AUGUSTINO CHIWINGA
JF-Expert Member
- Apr 23, 2017
- 220
- 689
Na Augustino Chiwinga
0659438889
Kuelekea mbio za uchaguzi mkuu mwaka 2020, Rais Dr. Johnn Magufuli ameonesha kuwa ndio mgombea pekee ambae hazuiliki katika kushinda tena kwa awamu ya pili mfulululizo. Kutokuzuilika kwake kunatokana na wanannchi wengi kutoka katika matabaka yote kumpenda kwa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana.
Falsafa yake ya mageuzi makubwa ya kiuchumi, kiungozi,kiuwajibikaji, kiutendaji na kiuadilifu, imekua ni chachu kubwa inayomweka Rais Magufuli kileleni kila siku.
Maendeleo yote haya makubwa tunayoyaona ni matokeo ya falsafa hizo.Dira kubwa ya Rais Magufuli ni kuhakikisha kwamba kila Mtanzania kabwela anakula keki ya Taifa, na sio iliwe na watu wachache wakivimbisha matumbo yao na kuwaacha wanyonge wakiogelea katika dimbwi la umaskini.
Tunaposema keki ya Taifa haimaanishi kwamba watu watapewa pesa bure la hasha bali ni katika kuboresha , kuimarisha na kurahisisha upatikanaji wa huduma za jamii kama vile maji, matibabu, miundombinu, uchukuzi, elimu kwa watu wote Raia wa Tanzania.
Rais Magufuli popote anapokwenda amekuwa ni mtu mnyenyekevu , muungwana mpole na mwenye huruma mwenye ari na uchungu mkubwa wa kuwakwamua watanzaniakutoka katika lindi kubwa la umaskini linalowakabili.
Spidi yake kubwa ya kutatuta kero za wananchi imekuwa ni mwiba mchungu kwa baadhi ya watu ambao wanajipanga kupambana nae katika uchaguzi mkuu wa mwakani. Nguvu ya Magufuli ndani na nje ya CCM ni kubwa na isiyoweza kuzuilika kwa maana ya kwamba wanachama wengi wanamkubali na wana imani nae kubwa jinsi alivyoweza kuwarudishia wanachama hao chama chao kutoka kwa baadhi ya watu wachache waliokuwa wamekihodhi na kukitumia kwa maslahi yao binafsi.
Nje ya CCM ndio kabisa anaungwa mkono na makundi na rika za aina zote wenye vyama na wasio na vyama.Nawiwa kusema kwamba huenda akavunja rekodi ya kupigiwa kura nyingi ambazo zinaweza zisifikiwe na Rais yeyote katika awamu zijazo.