalikuwa ni mpango wa uongozi wa mkoa wake na baadhi ya viongozi wa juu serikali. Alimsikia mpigaji akimfokea kwa kusema
“Lazima ufie gerezani kahaba wewe, huwezi kumuua ofisa wa polisi alafu ufumbiwe maji”
Yalikuwa ni baadhi ya maneno yaliyomtoka mpigaji. Mpigaji alimpiga binti yule mpaka akachoka, jasho lilimtiririka mithili ya mtu aliyetoka kucheza mpira wa miguu. Alitoka ndani ya chumba cha mahabusu, akafunga vizuri kwa kufuri nzito la chuma kisha akatokomea kusikojulikana. Binti akaendelea kulia kama sehemu ya kuomboleza maumivu. Akajikusanya taratibu na kuelekea kwenye moja ya kona ya chumba kile akajikunyata kama kifaranga kilichokosa mama. Kichwani aliendelea kujiuliza kwanini hapelekwi mahakamani kusomewa shitaka lake?, hakupata jawabu kamili.
Ulikuwa usiku wa siku ya tano tangu aingizwe ndani ya chumba hicho cha mahabusu. Chumba kichafu kilichotapakaa damu kila kona. Harufu za kinyesi na mikojo vilikuwa ndiyo mahala pake. Chumba hicho kilichobanduka sakafu na kuacha mawe nje yakisalimia na kuwatesa watuhumiwa kilikuwa kimening`inizwa minyororo toka darini, minyororo iliyotumika kuwafunga watuhumiwa wa makosa mbalimbali. Kwenye kona moja ya chumba hicho kulikuwa na kiti cha chuma kilichounganishwa na mfumo wa umeme, kiti hicho kilitumika kuwaadhibu wahalifu hasa waliogoma kutoa ushirikiano. Hakika kwa namna chumba kile kilivyokuwa hakikustahili kuwa chumba cha mahabusu bali chumba cha mateso, tena mateso ya magaidi au wahaini wa taifa lao.
Hata hivyo, chumba hicho kilikuwa cha siri na mara nyingi mhalifu aliteswa usiku ili kuondoa uwezekano wa watu wengine kubaini usiri huo. Mahabusu wa vyumba vya jirani walitambua uwepo wa chumba hicho kwa sababu walisikia kila kilichokuwa kikiendelea. Siri ilikuwa wa raia wa nje. Kilikuwa chumba cha mwisho kabisa kati ya vyumba vya mahabusu. Kwa nje kilionekana kama chumba kisichokuwa na matumizi yoyote. Hata sauti ya mateso ikipaa ilikuwa vigumu sana kufikia makazi ya raia kwa sababu kituo hicho cha polisi kilikuwa mbali na kilikuwa na sheria nyingi na ngumu kuruhusu raia kukisogelea. Kilikuwa kituo kilichoogopwa sana mkoani Rwama Mwanzo. Na kilikuwa ni moja ya kituo kilichokuwa na sifa mbaya sana nchini Malosha, lakini hakuna kiongozi aliyekemea suala hilo. Kiliendelea kutoa huduma za mateso kila siku. Hata wale watuhumiwa waliokuwa vyumba vya jirani waliporuhusiwa na kwenda uraiani walisema kuhusu uwepo wa chumba hicho cha mateso lakini hakuna aliyejali.
Machozi yakaendelea kutengeneza mifereji katika mashavu ya binti yule baada ya kukumbuka namna alivyoshuhudia kifo cha baba yake, siku hiyo hiyo ndiyo alikamatwa na kuswekwa mahabusu na kuanza kuteswa kama gaidi aliyekamatwa ikulu. Siku ya kukamatwa kwake alishuhudia namna vijana watatu waliovaa kiraia wakiwa wamefunika sura zao kwa soksi usoni wakimuonesha baba yake kitu kupitia simu iliyokuwa imeshika na kijana aliyekuwa katikati. Hakuweza kubaini ni kitu gani. Kati ya vijana wale watatu, mmoja alikuwa ameshika begi lililokuwa zimefunguliwa zipu na kuonesha kiasi kikubwa cha fedha (dollars). Mwingine alikuwa na bastola ndoto aina ya Beretta 92 akiizungusha kidoleni kwake kama mchezo wa watoto. Wa tatu alikuwa katikati yao na ndiye aliyekuwa mzungumzaji mkuu aliyekuwa akishurutisha jambo kwa ukali sana.
Baba yake alikuwa amepiga magoti akiomba kuachwa huru lakini hakuna aliyemsikiliza. Kipindi hicho binti yake alikuwa nyuma ya mlango akichungulia kupitia tundu la kupitishia funguo. Vijana wale watatu waliona ugumu wa mzee yule kutekeleza hitaji lao. Kijana aliyekuwa katikati ya mwenzake, alianza kutembea kushoto kisha kulia. Akainua kichwa na kukishusha chini. Alikuwa akitafakari kitu cha kufanya. Akafanikiwa kupata jawabu, akarudi mbele ya mzee yule kisha akaongea kwa sauti ya juu
“Plata o Plomo”
Kauli ya kijana yule ilimaanisha kuwa mzee achague kuchukua fedha na kutekeleza hitaji lao kisha aachwe huru au apigwe risasi baada ya kugoma kutimiza matakwa yao. Hakika ilikuwa ni ‘Plata o Plomo’. Kauli ilikuwa tata mbele ya mzee, hakuielewa hata kidogo. Vijana wale walielewa kuwa mzee hakuwaelewa walichomaanisha baada ya kusikia sentensi ile yenye maneno ya asili ya America. Kijana mzungumzaji alifafanua maana ya maneno yake. Akaeleweka kwa asilimia mia, lakini mzee hakuwa tayari kuwa msaliti. Aliongea kwa sauti ya juu kama alivyoulizwa
“Sijawahi kuwa msaliti. Sipo tayari kutimiza upuuzi wenu”
Majibu yake yaliwakera sana watekaji. Kijana aliyekuwa mzungumzaji akampa amri kijana mwenye bastola mkononi afanye kazi ya kuondoa uhai wa mzee. Hazikupita hata sekunde tano, binti aliyekuwa akichungulia mkasa wa baba yake alishuhudia baba yake akiwa marehemu baada ya kupigwa risasi ya kichwa. Bastola iliyotumika kufanya mauaji haikutoa sauti yoyote, ilikuwa imefungwa kizuia sauti. Japokuwa bastola haikuwa sauti lakini binti yule alitoa sauti ya mshituko na hofu nyuma ya mlango. Sauti yake ilisafiri mpaka kwenye masikio ya vijana wale waliomuua baba yake. Wale vijana wakageuka haraka kuangalia sauti ilipotokea.
Kitendo kile kilimuongezea hofu binti yule aliyekuwa amevaa sare za shule na begi mgongoni lenye madaftari na vitabu. Alivua begi akalitupa chini kisha akaanza kutimua mbio kuelekea nje. Alifanikiwa kufika nje ya nyumba yao lakini kabla hajafanikiwa kutoka nje ya geti alisikia mngurumo wa gari nje ya mlango wa geti kisha kimya kikatawala ghafla. Alijua si jambo jema kwake, alihisi kuishiwa nguvu kwa sababu hakujua ni nani aliyesimamisha gari nje ya geti lao. Alihisi labda ni wahalifu wengine. Alipofikiria kurudi nyuma, mwili ukakataa. Akakumbuka namna alivyoshuhudia kifo cha baba yake. Akabaki amesimama kama mlingoti wa umeme huku akitetemeka na kuruhusu haja ndoto kushambulia nguo yake ya ndani.
Kipindi akitafakari jambo la kufanya alishuhudia mlango wa geti ukifunguliwa kisha wakaingia watu watatu wakiwa na silaha za moto mikononi. Hawakutofautiana hata kidogo na wale watu aliowashuhudia wakiondoa maisha ya baba yake kipenzi, nao walikuwa wameziba sura zao kwa soksi nyeusi usoni. Watu wale walipomuona binti yule walinyooshea silaha zao haraka na kumshurutisha kusimama pale pale alipokuwa. Binti yule aliweweseka kwa hofu, akili zikaenda kushoto kisha kulia. Akahisi akishindwa kuhimili mwili wake. Akaanguka chini kama gunia na kupoteza fahamu.
Alishitushwa na kelele za hapa na pale. Alipofumbua macho aligundua yupo sebuleni kwao, maiti ya baba yake ikiwa pembeni. Alizungusha macho na kuona idadi ya polisi sita, alipojaribu kuinuka akashindwa. Aligundua alikuwa amefungwa pingu mikononi. Alihamaki kwa hofu na kutoa kauli aliyoshindwa kuielewa hata yeye. Kauli yake ikayakifikia masikio ya polisi, wakageuka na kumtazama. Walikuwa na sura za hasira na visasi dhidi yake. Mmoja kati ya polisi wale aliongea kwa ukali
“Mtoto mdogo kama wewe unafanya ukatili huu! Sasa utaieleza mamlaka”
Binti yule alishangazwa na kauli ya polisi, alihisi kama alisikia vibaya lakini haikuwa hivyo. Alisikia kwa usahihi kabisa. Sauti ya polisi yule haikuwa ngeni kwake, alihisi ilifanana kabisa na sauti aliyoisikia muda mfupi uliopita. Sauti ya miongoni mwa watu waliomuua baba yake. Sauti iliyomwambia baba yake
“Plata o Plomo” (Pesa au Risasi)
Lakini aliona kitu cha tofauti, vijana waliomuua baba yake walikuwa wamevaa mavazi ya kiraia, vile vile mauaji yalifanyika chumbani kwa baba yake na siyo sebuleni alipokuwa muda huo. Akakumbuka mara ya mwisho alikuwa nje ya nyumba yao akitafuta njia ya kutoa getini kisha akawaona vijana wengine watatu wakiingia, baada ya hapo hakuna alichokumbuka. Alijitazama vizuri akagundua amevaa mavazi ya nyumbani tofauti na alivyokuwa awali na nguo za shule. Akili ikaenda mbali sana, akahisi labda yamepita masaa mengi baada ya kushuhudia kifo cha baba yake lakini alipotazama saa yake ya mkononi ikamuonesha imepita robo saa tangu ashuhudie kifo hicho. Alikumbuka alishuhudia watu watatu wakiondoa maisha ya baba yake kisha akashuhudia watu watatu wakiingia getini, na muda huo alikuwa mbele ya polisi sita. Idadi sawa ya watu aliowaona. Akabaki njia panda. Kichwa kigagoma kufikiria zaidi.
ITAENDELEA
Kitabu cha riwaya ya MATEKA kinapatikana, piga namba 0758 195 890 utumiwe mkoa wowote
