SERGIO
JF-Expert Member
- Dec 13, 2012
- 348
- 145
Samwel Sitta, Waziri wa Uchukuzi, mara baada ya kuteuliwa kwenye wadhifa huo aliutangazia umma kuwa ameunda tume ya kuchunguza utendaji wa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Mhandisi Madeni Mapande, baada ya kumsimamisha kazi kwa tuhuma mbalimbali. Baadaye alitangaza kuwa tume imekamilisha kazi yake, lakini hajawahi kutangaza matokeo/mapendekezo ya tume hiyo. Alichofanya ni kumuondoa Mapande na kumpeleka Utumishi ili apangiwe kazi nyingine. Kwa maoni yangu umma una haki ya kujua tume iligundua nini katika uchunguzi wake. Au shida ya Sitta ilikuwa ni kumng'oa tu Kipande? Kwa nini amekuwa kimya kuhusu kilichogunduliwa na tume kwa manufaa ya TPA?