Rais Magufuli, msimamishe Makonda kazi kwa maslahi ya umma!

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,599
6,670
864211cdcd67b87f9ecb680defece855.jpg


Si kwa sababu ya wabunge kumwita akakataa, la hasha!

Si kwa sababu ya kutumiwa na wauza madawa na kujifanya yupo kwenye vita dhidi ya dawa hizo huku akiifanya kazi hii kwa maelekezo ya wahusika wakuu ili kuua vita yenyewe kabla ya kufika kokote (akishirikiana na baadhi ya maafisa wa vyombo vya dola wasio na weledi wa kazi yao).

Si kwa sababu ya zile taarifa mfu alizokuwa akikupenyezea ili ang'are mbele zako na Taasisi nzima ya urais kuwa ni RC bora zaidi ya RC yeyote nchini.

Si kwa sababu ya tuhuma za kuwa na mali zenye mashaka mengi tangu akiwa DC na hata sasa ambazo vyanzo vyake idara nyeti zinajua na zimekudokeza mara kadhaa huenda hukujua athari zake.

Si kwa sababu ya yaliyotokea kupitia kijana huyu katika Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Jakaya Kikwete ambayo mengine kuyaandika ni aibu.

Si kwa sababu ya vyeti vyake vyenye utata, la hasha!

Ni kwa Matumizi Mabaya ya Madaraka. Amelewa madaraka, ameota mapembe na sasa asipodhibitiwa Taasisi ya Urais (si wewe kama Magufuli) itaingia fedheha kubwa zaidi ya kinachoonekana sasa.

Haya unayoona ni mvua za rasharasha, mvua kamili itanyesha Aprili 2017 na hutoamini athari itakayoikabili Ikulu yako na kuchafua legacy yako.

Unao muda, chukua hatua mapema!
 
Ninaamini Mhe. Kitwanga hakuondolewa kwenye uwaziri kwa sababu ya ile "ulevi bungeni" hata kama alikunywa kweli! Ikumbukwe siku zile kashfa ya LUGUMI ilikuwa kwenye "burning hell", hivyo ni mtazamo wangu kuwa, ili kunusuru wengi, ilibidi Mhe. Kitwanga aondolewe kwa njia mbadala! "ulevi"!

Likewise, kashfa ya kughushi vyeti inayomkabili Makonda, endapo ikichukuliwa" seriously " ni wazi inaenda na wengi! Rais akimtumbua Makonda kwa kosa la vyeti bandia inabidi serikali yote ya mkoa wa Dar (hasa subordinates wa RC) ifumuliwe upya (ifahamike ma DC huapishwa na RC).

Hivyo, ili kuiepusha aibu hiyo dhidi ya MTEUZI na WANA USALAMA waliofanya "vetting" ya uteuzi, ni wazi sasa, aidha ni mbinu ya KITENGO au MTEUZI kumfanya MAKONDA afanye makosa mapya au kituko chochote ili aondolewe nayo, nje ya makosa ya vyeti!

Mfano:
1. kusafiri hovyo nje ya nchi,
2. kufanya jubilei ya gharama kutimiza mwaka kazini,
3. Kuvamia kituo cha redio usiku akiwa na "MAKUMANDOO" yenye silaha

Hayo ni baadhi ya matukio yanayolenga kumuondoa huyo jamaa bila kuhusisha kosa la vyeti bandia!

NB: nitamsifu Rais endapo Makonda atawajibishwa kwa suala la vyeti na si kosa lingine kwanza!

Nimewasilisha.

By the way, Wenye mapovu, leo weekend, mkafulie nguo zenu!
 
Ninaamini Mhe. Kitwanga hakuondolewa kwenye uwaziri kwa sababu ya ile "ulevi bungeni" hata kama alikunywa kweli! Ikumbukwe siku zile kashfa ya LUGUMI ilikuwa kwenye "burning hell", hivyo ni mtazamo wangu kuwa, ili kunusuru wengi, ilibidi Mhe. Kitwanga aondolewe kwa njia mbadala! "ulevi"!

Likewise, kashfa ya kughushi vyeti inayomkabili Makonda, endapo ikichukuliwa" seriously " ni wazi inaenda na wengi! Rais akimtumbua Makonda kwa kosa la vyeti bandia inabidi serikali yote ya mkoa wa Dar (hasa subordinates wa RC) ifumuliwe upya (ifahamike ma DC huapishwa na RC).

Hivyo, ili kuiepusha aibu hiyo dhidi ya MTEUZI na WANA USALAMA waliofanya "vetting" ya uteuzi, ni wazi sasa, aidha ni mbinu ya KITENGO au MTEUZI kumfanya MAKONDA afanye makosa mapya au kituko chochote ili aondolewe nayo, nje ya makosa ya vyeti!

Mfano:
1. kusafiri hovyo nje ya nchi,
2. kufanya jubilei ya gharama kutimiza mwaka kazini,
3. Kuvamia kituo cha redio usiku akiwa na "MAKUMANDOO" yenye silaha

Hayo ni baadhi ya matukio yanayolenga kumuondoa huyo jamaa bila kuhusisha kosa la vyeti bandia!

NB: nitamsifu Rais endapo Makonda atawajibishwa kwa suala la vyeti na si kosa lingine kwanza!

Nimewasilisha.

By the way, Wenye mapovu, leo weekend, mkafulie nguo zenu!
Well said

Sent from my Vodafone 875 using JamiiForums mobile app
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa (DSM) huyo a.k.a amiri jeshi mkuu wa dar ndivyo kichwa kinavyomtuma kwamba majeshi yote mkoani yako chini yake so can do anything kama alivyofanya huko Clouds. Hongereni IPP Media kwa kupuuza habari za huyu jamaa. Mliona mbali sana. You're really Super Brand.
 
Me natamani amuache ache kwanza tuzidi kushuhudia mengi.

Utawala huu una vitu vingi vinavyofanywa sawa au zaidi ya utawala uliopita halafu wanajidai wamechaguliwa na Mungu.

Me nachoona ni magenge mawili ya kuuza madawa ya kulenya yapo kwenye vita ila lenye nguvu lipo karibu zaidi na serikali na daraja lao ni bashite
 
Haitoshi kumsimamisha kazi.

Anapaswa kufikishwa central kuwekwa ndani mpaka ushahidi utimie bila dhamana. Hata miaka miwili akae huko.

Kisha ashitakiwe kwa kufoji vyeti, kutumia madaraka kujipatia mali na kutumia madaraka hovyo kuvamia vituo vya habari.

Haitoshi kumfukuza tu kazi mwehu huyu.
 
Back
Top Bottom