Rais aheshimiwe, mwekezaji adhibitiwe

Rais aheshimiwe, mwekezaji adhibitiwe

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Dharau kwa Rais haziruhusiwi. Ni marufuku kuu. Rais ni mamlaka kuu kuliko zote nchini. Yuko juu ya zote. Anayemdharau kimaneno au kimatendo hatabaki salama. Hasa anayekiuka amri za Rais.

Muda si mrefu,Rais alifuta vibali vya mashamba makubwa Arumeru. Ni mashamba ya mwekezaji huko. Kufutwa huko kuliendana na kuagizwa kugawiwa kwa mashamba hayo kwa wananchi ili waendeshe shughuli zao. Za kimaisha. Ilikuwa ni amri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Leo imeripotiwa ITV kuwa Mwekezaji amemdharau Rais. Ameuza baadhi ya ekari zilizofutiwa hati yake. Ameuza kwa wawekezaji mbalimbali. Ameuza baada. Halafu,askari wamekutwa wakilinda eneo husika. Difenda mbili. Wanalinda Rais kupuuzwa!?

Hakika,kuna watu lazima wawajibishwe. Kuanzia mwekezaji hadi askari. Rais lazima aheshimiwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
.
 
Kama yeye kilanja mkuu anapuuza wananchi kwa nini wananchi wasimpuuze?vipi wewe!!!



Swissme
 
ndio maajabu ya nchi hii. nani hasa anatawala nchi kama amri ya rais inapuuzwa na askari wa serikali wanatumika dhidi ya amri ya rais. mabwanyenye wa kihindi wanakua na jeuri ya kugoma kurejesha ardhi ya wananchi. wanameru ikibidi wajiandae kwa mapambano ya chimurenga. hakika ccm sasa inalinda makabaila na mabepari dhidi ya wakulima na wafanyakazi.
 
Dharau kwa Rais haziruhusiwi. Ni marufuku kuu. Rais ni mamlaka kuu kuliko zote nchini. Yuko juu ya zote. Anayemdharau kimaneno au kimatendo hatabaki salama. Hasa anayekiuka amri za Rais.

Muda si mrefu,Rais alifuta vibali vya mashamba makubwa Arumeru. Ni mashamba ya mwekezaji huko. Kufutwa huko kuliendana na kuagizwa kugawiwa kwa mashamba hayo kwa wananchi ili waendeshe shughuli zao. Za kimaisha. Ilikuwa ni amri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Leo imeripotiwa ITV kuwa Mwekezaji amemdharau Rais. Ameuza baadhi ya ekari zilizofutiwa hati yake. Ameuza kwa wawekezaji mbalimbali. Ameuza baada. Halafu,askari wamekutwa wakilinda eneo husika. Difenda mbili. Wanalinda Rais kupuuzwa!?

Hakika,kuna watu lazima wawajibishwe. Kuanzia mwekezaji hadi askari. Rais lazima aheshimiwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Rais ni Icon kuu ya Taifa. Kamwe hatuwez kukubali RAIS wetu kudharauliwa. Pamoja na tofauti ya Sera ya vyama, lakin tukiwa kama Taifa tusiruhusu RAIS kudharauliwa.
 
ndio maajabu ya nchi hii. nani hasa anatawala nchi kama amri ya rais inapuuzwa na askari wa serikali wanatumika dhidi ya amri ya rais. mabwanyenye wa kihindi wanakua na jeuri ya kugoma kurejesha ardhi ya wananchi. wanameru ikibidi wajiandae kwa mapambano ya chimurenga. hakika ccm sasa inalinda makabaila na mabepari dhidi ya wakulima na wafanyakazi.

Anayetawala nchi ni mwekezaji hebu tuanze na yule Singasinga yeye akaiweka serikali yote kwenye mfuko wa suruali,akawa wale wateuliwa wa rais wakifanya kazi kwa mujibu wa sheria walitupwa Mahakamani na wengine kutaka hata kufungwa.Sasa kwanini nishangae difenda inalinda mwekezaji.Wamewalea hivyo waa he wawanyooshe kidogo
 
Rais ni Icon kuu ya Taifa. Kamwe hatuwez kukubali RAIS wetu kudharauliwa. Pamoja na tofauti ya Sera ya vyama, lakin tukiwa kama Taifa tusiruhusu RAIS kudharauliwa.

Hakika mkuu CHAZA

Mzee Tupatupa
 
Last edited by a moderator:
Dharau kwa Rais haziruhusiwi. Ni marufuku kuu. Rais ni mamlaka kuu kuliko zote nchini. Yuko juu ya zote. Anayemdharau kimaneno au kimatendo hatabaki salama. Hasa anayekiuka amri za Rais.

Muda si mrefu,Rais alifuta vibali vya mashamba makubwa Arumeru. Ni mashamba ya mwekezaji huko. Kufutwa huko kuliendana na kuagizwa kugawiwa kwa mashamba hayo kwa wananchi ili waendeshe shughuli zao. Za kimaisha. Ilikuwa ni amri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Leo imeripotiwa ITV kuwa Mwekezaji amemdharau Rais. Ameuza baadhi ya ekari zilizofutiwa hati yake. Ameuza kwa wawekezaji mbalimbali. Ameuza baada. Halafu,askari wamekutwa wakilinda eneo husika. Difenda mbili. Wanalinda Rais kupuuzwa!?

Hakika,kuna watu lazima wawajibishwe. Kuanzia mwekezaji hadi askari. Rais lazima aheshimiwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

aliye toa amri ya polisi kwenda kulinda shamba la huyo mhindi akamatwe kwa kukiuka amri ya rais wa nchi
 
Hili jambo la kudharauliwa amri halali ya Rais wa JMT limenikera sana. Linatia kinyaaa zaidi kuona Polisi haohao wa Taifa ndio waliotumika kulinda upuuzi huu kama vile walindavyo maupuuzi mengine mengi tu. Zaidi sitashangaa kuona hakuna mtu yoyote atakayechukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria. Hapo pia ni wazi kuna muonekano wa rushwa ya hali ya juu. Awamu ya nne imekwishaanguka hata hivyo. Tuombe Mungu Awamu hii imalize muda wake salama. Miezi 6 iliyobaki naiona kama miaka 40. Tuzidishe maombi.
 
May b katika katika amri yake alimbakizia sehemu ya shamba hilo. Lete amri yake tujihakikishie
 
Dharau kwa Rais haziruhusiwi. Ni marufuku kuu. Rais ni mamlaka kuu kuliko zote nchini. Yuko juu ya zote. Anayemdharau kimaneno au kimatendo hatabaki salama. Hasa anayekiuka amri za Rais.

Muda si mrefu,Rais alifuta vibali vya mashamba makubwa Arumeru. Ni mashamba ya mwekezaji huko. Kufutwa huko kuliendana na kuagizwa kugawiwa kwa mashamba hayo kwa wananchi ili waendeshe shughuli zao. Za kimaisha. Ilikuwa ni amri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Leo imeripotiwa ITV kuwa Mwekezaji amemdharau Rais. Ameuza baadhi ya ekari zilizofutiwa hati yake. Ameuza kwa wawekezaji mbalimbali. Ameuza baada. Halafu,askari wamekutwa wakilinda eneo husika. Difenda mbili. Wanalinda Rais kupuuzwa!?

Hakika,kuna watu lazima wawajibishwe. Kuanzia mwekezaji hadi askari. Rais lazima aheshimiwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
.

Mzee Tupatupa, kuna uwezekano kabisa wa mtu ku-puuziwa kutokana na haiba yake na si vinginevyo.
 
Si jambo jema kinchi na kiutawala

Mzee Tupatupa

Nakubaliana na wewe mzee wangu lakini kama unatoa maagizo na haujali kama maagizo hayo yametekelezwa au la na pengine kuwajibisha pale ambapo maagizo hayajatekelezwa, tabia ya ku-puuza maagizo yanayotoka kwako hujengeka.
 
Raisi wetu anapenda kutoa ahadi hewa uku akijua jambo hilo haliwezekani. Nchi yake mfumo mzima umekuwa corrupted na yeye akiongoza, sasa kauli yake itapata wapi nguvu? Angalia makubaliano yake na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu katiba mpya aliwageuka dakika za mwisho yaani kawaacha kwenye mataa. Kwa kifupi raisi wetu haaminiki
 
Raisi ambaye ni amiri jeshi mkuu, ana kila uwezo wa kufanya watu wamheshimu. ukiona wa chini yake hawamheshimu maana yake ni kwamba yeye ameamua kuacha wamdharau.

Kitu ambacho si kizuri kwa Taifa.
 
Back
Top Bottom