Polisi Updates

lazima ukae

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2013
Posts
791
Reaction score
417
Habari zenu wakubwa kwa wadogo,kipindi cha nyuma kidogo kuna member humu JF alisema kwamba wizara ya mambo ya ndani siku chache zijazo watatangaza ajira za upolisi kwani wameshapewa kibari cha kufanya hivyo.

Siku zinasonga na wala hatujaona tangazo lolote la ajira kwa level ya graduate,je wameghairi kutangaza au inakuaje.Mwenye taarifa za uhakika tunaomba atujuze.

Asanteni.
 
kuwa na subira mkuu muda si mrefu nadhani watatangaza
 
lini tena jamani, si walichukua mwaka jana wakati watu wanamaliza chuo?
 

umemaliza chuo mwaka huu? ok yatatoka lakini nafasi zitakuwa chache kwa graduates hasahasa watachukua course zenye mrengo wa upolisi
 
lini tena jamani, si walichukua mwaka jana wakati watu wanamaliza chuo?

Kila mwaka jeshi linaajiri ndugu especially kipindi hiki tunapoelekea uchaguzi mkuu inawabidi wachukue watu wakutosha kuweza kudhibiti vulumai'
 
pia msishangae wakichukua wale wanafunzi wao tu waliowatrain pale Udsm
 
umemaliza chuo mwaka huu? ok yatatoka lakini nafasi zitakuwa chache kwa graduates hasahasa watachukua course zenye mrengo wa upolisi

Kozi zenye mlengo ni zipi sababu mimi nina bachelor ya information technology
 

Kumbuka POLISI hawaajili kutoka mtaani kwasasa!Usaili kupitia JKT umeshakamilika,Usaili kwa waliomaliza kidato cha 4 mwaka jana Umeshakamilika Kinachosubiliwa kwasasa ni Usaili kwa waliomaliza kidato cha sita tu...Vuta subira matokeo ya kidato cha 6 yakitangazwa tu anza kufuatilia Mchakato kwani majina yote yatakuwa hadharani..!
 
Watu waliosoma law enforcement wakiomba hawakosi, ata polisi wengi wanaojiendeleza vyuoni wanapenda kuchukua law enforcement.
 
wapi hao,wale wanaosoma law enforcements au?

yea hao hao kwa sababu nusu ya walimu wao wanatoka makao makuu ya polisi nusu nyingine ndo shule ya sheria UDSM

ila idadi yao still ndo nadhani wengine mtapata fursa japo mtakuwa wachache all in all best wishes poti watarajiwa
 
Watu waliosoma law enforcement wakiomba hawakosi, ata polisi wengi wanaojiendeleza vyuoni wanapenda kuchukua law enforcement.

law enforcement ilikuwa inaitwa police scince kwa kuwa vyombo vingine vya ulinzi na usalama pia wanapeleka maofisa wao kujiendeleza pale ikawa inakawabidi waite law enforcement still iko chini ya police
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…