Rais Magufuli kuisafisha CCM ni sawa tu

Rais Magufuli kuisafisha CCM ni sawa tu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,255
Reaction score
16,185
Baadhi ya viongozi wa CCM sio waaminifu kwa CCM, kwa wananchi na kwa taifa pia. Viongozi hawa walikifikisha chama, wananchi na taifa hapo vilipo sasa. Viongozi hawa walikuwa wanafiki mwanzo mwisho bila kujali elimu zao, dini zao, makabila yao wala taaluma zao.

Viongozi hawa ni wale ambao walikuwa wanafahamu kuwa nchi inaporwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kwamba sheria mbovu zinapitishwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kuwa mikataba mibovu inapitishwa lakini hawafanyi kitu. Viongozi hawa walikuwa wanawaongoza wanachama na watanzania kuimba iyena iyena CCM nambari one hata kama taifa linaporwa na kuliwa kama mchwa.

Rais Magufuli wabaini na kuwaondoa bila huruma viongozi hawa bila kuchelewa kwani hata wana-CCM tunawafahamu na unafiki wao kwa CCM na kwa taifa.

Sifa kubwa ya Viongozi hawa ni watu ambao hawakubali kustaafu hata kidogo, lazima watajichomeka kwa gharama yoyote kwenye uongozi wa chama, ubunge, kamati au bodi za mashirika nyeti. Wakishindwa wao watawachomeka watoto, ndugu au marafiki kwenye nafasi fulanifulani.

Nadhani Rais Magufuli kaletwa na Mungu kuiponya CCM na nchi, sio bure walahi!!!
 
Baadhi ya viongozi wa CCM sio waaminifu kwa CCM, kwa wananchi na kwa taifa pia. Viongozi hawa walikifikisha chama, wananchi na taifa hapo vilipo sasa. Viongozi hawa walikuwa wanafiki mwanzo mwisho bila kujali elimu zao, dini zao, makabila yao wala taaluma zao.

Viongozi hawa ni wale ambao walikuwa wanafahamu kuwa nchi inaporwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kwamba sheria mbovu zinapitishwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kuwa mikataba mibovu inapitishwa lakini hawafanyi kitu. Viongozi hawa walikuwa wanawaongoza wanachama na watanzania kuimba iyena iyena CCM nambari one hata kama taifa linaporwa na kuliwa kama mchwa.

Rais Magufuli wabaini na kuwaondoa bila huruma viongozi hawa bila kuchelewa kwani hata wana-CCM tunawafahamu na unafiki wao kwa CCM na kwa taifa.

Sifa kubwa ya Viongozi hawa ni watu ambao hawakubali kustaafu hata kidogo, lazima watajichomeka kwa gharama yoyote kwenye uongozi wa chama, ubunge, kamati au bodi za mashirika nyeti. Wakishindwa wao watawachomeka watoto, ndugu au marafiki kwenye nafasi fulanifulani.

Nadhani Rais Magufuli kaletwa na Mungu kuiponya CCM na nchi, sio bure walahi!!!


Unaambiwa siku zote mnafiki hana chake. Kuna siku tutaimba wimbo mwingine kabisa. Yaani wimbo wa Tumaini Jipya. Watanzania tumpe sapoti prezda wetu
 
Nadhani Rais Magufuli kaletwa na Mungu kuiponya CCM na nchi, sio bure walahi!!!
Kumbuka JK? Tuliambiwa ni chaguo la nani?Nani kasema CCM haimfii mikononi mwake?
 
Baadhi ya viongozi wa CCM sio waaminifu kwa CCM, kwa wananchi na kwa taifa pia. Viongozi hawa walikifikisha chama, wananchi na taifa hapo vilipo sasa. Viongozi hawa walikuwa wanafiki mwanzo mwisho bila kujali elimu zao, dini zao, makabila yao wala taaluma zao.

Viongozi hawa ni wale ambao walikuwa wanafahamu kuwa nchi inaporwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kwamba sheria mbovu zinapitishwa lakini hawafanyi kitu, walikuwa wanafahamu kuwa mikataba mibovu inapitishwa lakini hawafanyi kitu. Viongozi hawa walikuwa wanawaongoza wanachama na watanzania kuimba iyena iyena CCM nambari one hata kama taifa linaporwa na kuliwa kama mchwa.

Rais Magufuli wabaini na kuwaondoa bila huruma viongozi hawa bila kuchelewa kwani hata wana-CCM tunawafahamu na unafiki wao kwa CCM na kwa taifa.

Sifa kubwa ya Viongozi hawa ni watu ambao hawakubali kustaafu hata kidogo, lazima watajichomeka kwa gharama yoyote kwenye uongozi wa chama, ubunge, kamati au bodi za mashirika nyeti. Wakishindwa wao watawachomeka watoto, ndugu au marafiki kwenye nafasi fulanifulani.

Nadhani Rais Magufuli kaletwa na Mungu kuiponya CCM na nchi, sio bure walahi!!!
Magufuli kashiriki vizuri sana kupitisha mikataba mibovu ndani ya bunge na nje ya bunge (kwenye baraza la mawaziri) ambako ndio maamuzi yote ya mikataba hupitishwa chini ya mwenyekiti wa baraza la mawaziri (rais wa nchi) ambaye pia ni mwenyekiti wa ccm taifa, hivyo nakushangaa sana kumtofautisha magufuli na uchafu wowote ktk serikali kuanzia awamu ya 3 na 4 ambazo alikuwa waziri mwandamizi ndani ya serikali na mbunge pia, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawa ndio wameichafua nchi hii na kuifikisha hapa ilipo leo hii
 
Magufuli kashiriki vizuri sana kupitisha mikataba mibovu ndani ya bunge na nje ya bunge (kwenye baraza la mawaziri) ambako ndio maamuzi yote ya mikataba hupitishwa chini ya mwenyekiti wa baraza la mawaziri (rais wa nchi) ambaye pia ni mwenyekiti wa ccm taifa, hivyo nakushangaa sana kumtofautisha magufuli na uchafu wowote ktk serikali kuanzia awamu ya 3 na 4 ambazo alikuwa waziri mwandamizi ndani ya serikali na mbunge pia, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawa ndio wameichafua nchi hii na kuifikisha hapa ilipo leo hii
Vipi LOWASA ametakata huko alipo!
 
Viongozi wa wanafiki walimsifu Nyerere alipoondoka walimsifu Mzee Mwinyi na wakamponda Mzee Nyerere, alipoondoka Mzee MWINYI Walimponda na kumsifu Mzee Mkapa, nae alipoondoka walimponda na kumsifu Mzee Jk, nae alivyoseppa walimponda na sasa wanamsifu kinafiki Mzee JPM
 
Viongozi wa wanafiki walimsifu Nyerere alipoondoka walimsifu Mzee Mwinyi na wakamponda Mzee Nyerere, alipoondoka Mzee MWINYI Walimponda na kumsifu Mzee Mkapa, nae alipoondoka walimponda na kumsifu Mzee Jk, nae alivyoseppa walimponda na sasa wanamsifu kinafiki Mzee JPM
Hapa utakuwa unawasema wapinzani. Unakumbuka walivyomuita JK dhaifu.
 
Muulize Magufuli alipotembelewa Ikulu na Lowassa alisema maneno gani juu ya Lowassa kwenye utumishi wake ndani ya serikali!
Unafikiri angemwambiaje? Lowassa alijioendekeza, ilikuwa ni kazima apakwe mafuta kwa mgongo wa chupa. Lowassa ni mwizi na hatakaa awe safi hata siku moja
 
EPA iyena, IPTL iiyena, escrow iyena, Songas iyena, meremeta iyena, Richmond iyena, bandari inaporwa iyena, nyumbbba na za serikali zinauzwa iyena, viwanda vya umma vinauzwa iyena, tembo wanauawa iyena, midini tunapewa 3℅ iyena, makanikia yanapelekwa ng'ambo iyena, safari za nje kila siku iyena, watu wanakwepa Kofi iyena CCM nambari one. Hawaeleki wacha tu aisafishe buana.
 
Unafikiri angemwambiaje? Lowassa alijioendekeza, ilikuwa ni kazima apakwe mafuta kwa mgongo wa chupa. Lowassa ni mwizi na hatakaa awe safi hata siku moja
Kumpaka mtu mafuta kwa chupa si unafiki pia? Kwanini unamtusi Rais wa nchi namna hii? Nchi haiwezi kuwa na Rais mnafiki. Mwombe Rais radhi tafadhali.
 
itabidi ajianze mwenyewe maana alikuwepo hayo yote wakati yanafanyika na hakusema kitu chochote
 
Back
Top Bottom