Rais Kagame umesema kweli.... World Economic Forum 2013

Rais Kagame umesema kweli.... World Economic Forum 2013

Mwanahisa

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2012
Posts
1,382
Reaction score
515
Haya ni maneno ya Rais Kagame.

Tatizo kubwa la historia ya Afrika, imeandikwa kutoka sehemu nyingine na watu wengine wasiokua Waafrika. Ndio maana kila mtu anaiangalia Afrika nakuisemelea vile anavyojisikia kusema.Wanatunga mitizamo ya hisia zao na sio uhalisia ulivyo. Tunachoweza kufanya kwa manufaa yetu ni kuyamiliki matatizo yetu, na kutengeneza utatuzi wetu wenyewe kisha tuandike historia yetu wenyewe. Hii itatusaidia kujua ni kiasi gani cha hatari inatukabili, na mtizamo utakua halisi.

8409657466_47d92e9203_m.jpg
Huyu ndie Rais anaongoza watu wake, sio anaeruka juu ya vichwa vya anaowaongoza. Kudos Kagame. ​MODS mpeni huyu jamaa membership, typical great thinker.
 
Humjui vizuri huyu serial killer!!
HUYU MPAMAGAYA anaropoka nini ili asionekane ji serial killer?

angeacha kwanza kuwasaport M23 ili aonekane mtu mwenye busara. azama ya kanila lake la kitutsi ya kuanzisha taifa la kitutsi mashariki ya zaire limeshindikanika ndio maana an laumu west and USA.
 
Haya ni maneno ya Rais Kagame.

Tatizo kubwa la historia ya Afrika, imeandikwa kutoka sehemu nyingine na watu wengine wasiokua Waafrika. Ndio maana kila mtu anaiangalia Afrika nakuisemelea vile anavyojisikia kusema.Wanatunga mitizamo ya hisia zao na sio uhalisia ulivyo. Tunachoweza kufanya kwa manufaa yetu ni kuyamiliki matatizo yetu, na kutengeneza utatuzi wetu wenyewe kisha tuandike historia yetu wenyewe. Hii itatusaidia kujua ni kiasi gani cha hatari inatukabili, na mtizamo utakua halisi.

8409657466_47d92e9203_m.jpg
Huyu ndie Rais anaongoza watu wake, sio anaeruka juu ya vichwa vya anaowaongoza. Kudos Kagame. ​MODS mpeni huyu jamaa membership, typical great thinker.

Naunga mkono hoja

kuna haja ya kumwalika kwenye great thinker forum halafu tuwe na Q&A na yeye, lakini pia akubali kujibu maswali magumu ya peace kwenye maziwa makuu na role yake katika kuleta au kuharibu amani
 
Acha chuki binafsi na ujadili hoja...
Man of God, nisaidie mtumishi yani mtu anaongelea swala la bara la Afrika kwenye kioo cha uso wa dunia nzima, wewe unaanza kumuongelea udhaifu na machafu yake. Tuache fikra za kujadili watu, tujadili ukombozi jamani wa fikra zetu kwanza.:target:
 
Ufumbuzi wa matatizo yetu Afrika ni sisi Waafrika wenyewe! Sii wazungu au Wachina
 
Jamaa ninamkubali! usicheze na mtu aliwahii kutufunga mnyororo na kutuuza kama bidhaa! na leo hii tunantegemea kutuondolea umasikini
 
Jamaa ninamkubali! usicheze na mtu aliwahii kutufunga mnyororo na kutuuza kama bidhaa! na leo hii tunantegemea kutuondolea umasikini
Mkuu niko na wewe 100%,
Kama utakua umeipitia historia vizuri kuna mkondo wa biashara ulivuma sana zamani ukijulikana kama Triangular Trade, hii biashara ilifanyika kwa karne 4, namaanisha miaka 400, wazungu wakisomba dhahabu, vipuri na kila kilicho kizuri mbele ya macho yao, pamoja na Waafrika kuuzwa kama bidhaa na mashine zakufanyia kazi. Ila cha ajabu mali asili hazijaisha Afrika maana ni zetu na watoto wetu, ukombozi ni sisi wenyewe tu na sio ngozi nyeupe.
 
Nayaheshimu sana maoni yako kwani yanaonesha mtazamo wako
kwa mtu, lakini kumbuka kuwa kumshutumu mtu pasipo kubainisha
kwanini yeye ni hatari pia unaonekana hata wewe ni HATARI...
Man of God, Its better to be hated for who you are, than to be loved for someone you are not...... Mungu amaekuleta kwenye hii mada kwa kusudi. Naamini.
 
Sio chuki binafsi!!! huyu mtu hatari sanaAAAAAAAAAAAA!!

...

Humjui vizuri huyu serial killer!!

Niliwahi kusoma na Warundi chuo fulani zamani. Katika moja ya majadiliano yetu yalikuwa kiongozi bora aliyewahi kutokea Afrika. Kama kawaida na utanzania wangu mimi nikamtaja Nyerere.
We we we..walinicharukia aje!!! Wanasema wao wanafundishwa shuleni kabisa kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa dikteta na aliwaua Warundi wengi sana...
Nadhani na wewe unaweza kuwa umemu-experience Kagame from that angle, lakini je, uovu wake umezidi wema wake?
No...nisonekane am justifying his wrongs for some good, lakini, can we get constructive evidence citing him as a serial killer?
 
Kila kiumbe kina madhaifu yake Kagame pamoja na udhaifu wake wanyarwanda wana mengi ya kujivunia chini ya utawala wake! Na binafsi namuunga mkono kwa fikra zake matatizo ya waafrika yapaswa kutatuliwa na waafrika wenyewe kwani mengi ya matatizo yenyewe yanasababishwa na waafrika wenyewe hivyo basi yatupasa kujilaumu wenyewe kwa matatizo yanayotukabili!!!!
 
Back
Top Bottom