Rais Magufuli ana tatizo gani na uhuru wa upashanaji habari?

Papa1

JF-Expert Member
Apr 21, 2012
2,017
2,210
Siamini kama Jitihada zinazofanywa na Nape kuhusu kuhujumu matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni ni maamuzi yake na kwamba hayana baraka za Rais John Pombe Magufuli.

Mwanzoni tatizo lilionekana ni kubana matumizi ya TBC, ikaonekana sawa, TBC waache wazime kuonyesha live, Star TV na Azam TV wakaendelea kuonyesha.

Baadaye, ikajitokeza taasisi isiyo ya serikali ikajitolea kulipia matangazo hayo, maana yake kwamba tatizo la budget lilitatuliwa.

Baada ya kuona hivyo, Nape anakuja na ajenda mpya na kusema Bunge litakuwa na TV yake, na kwamba vyombo vingine vyote vinavyotaka kuonyesha matangazo ya bunge ya-copy kutoka kwenye TV hiyo ya bunge. Hii inadhihirisha kwamba tatizo halijawahi kuwa gharama za uendeshaji, bali kunyima wananchi uhuru wa kujipatia habari ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Mimi naamini haya ni maandalizi ya kuja kufanya mambo mabaya zaidi hapo mbele ambayo serikali inauhakika haitaki yaonekane kwa wananchi.

Naomba kwa wenye uwelewa zaidi, watueleze sisi wananchi tunawezaje kupinga kitendo cha kiongozi/viongozi kutunyima haki yetu ya msingi ya kuoata habari! Je, wabunge wetu hawana jinsi ya kukataa maamuzi haya? INAUMA SAAANA.
 
Siamini kama Jitihada zinazofanywa na Nape kuhusu kuhujumu matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni ni maamuzi yake na kwamba hayana baraka za Rais John Pombe Magufuli.

Mwanzoni tatizo lilionekana ni kubana matumizi ya TBC, ikaonekana sawa, TBC waache wazime kuonyesha live, Star TV na Azam TV wakaendelea kuonyesha.

Baadaye, ikajitokeza taasisi isiyo ya serikali ikajitolea kulipia matangazo hayo, maana yake kwamba tatizo la budget lilitatuliwa.

Baada ya kuona hivyo, Nape anakuja na ajenda mpya na kusema Bunge litakuwa na TV yake, na kwamba vyombo vingine vyote vinavyotaka kuonyesha matangazo ya bunge ya-copy kutoka kwenye TV hiyo ya bunge. Hii inadhihirisha kwamba tatizo halijawahi kuwa gharama za uendeshaji, bali kunyima wananchi uhuru wa kujipatia habari ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Mimi naamini haya ni maandalizi ya kuja kufanya mambo mabaya zaidi hapo mbele ambayo serikali inauhakika haitaki yaonekane kwa wananchi.

Naomba kwa wenye uwelewa zaidi, watueleze sisi wananchi tunawezaje kupinga kitendo cha kiongozi/viongozi kutunyima haki yetu ya msingi ya kuoata habari! Je, wabunge wetu hawana jinsi ya kukataa maamuzi haya? INAUMA SAAANA.
Ni kwenda mahakamani kupinga kwa kufungua kesi ya kikatiba kwa sababu suala la watu kupata habari ni haki ya msingi iliyopo kikatiba, ila tatizo ni je mahakama ipo huru kuweza kufanya maamuzi ya haki kwa suala kama hilo au itaegemea upande wa serikali?
 
Siamini kama Jitihada zinazofanywa na Nape kuhusu kuhujumu matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni ni maamuzi yake na kwamba hayana baraka za Rais John Pombe Magufuli.

Mwanzoni tatizo lilionekana ni kubana matumizi ya TBC, ikaonekana sawa, TBC waache wazime kuonyesha live, Star TV na Azam TV wakaendelea kuonyesha.

Baadaye, ikajitokeza taasisi isiyo ya serikali ikajitolea kulipia matangazo hayo, maana yake kwamba tatizo la budget lilitatuliwa.

Baada ya kuona hivyo, Nape anakuja na ajenda mpya na kusema Bunge litakuwa na TV yake, na kwamba vyombo vingine vyote vinavyotaka kuonyesha matangazo ya bunge ya-copy kutoka kwenye TV hiyo ya bunge. Hii inadhihirisha kwamba tatizo halijawahi kuwa gharama za uendeshaji, bali kunyima wananchi uhuru wa kujipatia habari ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Mimi naamini haya ni maandalizi ya kuja kufanya mambo mabaya zaidi hapo mbele ambayo serikali inauhakika haitaki yaonekane kwa wananchi.

Naomba kwa wenye uwelewa zaidi, watueleze sisi wananchi tunawezaje kupinga kitendo cha kiongozi/viongozi kutunyima haki yetu ya msingi ya kuoata habari! Je, wabunge wetu hawana jinsi ya kukataa maamuzi haya? INAUMA SAAANA.


Lengo lake ni kwamba HAKUNA KUANGALIA TV MUDA WA KAZI!
 
Magu aje na maono sio ubabe usio na tija! Afunge basi hata TV Taifa haina maana abane matumizi atumie Radio Tanzania pekee inatosha!
 
Kwahiyo hautaki Bunge kuwa na TV yake? Mbona wenzetu Kenya wanayo na inaonekana wakati wa Bunge lao!
 
Ni kwenda mahakamani kupinga kwa kufungua kesi ya kikatiba kwa sababu suala la watu kupata habari ni haki ya msingi iliyopo kikatiba, ila tatizo ni je mahakama ipo huru kuweza kufanya maamuzi ya haki kwa suala kama hilo au itaegemea upande wa serikali?

Tatizo wengine hata hamuelewi uhuru wa kupata habari ni kitu gani.Mfano ukitaka kupata habari za Wilaya ya kilwa,au habari za mamlaka ya bandari kuzipata unaenda kule unaonana na wahusika wanakupa hizo habari!

Kwani ukienda bungeni huwezi zipata hizo habari? Hadi ma-hansard wanachapisha.Nenda bungeni kutafuta habari watakupa.

Ukifungua hicho kikesi uchwara utashindwa hata kabla ya kesi kuanza.
Habari za bunge ni mali ya bunge na lenyewe ndio linatakiwa lizitoe kwa umma kwa kupitia TV YAO AU msemaji wao wa bunge!
 
mkuu kwani wewe ulifikiri Nape anapata wapi kibesi cha kufanya yote hayo?
ccm ni janga la kitaifa
 
Live Coverage ya Bunge ililetwa na Rais "dhaifu" ambae tumekuwa tukiambiwa 10 years hakuna jema hata moja alilofanya. Live coverage na MCC pia ni sehemu ya udhaifu tuache kulalamika.
 
Tatizo wengine hata hamuelewi uhuru wa kupata habari ni kitu gani.Mfano ukitaka kupata habari za Wilaya ya kilwa,au habari za mamlaka ya bandari kuzipata unaenda kule unaonana na wahusika wanakupa hizo habari!

Kwani ukienda bungeni huwezi zipata hizo habari? Hadi ma-hansard wanachapisha.Nenda bungeni kutafuta habari watakupa.

Ukifungua hicho kikesi uchwara utashindwa hata kabla ya kesi kuanza.
Habari za bunge ni mali ya bunge na lenyewe ndio linatakiwa lizitoe kwa umma kwa kupitia TV YAO AU msemaji wao wa bunge!
Kwa hiyo yale matangazo ya siku zilizopita yalikuwa yakiendelea kimakosa sio?
 
Back
Top Bottom