Rais Magufuli awaapisha kiapo cha uadilifu Makamishina/Manaibu waliopandishwa vyeo Ikulu

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386

Magufuli nadhani yupo na wale maaskari aliowapandisha vyeo..

=> Kawapa Rungu kawaambia yale mambo ya unanijua mimi nani... Hakuna...
Na kawaambia kuwa polisi wafanye kazi zao..

=> Kuhusu meli kupungua bandarini kasema bora zisije kama hazilipi kodi.

=> kuhusu watalii kasema bora awe na watalii laki tano wanaolipa kodi kuliko watalii mia mbili ambao hawalipi kodi.

=> kasema raia wote ambao wanafanya kazi kwenye jeshi la Polisi waondolewe wote kuanzia kwenye uhasibu na kazi zingine waondolewe warudishwe utumishi..

=> kasema kaambiwa kuwa Sinza nyumba zimekosa watu.. Kacheka anadai watu walikuwa na kufuru.. Mtu mmoja anapangishia michepuko mitatu minne... Na week end anaenda Dubai na kurudi..

=> Polisi wakikamata gari hata kama ni ya RPC waachwe na sheria ifuate mkondo wake. Katolea baadhi ya mifano ya magari kama Happy Nation alisikia kuwa haya magari na mengine ukiyakamata bara barani ujue utahamishwa na kituo..


 

Attachments

  • 13726734_1124334634312462_33600281238670896_n.jpg
    16.2 KB · Views: 124
Akizungumza Ikulu na maofisa wa Polisi walio pandishwa vyeo Leo, Rais ameshangaa Traffic wanaopata shida ya kunyeshewa mvua barabarani eti wakipewa 5,000 ya kubrashi viatu watu wanaita rushwa wakati kuna watu serikalini wanaiba mafedha?
Hiyo ni kauli ya Rais wetu.
Source; TBC 1
 


Nashukuru kwa kutoa tahadhari kwa wale wazito wa kufikiri.. Na wapotoshaji
 
Sasa huyu wa dar akisikia hivyo na yeye anajiona Raisi wa dar, kesho utasikia mashoga wote wajisalimishe, wasio na kazi wajisalimishe, wavuta shisha na sigara hadharani wajisalimishe, machangudoa wajisalimishe, badala ya kushirikiana na viongozi wengine wa kisiasa waliochaguliwa na wananchi na kujenga mahusiano mazuri ili kuwaletea wananchi maendeleo anakomalia matamko yasiyo ya msingi.
Matatizo ya msingi ya wana dar ni haya hapa:-
1. Maji safi na salama,
2. Majitaka na uchafu
3. Barabara mbovu
4. Upungufu wa madarasa, madawati, na vitendea kazi vingine mashuleni
5. Sehemu za kufanyia biashara machinga
6. Uhalifu wa aina mbalimbali pamoja na ujambazi
 
Wadau amani iwe kwenu.

Katika kuhakikisha kuwa kunakuwa hakuna mwingiliano wa majukumu baina ya Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Utumishi wa Umma, Rais Magufuli leo aamemwagiza IGP kuorodhesha majina ya watumishi wote ambao si Polisi na ayapeleke Utumishi wa Umma ambako watapangiwa majukumu mengine. Hayo ameyasema leo Ikulu Jijini Dar es Salaam aliposhuhudia kiapo cha Makamishna Wasaidizi wa Jeshi la Polisi. Amesema jeshi ni jeshi na raia ni raia. Kunapokuwa na muingiliano baina ya jeshi na Raia kunatengeneza mwanya wa ubadhilifu.

Ametolea mfano wa Frank Charles Msaki, aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa jeshi la Polisi ambaye alikuwa anawalipa posho ya chakula watumishi ambao si polisi hali iliyopelekea upotevu wa zaidi ya milioni 300. Amesema kuwa Msaki alikuwa jeuri na alikuwa na mamlaka ya kumfokea hata askari ijapokuwa yeye si Askari kwa vile tu alikuwa anashika fedha.

Aidha, Rais anasema kuwa mchanganyiko huu ulisababisha jeshi la polisi kushindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu Raia wanaofanya kazi kwenye jeshi lao kwa vile misingi ya kuchukuliana hatua baina ya polisi na Utumishi wa Umma ni tofauti.

Ijapokuwa kauli hiyo ameitoa kwenye hafla ya kula kiapo kwa Makamishna Wazaidizi wa Jeshi la Polisi, ameagiza pia vyombo vyote vya Dola kutekeleza agizo hilo kwa vile viongozi wa vyombo vyote vya dola walihudhuria hafla hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…