Prof. Mwandosya anena ya moyoni

Prof. Mwandosya anena ya moyoni

Status
Not open for further replies.

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
Thursday, July 30, 2015

PROFESA MWANDOSYA ANENA YA MOYONI



mwandosya.jpg

Na Profesa Mark Mwandosya


Leo ni siku inayofuatia jana, siku ambayo Ndugu yangu Edward Ngoyai Lowassa aliacha rasmi uanachama wa CCM na kupewa kadi ya uanachama wa Chadema. Si yeye tu bali alisindikizwa na mke wake mpendwa Mama Regina Lowassa.

Nilidhani leo mitandao yote ingesheni habari hiyo kubwa. Kumbe nami nimekuwa "staa" katika mitandao ya kijamii. Kuanzia asubuhi nimekuwa nikipokea na kujibu simu mbalimbali nikiulizwa maoni yangu kuhusu tukio la jana, kuhusu mchakato wa Dodoma uliomalizika hivi karibuni, na "habari" kubwa imekuwa Mwandosya, Mwapachu na ole Medeye wahamia Chadema!

Kuhusu Ndugu Lowassa kuhamia Chadema nionavyo mimi ni jambo la kawaida sana katika demokrasia ya vyama vingi.

Wanachama hutoka na kuingia karibu kila siku. Hivyo basi tukio la jana lisingegonga vichwa vya habari kama isingekuwa kwa umaarufu wa mhusika. Jambo la msingi kwa CCM ni kutafakari, bila ghadhabu, na kwa utulivu, ni sababu zipi za msingi zilizofanya hili jambo litokee? Je tunaweza kujifunza lolote katika hili ili kukiimarisha Chama?

Tunaweza kuboresha nini katika taratibu na kanuni zetu? Nimeulizwa pia kitendo cha Ndugu Lowassa kuhamia Chadema kina athari gani kwa CCM?

Pamoja na kutotokuwa msemaji rasmi wa Chama, tukio hili lina maslahi ya umma kwa ujumla hivyo kukwepa kujibu hakusaidii. Siasa ni takwimu, hasa tunapoelekea Oktoba. Kwa mantiki hiyo mtu mmoja kukihama Chama kuna maana kura moja iliyopungua.

Kwa kuwa haiwezekani kuirudisha, basi changamoto ni kuwa na mkakati wa kutafuta kura ya kufidia, kuzuia kupotea kwa kura nyingine, na kuongeza idadi ya wanaoingia ili iwe kubwa kuliko ile ya wanaotoka.

Msaafu wa dini unasema mchungaji bora ni yule anayeweza kuwaacha kondoo wake tisini na tisa walio salama ili amtafute yule mmoja aliyepotea! Suala la kujiuliza katika mazingira ya yaliyotokea ni je tulikuwa wachungaji bora?

Nadhani moja ya mambo ya msingi CCM itabidi tulitafakari kuhusiana na mchakato wa kumpata mgombea wetu kwa nafasi ya urais ni je tunamtafuta mwanachama ambaye atakuwa Rais? Je tunamtafuta mtu ambaye atakuwa Rais wa nchi na Mwenyekiti wa Chama? Au tunamtafuta mtu atakayekuwa Rais na Waziri Mkuu?

Vigezo vya kumtafuta mtu huyo vinapishana kama ambavyo orodha wa wenye nia au mifumo ya kumpata itapishana. Naamini tungelitafakari haya yote huenda tusingefika hapa tulipo. Lakini Taifa ni kubwa kuliko sisi watu na uhai wake ni mpaka "kiama cha wafu".

Tujadili masuala haya na mengine muhimu, kwa ujasiri, uwazi na ukweli. Nahitimisha kwa kujibu taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii na watu wengi ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari kuhusu Mwandosya kuhama kwenda Chadema.

Misingi iliyojengwa na waasisi wa Chama, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Amani Karume naendelea kuamini bado ni sahihi. Ndiyo iliyotuletea heshima kubwa kama Taifa.

Kama tumeyumba turudi katika misingi. Itikadi ya Chama inajengwa juu ya misingi hiyo. Hivyo basi kwangu mimi Ilihali misingi ipo, na imara, nitaendelea kuwa mwanachama wa CCM ili kwa pamoja na wanachama wenzangu tuendelee kulijenga Taifa juu ya misingi hiyo, kila wakati tukikumbuka kile alichotuasa Baba wa Taifa, Tujisahihishe!
 
no correlation between the point and the title ,,expand your thread
 
Nimegundua kwamba ni dhahiri Prof.Mark Mwandosya hamkubali Magufuli na haoni kama atamudu kukiimarisha chama hata kama ataukwaa urais
 
Asante Prof Mwandosya kwa busara zako. Lakini ni misingi ipi unayoongelea juu ya chama chenu ambayo iliwekwa na hao waasisi uliowataja ambayo bado ipo hai (valid )? Ni kweli wapendwa hao waasisi waliweka misingi safi na imara, ambayo mara walipotoweka ilikosa wa kuilinda na hivyo ikatoweka. Prof kama ulikuwa huna habari hivi sasa misingi hiyo imebakia historia tu. Sana sana wewe na baadhi ya wenzako mnadanganywa tu kwamba bado mpo ndani ya misingi hiyo. Na ninashauri msiendelee kutumia majina ya hao waasisi kwa lengo tu la kufanikisha masilahi yenu, huku miiko waliyoiamini mmeiacha. Asante.
 
Unaweza kuenzi misingi iliyo kwisha bomokabomoka!?? Toka kati yao ukatengwe nao!!
 
Sio Mwandosya tu,ni wengi wanaoamini hivyo.Magufuli sio presidential material.Huyu angefaa kiasi fulani kuwa waziri mkuu.Ana mchecheto mno na hana uvumilivu.
Nimegundua kwamba ni dhahiri Prof.Mark Mwandosya hamkubali Magufuli na haoni kama atamudu kukiimarisha chama hata kama ataukwaa urais
 
Kajisemea wazi kuwa kama misingi ya waasisi wa chama ipo ataendelea kuwa CCM...sasa anatambua kuwa Kolimba aliondoka kwa kuhoji kuondoka kwa misingi hiyo hiyo...haya Azimio la Zanzibar nalo ni balaa zaidi la kufuta misingi ile, kufuta miiko ya uongozi na kujilimbikizia mali vyote vimefuta misingi ile...huyu ni profesa kwa maneno mengine anasema anahama...natafsiri tu
 
Pole Mwandosya, msingi ulibomoka kitambo
 
hamuwez kujisahihisha mna vichwa vigumu kama mawe anzeni kuaga jinga ninyi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom