Profesa Mbilinyi: CCM na Serikali yake ni vurugu

I support Mr Mbilinyi I think zanzibar deserves to be a region and pemba to be a district.Hawa watu wanatumia fedha za serikali ya muungano bila sababu za maana imagine wanao wambunge ambao wanapitisha sheria wakati sheria hizo sio aplicable zanzibar.mpaka zipitishwe na baraza la wawakilishi sasa kwanini wanapitisha sheria ambazo haziwahusu.Jimbo moja la bara huwa na watu zaidi ya laki moja huko zanzibar watu chini ya elfu kumi.kama si ufujaji wa pesa ni nini.
 
Kauli ya Mbilinyi juu ya Zanzibar na Pemba ni kauli ya kujitafutia ujiko, hakuna cha ziada hapo.
 
“ Serikali ifikirie hili kwa kina zaidi na iwe na watu strong (wenye nguvu), isiwe na ideas (mawazo) za zamani za huyu ni mwenzetu, tuseme huyu anaweza. Tukisema huyu ni mwenzetu tutaumia.

- Unaona sasa ameshasahau kwamba hata yeye aliposhikwa na rushwa ya hela za samaki kama serikali yetu ingekwua inafanya kazi inavyotakiwa, alitakiwa afanye hii interview yake akiwa jela, lakini kwa sababu ya huyu ni mwenzetu akaishia kuachiwa, sasa huyooo anautukana mkono uliomponya akifikiri sisi wananchi wote ni wajinga.
 


Mkandara mimi sio msomi. Shule nilipitia kwa bahati mbaya tu kwa sababu ya kutaka visa ya kuja mtoni.

Na vilevile watanzania hacheni uongo wa kusema kuwa mlipiga maendeleo katika miaka ya 70 na 80.

Hakuna maendeleo yoyote yaliopatikana katika miaka ya 70 na 80 bila kutegemea misaada, grants na mikopo. Maendeleo uliyoyaona wewe hayakutegemea mapato halisi ya Tanzania.

Hivyo Tanzania kuwa katika nafasi ya 120 miaka ilikuwa ni uongo uliokithiri. Maendeleo ni lazima uweze kuya-sustain kwa mapato yako mwenyewe au mikopo ambayo unaweza kulipa bila kuathiri ubora wa maisha yako. Tanzania haijawahi kufanya hivyo hata siku moja.

Kuhusu niliyosema huo ni msimamo wangu. Na sasa ngoja ni fanunue. homogeneous ya jamii ni moja ya masharti ya maendeleo au national building. Mataifa ya Africa ni legacy za ukoloni na mipaka ya mataifa hayo ni ramani za kijiografia sio identity ya watu waishio ndani ya nchi hizo.

Tanganyika ni eneo la kijiografia lakini waishio ndani sio watanganyika ni wamakonde, wasukuma, wazigua n.k

Kenya ni eneo la kijiografia tu lakini ndani wamo wakikuyu, wajaluo, wakamba n.k

Hata hizo nchi ndogo za Afrika magharibi zinakabiliwa na matatizo hayo. Kwamba lipo taifa linalotambulika kijiografia lakini ndani watu hawafanani.

Matatizo yaliopo ni kuwa watu hamtaki kuambiana ukweli. Labda tukiambiana tunaweza kupata ufumbuzi wa matatizo yetu na kuelewana.

Mimi na wewe Mkandara tunafafana ngozi tu lakini mambo mengi tupo tofauti. Mimi na profesa Mbilinyi hatufanani kabisa; hata huko kwao sitaki kwenda. Sasa unapokuja ku-impose values zako kwangu, mimi sikuelewi hata kidogo.

Angalia mjadiliano wa IOC peke yake ulivyovuta nchi. Mwislamu atakupa sababu nyingi za kujiunga. Na mkristo atakupa sababu nyingi za kutojiunga, mojawapo ikiwemo national unity. Ni national unity gani kila mtu anakuwa suspicious na mwenzake.
 
Hiyo ya Zenji, I like it! Yaani kaamua atupe changamoto ni kama throwing a bomb in the midst of a strife, but atleast he gets what he wants - ATTENTION! Kwkwikwiii.
Huyo Mzee wenu uzee unamjia vibaya. Kwani ilikuwa lazima azumgumzie hayo ya Zenj. Khaa !!!! amekuwa kama wale huku kwetu tunawasema kuwa wanabugia vinibu halafu na kuanza kuropoka ovyo. Si angezungumza ya CCM tu tukajua kuwa anabeza fadhila alizopewa.
 

Bora unyamaze maana ule waraka alioutoa Juma Duni London ungeona ni nani fisadi ambae anatumia hela ya mwenzake na hamrudishii faida.

Halafu Baba yenu Nyerere alipotaka Muungano hakuliona hilo la idadi ya watu ?
Wanapitisha sheria kwa Tanzania na si kwa Tanganyika au Zanzibar ndio pale tunaposema Tanganyika imekwenda wapi ? Kuna mambo ya Tanganyika kuna mambo ya Zanzibar na kuna mambo ya Tanzania(Muungano).

Rudini muitafute Tanganyika kama wale waliojaribu ,wale wa kundi la akina Kikwete naamini mutafanikiwa kuipata ikiwa ipo hoi ,maana mnadharau kitu chenu na hapo ndio hatari mliyonayo ,na kwa kweli ni vizuri kuchukua hatua za dharura ili kuirudisha Tanganyika kwa hapa tulipo ,maana kushitukizia tu Muungano umekufa kifo cha ghafla kutokana na msukumo wa damu basi itakuwa pata shika huko,maana kama kulinda itabidi mulinde huko kwanza ,kwani wananchi walio wengi huko Tanganyika watakuwa na matatizo roho zao zitauma sana na kuona walipoteza muda ,hivyo atakae jaribu kulinda Muungano na kuurudisha atakosa sapoti ya wananchi ambao kwa wakati huo watapandisha ari na kusema kuwa sasa ni wakati wa sisi WaTanganyika kujitambua na kuwa na chetu kwani kuna tabu gani tunaona aibu gani kuitwa Tanganyika ?,hivyo hali iliyopo sasa ni nzuri sana kwa Upande wa Tanganyika na maendeleo yao yatakuwa ya kweli mafisadi watakuwa ni bidhaa adimu.
 
Zakumi,
Mkuu mbona maelezo yako yote yanazungumzia WATU na sio ARDHI..
nimesoma vizuri hoja zako zote zina point kuwa wenye matatizo ni sisi binadamu iwe makabila au dini na sio ukubwa wala udogo wa nchi..
 
Zakumi,
Mkuu mbona maelezo yako yote yanazungumzia WATU na sio ARDHI..
nimesoma vizuri hoja zako zote zina point kuwa wenye matatizo ni sisi binadamu iwe makabila au dini na sio ukubwa wala udogo wa nchi..

Bob:

Samahani kwa posti yangu ya mwanzo mimi na wewe tunafanana. Isipokuwa Afrika mpaka watu wamwage damu ndio waelewe kuwa tofauti na perception za mtu mwingine kuhusu maisha vinafaa kuheshimiwa.

Intellectuals wetu mara nyingi wanatumia rangi kuwa ni kigezo cha kutufanya kuwa taifa wakati kuna mila na utamaduni uliokuwepo zaidi ya miake elfu.

Hivyo huwezi kusema kuwa Zanzibar uwe mkoa au Pemba wilaya wakati identity ya Zanzibar ime-exist kabla Karl Peter kuja.

Kuna watu wanataka East Afrika wakati hile identity ya Tanzania ndio kwanza inaanza kuota mizizi.

Hizi project za kutafuta umoja wakati hatuna identity zinatumalizia resources tu.
 

Ba Mkadara, si kesi ya kugawa majimbo. Ni kuigawa nchi ili kila upande ujitegemee na ujiangalie kama Taifa na SEREKALI yake. sasa hivi ZANZIBAR is treated as jimbo na ndio maana inachapa miguu hapo ilipo ingekua mbali bila kuwa jimbo au mkoa wa Tanganyika kama baadhi yetu wanavyoamini. Unakumbuka mikoa ya kusini ilkuwa kwa kuwahamishia Wafanya kazi wabovu? (adhabu yako ukikorofisha kazini: LINDI/MTWARA) Huko kukasahaulika ikawa kama sio sehemu ya Tanzania/Tanganyika.Unakumbuka sera ya madaraka mikoani? nayo haikusaidia. Mwl Akaja na Mpya Makao makuu DODOMA ati akiwa hapo katikati atatuona vizuri na atatuhudumia na kutushughulikia kirahisi. Yote ilikuwa kutafuta nafuu ya kumudu kuiongoza nchi na kuwanufaisha Wananchi Lakini yaelekea ukubwa wa eneo na wingi wa watu (population) unashinda NYENZO na UWEZO wa utekelezaji na ndio maana TUMEBOBEA KATIKA KUOMBAOMBA KUKOPA na KUIBIANA. Tumeshaona mbinu ya kujiunga inatusumbua, tujaribu ya KUJIGAWA.
 
Habari kama hizi zimepotea sana JF hakuna waandishi wenye weledi tena...hata magazeti yashazimwa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…