Rafiki yangu amelikoroga

Anold

JF-Expert Member
Jul 15, 2010
1,456
615
Amani (jina sio halisi) ambaye ni rafiki yangu wa karibu, ndoa yake sasa ina muda wa miaka minne na amejaliwa kupata watoto wawili, wakati mke wake anakwenda kujifungua kijijini, Amani alibaki peke yake nyumbani ambapo kwenye hiyo nyumba aliyokuwa amepanga kunawapangaji wengine wakiwemo wanachuo wa Chuo fulani maarufu jijini. Fursa hii ya kuwa peke yake ilimfanya ajiingize kwenye mahusiano na mmoja wa mpangaji ambaye ni mwanachuo, kilichoendelea hapo ni kuwa mwanachuo kapata ujauzito na alipowaeleza ndugu zake ilibidi Amani aitwe na wazazi wa binti ambapo alikiri kuwa anahusika na huo ujauzito. baada ya hapo ndoa ya mkeka kufungwa huko nyumbani kwa binti bila majirani na watu wengine kujua (majirani wa Amani)

Uhusiano umeendelea na Amani amekuwa akihudumiwa na binti kwa kificho bila majirani wengine kujua. Sasa mke mkubwa kesharudi na Amani hajaeleza yaliyomkuta wakati mkewe hayupo,usiri umetawala na binti ambaye naye ni mjamzito anaishi kwenye hiyo nyumba mimba inaendelea kukua, Amani amekuwa akijiiba usiku wa manane au asubuhi sana akimtembelea bi mdogo, Amani anachofikiri ni kumfahamisha mke mkubwa UKWELI. Mimi binafsi sikufurahishwa na tukio hili na hii nikitokana na ukweli kuwa mke wa Amani ni dada mtulivu mwenye bidii na moyo wa huruma hivyo nimekuwa mzito hata kushauri ila kwa kuwa dini ya Amani haimzuii kuwa na zaidi ya mke mmoja nafikiri anaweza kupata ushauri kwa wabobezi wa dini pamoja na wanajamvi.
 
Amwambie ukwel mkewe na ndoa ihalallishwe, otherwise amuhamishe hapo nyumban huyo binti ampeleke sehem nyengne na yeye ahame after sometimes.
 
Kwanini umuite 'Amani' na siyo 'Fujo', huo ni uzinzi tu hatakama dini yake inaruhusu(dini inaruhusu kuoa mke wa 2 na siyo kuchepuka kwanza kisha ndipo alazimishwe kuoa).
 
Hivi vibinti vimezidi kujirahisisha na kutegea kupata mimba kama chambo cha ndoa mfyuuu zao wanaboa mno kutingisha ndoa za wenzao.
 
Amani (jina sio halisi) ambaye ni rafiki yangu wa karibu, ndoa yake sasa ina muda wa miaka minne na amejaliwa kupata watoto wawili, wakati mke wake anakwenda kujifungua kijijini, Amani alibaki peke yake nyumbani ambapo kwenye hiyo nyumba aliyokuwa amepanga kunawapangaji wengine wakiwemo wanachuo wa Chuo fulani maarufu jijini. Fursa hii ya kuwa peke yake ilimfanya ajiingize kwenye mahusiano na mmoja wa mpangaji ambaye ni mwanachuo, kilichoendelea hapo ni kuwa mwanachuo kapata ujauzito na alipowaeleza ndugu zake ilibidi Amani aitwe na wazazi wa binti ambapo alikiri kuwa anahusika na huo ujauzito. baada ya hapo ndoa ya mkeka kufungwa huko nyumbani kwa binti bila majirani na watu wengine kujua (majirani wa Amani)

Uhusiano umeendelea na Amani amekuwa akihudumiwa na binti kwa kificho bila majirani wengine kujua. Sasa mke mkubwa kesharudi na Amani hajaeleza yaliyomkuta wakati mkewe hayupo,usiri umetawala na binti ambaye naye ni mjamzito anaishi kwenye hiyo nyumba mimba inaendelea kukua, Amani amekuwa akijiiba usiku wa manane au asubuhi sana akimtembelea bi mdogo, Amani anachofikiri ni kumfahamisha mke mkubwa UKWELI. Mimi binafsi sikufurahishwa na tukio hili na hii nikitokana na ukweli kuwa mke wa Amani ni dada mtulivu mwenye bidii na moyo wa huruma hivyo nimekuwa mzito hata kushauri ila kwa kuwa dini ya Amani haimzuii kuwa na zaidi ya mke mmoja nafikiri anaweza kupata ushauri kwa wabobezi wa dini pamoja na wanajamvi.
unataka tukushauri mkuu ?.
 
Mabinti wa siku hizi anakuona unaishi na mkeo, anajua mkeo ana mimba na amekwenda home kujifungua lakini UNAMTONGOZA naye ANAKUBALI
 
Kunanamna yaushamba wewe mleta umbea +mwenye umbea, kwanini huyo binti msipeleke mbali na hapo?? Unajifanya kubana pua hapa mnahahibisha na ngono zembe..
 
Binadamu huwa tunaendeshwa sometimes na tamaa za muda mfupi ambazo mwisho wake hauna kheri nasi.
 
me huwa sielewi unajua kabisa huyu ni mume wa mwanamke mwingine wewe unatiiiwa mpaka mimba iningia si kujitafutia stress tu,, sababu ya jamaa kuchepuka ni kwa sababu mkewe anamimba we nawe unategesha mimba ili akuchepukie na wewe nyambafu ............. ooh wanaume wabaya fyooko pimbi kabisa
 
Back
Top Bottom