Rais Magufuli wa kile kipindi cha kampeni si huyu wa sasa

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,652
Kwenye campain za 2015 alijifanya kama vile alikuwa hana tamaa ya kuwa Raisi. Campain zake zilijaa kejeli na kuponda utawala uliokuwa umepita hasa wa kikwete. Alionekana hakuwa na nia hata ya kuwa mwenyekiti wa CCM. Ila baada ya kuupata huo Uraisi kwa magumashi bado anaendelea na campain. Mwaka sasa umepita na miezi kazaa yupo bado kwenye campain. Kila anapoongea anaongea kisiasa zaidi. Hajui hata mambo yapi aongelee sehemi ipi ( what to talk at right time at right place to right people.)

Baada ya kukaa Mjengoni sasa kaona utamu wa kuwa Raisi Tanzania. sasa anaonyesha kuwa na uchu sana na madaraka. Nguvu anazotumia kuuwa upinzani Tanzania umeanza kutupa hofu kuwa anaweza kuwa kama wale maraisi wanaong'angania madarakani kutolewa mpaka kwa mtutu.

Sasa anajitengenezea mazingira ya kuogopwa na walio chini yake. Hakuna anayejaribu kumuhoji au kumkosoa. anachoamua yeye wao ni "ndyo mzee" hata kama wanajua sio kizuri. Viongozi wa "ndyo mzee" anawatengenezea mazingira ya kuwapa vyeo. Wale wa "mzee hapa umekosea" anawatengenezea mazingira ya kuwatumbua. TUNAELEKEA WAPI KAMA SERIKALI ITAJAA WATU WA NAMNA HII?



Huyu aliyeonekana kutetea wanyonge mbona amekuwa ndye wa kuzidi kuwanyonga hawa wanyonge? Maisha yamekuwa magumu kwa masikini na si kwa matajiri.

JE KIPI KIFANYIKE.

SIASA SIASA SIASA ni kikwazo kikubwa kinachokwamisha maendeleo ya Tanzania. Hii nchi tungekuwa tumefika mbali kama tungekuwa na siasa zilizojikita katika maendeleo ya nchi na si ya chama. Watanzania tunafanya ushabiki wa vyama kama vile timu za Mpira. ( Simba na yanga).

Kipindi kile Magufuli yupo kwenye kampain alionekana kama atakuwa kiongozi ambaye angetumia hata wapinzani wake kushirikiana kutatua matatizo yanayoikumba Tz. Lakini wamekuwa kama paka na panya kama sio tom and Jerry.
Kwanini tusiwe tunaiga hata wenzetu kwenye nchi zilizoendelea? Wao wakishamaliza uchaguzi wanakaa pamoja na kuanza kushirikiana kutatua matatizo ya nchi zao. KIONGOZI MWENYE NIA NJEMA NA NCHI YAKE NA MZALENDO HASHINDWI KUSHIRIKIANA NA WAPINZANI WAKE KUJENGA NCHI.

Kikwete naye alikuwa kafikia hatua iyo sema ups and downs zilikuwa nyingi. Ni mara nyingi alikutana na wapinzani wake na kujadili mambo ya msingi ili kutatua changamoto mbalimbali. Hakuishia hapo tu. Aliwapa hata fursa ya kupata exposure nje na walikuja kushiriki pamoja kuendeleza Taifa letu.

Magufuli yeye kwa nini ameua uo utamaduni? Kwanini anatutengenezea matabaka yasiyokuwa na tija? Nini malengo yake hasa ya baadaye.

Na sisi watanzania tuache ushabiki wa vyama huu sio muda wa kushabikia mavyama ya kusiasa. Tumejikita kushabikia vyama huku tukisahau kitu cha msingi ni maendekeo ya Taifa letu. Vyama vyote ni vibovu. Hawa viongozi wa vyama wao wanatetea matumbo yao tu.
Watanzania tuache unafiki. Kiongozi akikosea tuseme amekosea bila kigugumizi na akifanya jema tusiache kumsifu.
 
Tunataka chanel zile za bure zirudishwe la sivyo waturudishie analogia yetu maana antena bado tunazo. Hii ni laana na unyonyaji mkubwa kwa kutaka kuwakamua maskini wa nchi hii kila walichonacho.
 
JPM anajua ukicheka Cheka na Kuku unaowafuga watakuita Dhaifu

Ni full ukauzu, ubandidu, ubaba Ubaya na Full Mikwala ya Kaboka Mchizi
 
Kwenye campain za 2015 alijifanya kama vile alikuwa hana tamaa ya kuwa Raisi. Campain zake zilijaa kejeli na kuponda utawala uliokuwa umepita hasa wa kikwete. Alionekana hakuwa na nia hata ya kuwa mwenyekiti wa CCM. Ila baada ya kuupata huo Uraisi kwa magumashi bado anaendelea na campain. Mwaka sasa umepita na miezi kazaa yupo bado kwenye campain. Kila anapoongea anaongea kisiasa zaidi. Hajui hata mambo yapi aongelee sehemi ipi ( what to talk at right time at right place to right people.)

Baada ya kukaa Mjengoni sasa kaona utamu wa kuwa Raisi Tanzania. sasa anaonyesha kuwa na uchu sana na madaraka. Nguvu anazotumia kuuwa upinzani Tanzania umeanza kutupa hofu kuwa anaweza kuwa kama wale maraisi wanaong'angania madarakani kutolewa mpaka kwa mtutu.

Sasa anajitengenezea mazingira ya kuogopwa na walio chini yake. Hakuna anayejaribu kumuhoji au kumkosoa. anachoamua yeye wao ni "ndyo mzee" hata kama wanajua sio kizuri. Viongozi wa "ndyo mzee" anawatengenezea mazingira ya kuwapa vyeo. Wale wa "mzee hapa umekosea" anawatengenezea mazingira ya kuwatumbua. TUNAELEKEA WAPI KAMA SERIKALI ITAJAA WATU WA NAMNA HII?



Huyu aliyeonekana kutetea wanyonge mbona amekuwa ndye wa kuzidi kuwanyonga hawa wanyonge? Maisha yamekuwa magumu kwa masikini na si kwa matajiri.

JE KIPI KIFANYIKE.

SIASA SIASA SIASA ni kikwazo kikubwa kinachokwamisha maendeleo ya Tanzania. Hii nchi tungekuwa tumefika mbali kama tungekuwa na siasa zilizojikita katika maendeleo ya nchi na si ya chama. Watanzania tunafanya ushabiki wa vyama kama vile timu za Mpira. ( Simba na yanga).

Kipindi kile Magufuli yupo kwenye kampain alionekana kama atakuwa kiongozi ambaye angetumia hata wapinzani wake kushirikiana kutatua matatizo yanayoikumba Tz. Lakini wamekuwa kama paka na panya kama sio tom and Jerry.
Kwanini tusiwe tunaiga hata wenzetu kwenye nchi zilizoendelea? Wao wakishamaliza uchaguzi wanakaa pamoja na kuanza kushirikiana kutatua matatizo ya nchi zao. KIONGOZI MWENYE NIA NJEMA NA NCHI YAKE NA MZALENDO HASHINDWI KUSHIRIKIANA NA WAPINZANI WAKE KUJENGA NCHI.

Kikwete naye alikuwa kafikia hatua iyo sema ups and downs zilikuwa nyingi. Ni mara nyingi alikutana na wapinzani wake na kujadili mambo ya msingi ili kutatua changamoto mbalimbali. Hakuishia hapo tu. Aliwapa hata fursa ya kupata exposure nje na walikuja kushiriki pamoja kuendeleza Taifa letu.

Magufuli yeye kwa nini ameua uo utamaduni? Kwanini anatutengenezea matabaka yasiyokuwa na tija? Nini malengo yake hasa ya baadaye.

Na sisi watanzania tuache ushabiki wa vyama huu sio muda wa kushabikia mavyama ya kusiasa. Tumejikita kushabikia vyama huku tukisahau kitu cha msingi ni maendekeo ya Taifa letu. Vyama vyote ni vibovu. Hawa viongozi wa vyama wao wanatetea matumbo yao tu.
Watanzania tuache unafiki. Kiongozi akikosea tuseme amekosea bila kigugumizi na akifanya jema tusiache kumsifu.
UNASHANGAA? kama unajua neno METAMORPHOSIS/MABADILIKO. Huo ndo UDHAIFU wetu binadamu.
Tunasahau haraka sana na kubadlilika. Je hujakutana na mtu mlikuwa Level-Daraja-Ngazi nk moja baadaye akapanda zaidi yako na KUJIFANYA hakukumbuki?
Ni udhaifu wetu binadamu.
Lakini ukiwa na watu wazuri watakukumbusha na kukuambia ukweli.
Hata kama ni mchungu!
 
UNASHANGAA? kama unajua neno METAMORPHOSIS/MABADILIKO. Huo ndo UDHAIFU wetu binadamu.
Tunasahau haraka sana na kubadlilika. Je hujakutana na mtu mlikuwa darasa moja baadaye akafanikiwa hata ANAJIFANYA hakukumbuki?
Ni udhaifu wetu binadamu.
Lakini ukiwa na watu wazuri watakukumbusha na kukuambia ukweli.
Hata kama ni mchungu!
Umeandika nini sasa apo
 
Maana yake chadema wanatuambia 2020, watakuja na sera za

kurudisha posho zote kwa watumishi

Kurudisha wote waliotumbuliwa kwa ufisadi

Kufunga mahakama ya mafisadi

Kwa sera za kilofa namna hii nani atawachagua??
Jitahidi kufuatilia jambo kabla ya kuandika. Usiwe bendera fuata upepo
 
Maana yake chadema wanatuambia 2020, watakuja na sera za

kurudisha posho zote kwa watumishi

Kurudisha wote waliotumbuliwa kwa ufisadi

Kufunga mahakama ya mafisadi

Kwa sera za kilofa namna hii nani atawachagua??
Hivi watu wa hivi huwa mnacoment mkiwa mmesha kunywa gongo au ugumu wa maisha ndyo umewafanya wehu
 
Back
Top Bottom