Ndugu zangu habari za saahizi? Yapata miaka saba sasa tangu nipost kwa mara ya mwisho katika jukwaa hili. Leo nimepata wito wa kuandika jambo walau na mm nitoe ya moyoni kwa kinachoendelea sasahivi katika taifa leo.
Naanza kwa kujiuliza, kwani Rais ni mtu au taasisi? Nijuavyo mimi Rais ni taasisi, haijakishi jinsia, rangi, dini wala kabila yeyote atakayekaa katika nafasi hiyo ndio wetu tayari. Sote tunapaswa kumsikiliza na kutekeleza maagizo yake kwa utii.
Leo hii wale viongozi waliokuwa na nafasi kubwa katika Serikali na kuzipoteza wameonekana vinganganizi na watovu wa nidhamu kwa taasisi (Rais). Ushauri wangu, ni vema wakakubali matokeo ya kwamba, wakati wao umekwisha na sasa ni wakati wa wengine kuitumikia nchi yao.
Imebainika kuwa, vinganganizi hao walichuma sana fedha za umma wakati huo hata ziwape viburi na kutomtii mtawala wa sasa. Wafahamu kuwa mtawala anafahamu juu ya chuki yao kwake, namna walivyochota mali ya umma wakati huo lakini pia anafahamu mipango yao ya baadae.
Sasa basi, mwenye masikio na asikie maneno haya. Walipata bahati wakaitumia kwa maslahi yao, basi wakae pembeni ili wazalendo wa kweli waendeshe nchi kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Asanteni.
Ni mimi mtiifu wa Rais (Taasisi).
Naanza kwa kujiuliza, kwani Rais ni mtu au taasisi? Nijuavyo mimi Rais ni taasisi, haijakishi jinsia, rangi, dini wala kabila yeyote atakayekaa katika nafasi hiyo ndio wetu tayari. Sote tunapaswa kumsikiliza na kutekeleza maagizo yake kwa utii.
Leo hii wale viongozi waliokuwa na nafasi kubwa katika Serikali na kuzipoteza wameonekana vinganganizi na watovu wa nidhamu kwa taasisi (Rais). Ushauri wangu, ni vema wakakubali matokeo ya kwamba, wakati wao umekwisha na sasa ni wakati wa wengine kuitumikia nchi yao.
Imebainika kuwa, vinganganizi hao walichuma sana fedha za umma wakati huo hata ziwape viburi na kutomtii mtawala wa sasa. Wafahamu kuwa mtawala anafahamu juu ya chuki yao kwake, namna walivyochota mali ya umma wakati huo lakini pia anafahamu mipango yao ya baadae.
Sasa basi, mwenye masikio na asikie maneno haya. Walipata bahati wakaitumia kwa maslahi yao, basi wakae pembeni ili wazalendo wa kweli waendeshe nchi kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Asanteni.
Ni mimi mtiifu wa Rais (Taasisi).