Danisamweswa
JF-Expert Member
- Jun 26, 2013
- 453
- 154
Ni jambo linalosikitisha kuona kuwa Jeshi letu la Polisi badala ya kuwa chombo cha kulinda raia na mali zao kinageuka kuwa chombo cha kuumiza raia na kuharibu mali zao. Jambo hili nimeliona wala siyo mara moja. Tukio la jana makao makuu ya polisi jijini Dar lilikua tukio la hovyo na la aibu kwa nchi yetu. Watu wamemsindikiza mwenyekiti wao wa Chama Chao wamekaa chini kwa amani kabisa polisi wanawafukuza na mbwa kama vile wamekuwa swala. Hili jeshi linalinda amani kwa mtindo huo au linavuruga amani?
Ni kigezo gani kilichotumia wa polisi kuwafukuza wanachama wa CHADEMA na hata kuwapiga waandishi wa habari? Ninapata shida kuwa jeshi hili linashindwaje kufanya kazi zake kwa weledi? wangekuwa ni wanachama wa CCM wamemsindikiza mwenyekiti wao jeshi la polisi lingefanya walichokifanya jana?
Kwa nini jeshi la polisi lisijitenge na siasa? Polisi wanalinda nani? Wananchi wanapokasirishwa na kinachoendelea dodoma wanataka kufanya maandamano polisi wanasema maandamano hayo ni haramu? Nani asiyoeona uharibifu wa fedha unaoendelea dodoma kwa kisingizio cha bunge la katiba? Siyo halali wananchi kuonyesha kutokuridhika kwao kwa maandamano?
Nguvu inayotumika kuzima maandamano ya amani kwa nini zisitumike kuzima uahalifu katika nchi hii na kupambana na majangili wanaomaliza tembo zetu? Iko haja kwa jeshi la polisi kujitoa kwenye ushabiki wa vyama vya siasa. Lisipofanya hivyo litahatarisha usalama na amani ya nchi yetu. Badala ya kuwa walinzi wa amani litageuka kuwa wavurugaji wa amani. Picha ya namna hii haifai kwa jeshi letu la polisi.
Ni kigezo gani kilichotumia wa polisi kuwafukuza wanachama wa CHADEMA na hata kuwapiga waandishi wa habari? Ninapata shida kuwa jeshi hili linashindwaje kufanya kazi zake kwa weledi? wangekuwa ni wanachama wa CCM wamemsindikiza mwenyekiti wao jeshi la polisi lingefanya walichokifanya jana?
Kwa nini jeshi la polisi lisijitenge na siasa? Polisi wanalinda nani? Wananchi wanapokasirishwa na kinachoendelea dodoma wanataka kufanya maandamano polisi wanasema maandamano hayo ni haramu? Nani asiyoeona uharibifu wa fedha unaoendelea dodoma kwa kisingizio cha bunge la katiba? Siyo halali wananchi kuonyesha kutokuridhika kwao kwa maandamano?
Nguvu inayotumika kuzima maandamano ya amani kwa nini zisitumike kuzima uahalifu katika nchi hii na kupambana na majangili wanaomaliza tembo zetu? Iko haja kwa jeshi la polisi kujitoa kwenye ushabiki wa vyama vya siasa. Lisipofanya hivyo litahatarisha usalama na amani ya nchi yetu. Badala ya kuwa walinzi wa amani litageuka kuwa wavurugaji wa amani. Picha ya namna hii haifai kwa jeshi letu la polisi.