GE2025 RC Morogoro: Wanaoratibu vitendo vya uvunjifu wa amani uchaguzi mkuu kukiona

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, ametoa onyo kali kwa makundi au watu wenye nia ya kuanzisha fujo ama vurugu wakati wa kipindi cha uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo imara na makini kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa nchini.

Malima ametoa kauli hiyo leo Jumatano Oktoba 22, 2025, wakati wa Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu, lililoandaliwa na Taasisi ya Ukumbusho wa Zakkat Tanzania na kufanyika mkoani Morogoro, akisema kuwa baadhi ya watu wanaojaribu kuvuruga amani nchini ni watu wanaoshawishiwa na kuiga matendo kutoka nje, na hawana nia njema na Taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa , amesema watanzania wanapaswa kukataa kwa nguvu zote watu wanaoeneza chuki na kuhatarisha maisha ya wengine, hasa katika kipindi hiki nyeti cha uchaguzi.

Naye Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Morogoro, Dkt. George Pindua, ameahidi kuwa viongozi wa dini wataendelea kuhubiri amani, mshikamano na upendo ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira ya utulivu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…