Q-NET naomba pesa yangu milioni 5, nimenunua saa mpaka sasa najuta kuwafahamu

Nashauri tufanye utafiti kwanza wa namna ambayo network marketing inafanya kazi! Network marketing believe it or not is an industry kama ilivyo industry ya mziki, kilimo, uzishaji nakadhalika. It is a legitimate business sema haifanani na biashara tulizozoea na utashi wa biashara tulizozoea hautumiki huku! Me nashauri kila mtu afanye utafiti yakinifu na jaribu kidoogo kuwa open minded msiache hizi negative comments ziwaaminishe kwamba biashara ama kampuni ya Qnet ni magumashi. Kuna wasomi kibao wamemaliza chuo wamo humu, Auditors wa the Big 4, bankers, accountants vijana wadogo tu! Kwani unadhani wao wameona nini?? Hata Kampuni kama Apple, samsung, Tesla, inapata alot of negativity but they still make huge profits so dont let these few negative comments zikuzuie fursa nzuri ya kutengeneza passive income waache wanaobisha wapambane na ajira na small businesses(Mngesoma basi ata Rich Dad Poor Dad na 21st Century Business cha Robert Kiyosaki before spewing all this rubbish)! Nimepata presentations na nafanya mchakato wa kupata iyo hela nijiunge na hii fursa japo mchakato ni mgumu sio siri ila itafahamika tu!
Ww hata hutafuti hela ya kujiunga acha uongo. Sema umeshaliwa unataka wengine waingie mkenge urudishe hela yako
 
Haha! Wajinga ndio waliwaoo.

Inasikitisha kumpoteza rafiki yangu kwa upumbavu na Ujinga wake wa kujiingiza QNET, Kuna mpuuzi mwenzie alimdanganyaa akaingia mkengee,
Ishu ilikua ngumu kwake pale alipotaka kunipumbaza kwa kuniita niijue Qnet

Kiukweli nilikua namuamini sana, hivyo kwa wito wake ulivyokua mzito ilinibidi niende kishingo upande baada ya siku kama 2 ivi kwa kutafakari ni biashara gani tena hii ananiitia huyuu , japo akili yangu ilihisi sawia na wito wake. Nikamdaganya sina nauli, akanitumia, nikasema sio kesi wacha niende

Maraa paap Morocco hiyapa, kuna kmtaa gani cjui nikafika,
Ajabu nimefika saa saba naona jamaa Anipa GOOD MORNING la nguvu bila aibu , Aalooh dah Fresh nikapiga moyo konde, Ile nafika tena ndani GOOD MORNING Zikamwagika kama Mvuaa, Vilee nataka kuwachana tu, akanitonya kausha nikapoaa mpole. Baadae baadae ikafika mda wa kusikilizaa upuuzi wao.

Sikua na iyana nikawasikiloza wee! Kutaka kuuliza maswali waksema dubiri 2nd Pres
Nikasema kwanini mspige Leo Leo wakasema, tunakupa mda wa tafqkari hivyo usikose next Pres
Siku ya next Press nkawatwanda maswali kisawasawa ila sikuridhika nayo, Sasa ishu ni namna ya kujinunga bhanaa nikajua mamboo mtelezoo...! Kumbe Ushenzi tu, ninunuee saa kwa 4M+ nikashtuka sana,
Jamaaa wakajua watanikosa wqkabidi wanipe mbinu za kutapeli ndugu zangu I'll nipate 4M+
Nikawaambia haiwezi kuwa ivyoo, kwanini msinikopeshe ninyi kisha nitawalipa? Wakapiga blablaa wakaniambia tutakusaidiaa nikasema poa nikaaga pale , tukatoka na friend kuteta kidogoo uku ananisndikizaa

Nikamuuliza we umewezaje kupata hizo pesa zotee,
Ananijibu nilidanganya naumwa cjui, mara boom lote niliweka na nilizo ungaunga kwa namna hiyo ya kudanganya, nikakmbuka nilimpa kama elfu amsini ivi alikua analia shida kumbe amekuja kuitupa. Duh

Pale palee nikamchana nikampa live mqana hua sipendi ujinga Mimi

*Nimarakumi hiyo pesa ungeenda kununua mashamba heka hata 3 Ukalima kuliko ujinga ulioufanya*
Rafiki alinuna , alitaka kupasuka ,alitaka kunipiga hata kofi, alitaka hata kuni zamisha ardhini asinione maana alijua amenikosa .
Alinipigia simu, siku mbili tatu nikamwambia usinipigie simu kwa kuniuliza ujinga wako, laa uwe navitu vy maana .

Hakika tangu 12/9 2017 siku hiyo hakupokea simu yangu kila nilipompigia, nikampotezea ,
Siku ya mwakampya tarehe 1 , ananitakia memaa Kwa kweli ninavyo mfahamu huyu kiumbee najua sasaivi anakumbuka maneno yangu .Na nimemuacha apambane na hali yake kwanzaa.

QNET NI UTAPELI --OGOPA HAO KAMA UKOMA.
 
peleka undezi wako huko Qnet .... yaani niache kufanya shughuli zangu halali za kuingiza kipato nianze kupoteza muda wa kufanyia utafiti utapeli wa Qnet ..... wajinga mmebaki wachache sana ndio maana mpo huko Qnet

Hapana si lazma uache shuhuli zako halali za kukuingizia kipato kwani unaeza fanya vyote. Lakini fahamu pia kwamba “No research no right to speak”. Kama huoni maana kutafiti jambo basi usilizungumzie kaa kimya na ignorance(ujinga) wako usituambukize wenye nia na uthubutu wa kuelewa.
 
You are Right, but why all these networks business their headquarters located abroad!
Why not tz?
inamaana nyinyi watanzania hamuwezi kuwa network business ya kuuza hata matikiti yanayolimwa tarime,
Kwani lazima Saa au imported products made in China?
Ujinga ni pale unapofanya international businesses bila kujua chimbuko lake na kujiunga na mtaji wa 5millions huo ni ujinga uliovuka mpaka,
its like unacheza kamali, that's not good investment koz risk of being a loser ipo juu sana almost 97% ni mjinga pekee who can take risks of this!
What if hiyo 5m uka invest kwenye ardhi ndan ya tz, let say kilimo cha matikiti then ukatengeneza local network ya watumiaji wa matikit baadae international matikit business network hapo sasa 5m ndo inauwezo kukufanya kuwa billionaire, very interesting! sio kama huko mnakojambajamba!!

Well as per my understanding, all these network marketing businesses originate from abroad because the products themselves come from abroad. We are not in the 1800s we are in the 21st Century. Mkuu si unafaham concept ya Globalization na international trade? Hata we unaweza kuongeza sales za ur business kwa kutumia network marketing yani kama tu apo ulivyoeleza, ni wewe tu kuamua what marketing strategy you implore as there is no limitation.

Of course ni Ujinga ni pale unapofanya international businesses bila kujua chimbuko lake lakini the good thing Qnet ina chimbuko lake where it all started so nadhani hii haihusu members wa Qnet.
 
Elimu inatakiwa itolewe kuhusiana na pyramid scheme...hela ya kiingilio inakuwa imepigigiwa mahesabu makali sana....kuna kpind itafka atakayejiunga hela yake itapita kwenye chain kiasi kwamba haitamfikia aliyeko juu (saturated)....na hapo ndo utasikia kampuni imekufa cse waliopo juu hawatapata hela...na hivyo wataipiga chini na kuhamia nchi nyingine..kwanza qnet sio biashara ni kuchangiana...ni kama saccos Fulani....hata hvyo unaibiwa mchana kweupe kabisa unaona..ukijiunga itakugharimu walau chain yako iwe na watu zaidi ya 20...ndo faida utaanza kuiona...mpak ufikishe watu 20 ni kazi sana...labda kama ww ni wakwanza kujiunga au unazungukwa na watu wenye pesa Ila wenye akli kama za kondoo..rahsi kuwaingiza mkenge...hivyo ni umaskini mkubwa unaofaidisha wachache
 
Hawa jamaa walinishawishi sana mpaka kunifuata ofisini lakini niliwastukia. Waliniita kwenye visemina vyao nikaenda kama mara 3 lakini niliamua kutojiingiza kwenye biashara za kupata pesa kirahisi bila kutoka jasho. Tunatapeliwa kutokana na kutaka kupata pesa za haraka. Itakuwaje mtu ambaye siyo ndugu yako ajifanye anataka akufanye upate pesa nyingi kwa muda mfupi? Umasikini na tamaa ndio chanzo cha kutapeliwa
 
Mkuu Tangia adamu na eva hakujawahi kufanyika biashara isiyokua na faida au kupata pesa za bure kirahisi rahisi ..siku nyingine uwe na akili timamu umeshaelewa sasa."imependeza sasa kwa sauti ya Dr.Lui"
Excellent advice!
 
Hawa majamaa wana ofs mwanza ipo mafichoni sana milimani kona ya bwiru kama unaenda kilimahewa....wamempiga jamaa yangu...ameacha kazi ya mshahara wa lak saba, akajiunga na hawa majamaa..ila nimekuja gundua jamaa amekuwa frustrated sana....nahs akli imemrudia akiwa tayar keshapigwa hasara ya kufa mtu....aliniita kwa usiri mkubwa nikaenda, nikapigwa attention ya kufa mtu mixer na gdmorning za hatar....nikaonyeshwa dogo mmoja nimesoma nae amejiunga na majamaa now amenunua range rover ya 300ml, na alidrop versity IFM ili apate kiingilio...nikapata matumaini ya mafanikio hatar... Bahat nzur huwa sifanyi kitu bila kumhusisha sir God...nikajifungia ndan ili nipate go ahead ya Mwenyezi Mungu...cha kushangaza Mungu aka reject nisiingie kwenye business... Nikaumia moyoni maana nilifkr Mungu kanifungulia njia, na nkahsi Mungu hanitakii mema....ila kwa vile Mungu amenisaidia mambo mengi nikaapa kutoingia kwny business japo nilikuwa nataman kweli....ofcn kwao niliambiwa nisimwambie mtu, na sikuambiwa bei ya product... Badae nikaamua kuingia jamii forum kuisakua hii Qnet....ndo nikakuta uozo mkubwa kama huu....dah nilishkuru Mungu sana ...kesho yake nikawatumia text kwamba totally nimeahrisha hyo biashara....
hahahhahhahahhahahahhhahah
 
Qnet naomba muwe waungwana mlimshawishi mke wangu na shemeji watoe milioni 8 ambayo walinunua saa mkasema baada ya miezi 13 watapata bilioni 3.3, mbaya zaidi mkamwambia don't share the information. Yaani mnafanya siri mazungumzo, hela mke katoa lakini mnamzungusha sijui mnasema apeleke mtu mwingine tena ndo alipwe, nyie ni matapeli wakubwa na kesi iko police.

Nawapa onyo mkinishinda mahakamani naenda Gamboshi kuwaroga, nyie watu wa ajabu mlianza kwangu baada ya kunipiga porojo zenu nikawashitukia mkamdanganya mke na shemeji na hii njia yenu kutusalimia good morning hata jioni nahisi ndo njia ya kuwapumbaza watu, nawaambia io hela mtaitoa, mama yangu msukuma.
 
ha ha ha ukiona unaitwa kwenye fursa jua wewe ndie fursa yenyewe...

na hawa jamaa wana ushawishi noma


kuna jembe humu alikuwa ana introduce cryptocurrency kama riple, bitcoin na wenzake akaanzia mbali kutaja maroboti, nyumba zinazoprintiwa... aya kama 8 anavuruga watu halafu aya ya mwisho ndio akaweka hizo coins... wajanja na werevu tukashtuka mapema kwamba anataka awapige watu
 
Back
Top Bottom