Polepole acha kupotosha umma kuhusu siri ya ushindi wa CCM

MangwelaJr

Senior Member
Jan 4, 2017
102
241
Chama cha Mapinduzi kimewashukuru watanzania kwa kukipa ushindi mkubwa katika chaguzi ndogo za madiwani na ubunge zilizofanyika mwishoni mwa wiki huku kikiweka hadharani siri ya ushindi.

Akizungumza na vyombo vya habari katika ofisi ndogo za makao makuu ya CCM Lumumba Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Humprey Polepole amesema ushindi huo ni ishara tosha ya jinsi ambavyo watanzania wana imani na chama hicho, na kwamba kuna siri mbili kubwa zilizokipa chama hicho ushindi.

Siri ya kwanza aliyoitaja Polepole ni MAGEUZI ambapo uamuzi wa CCM kuzaliwa upya na kufanya mageuzi makubwa yanayolenga kukirudisha chama hicho kwa wanachama pamoja na kushughulika na shida na kero za watu umefanya watanzania wakielewe zaidi chama hicho.

Siri ya pili ya ushindi wa chama hicho kwa mujibu wa Polepole ni kazi nzuri ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli ambaye tangu apewe dhamana ya kuiongoza Tanzania ametekeleza kwa kiasi kikubwa ahadi nyingi nyingi alizoahidi ikiwemo ya kupambana na rushwa na ufisadi ikiwa ndiyo kazi ya kwanza aliyoanza nayo.

Polepole ametaja ahadi nyingine ambazo zimekuwa ni kivutio kikubwa na kuwafanya watanzania wakipe ushindi chama hicho ni utoaji wa elimu bure, ujenzi wa viwanda, miundombinu ikiwemo ununuzi wa ndege na zaidi ya yote kuwasikiliza wananchi na kero zao.

My take:
Humphrey Polepole anaendelea kupotosha umma kwamba ccm ni chama kinachopata mafanikio kwa kuwa kinaaminika na wananchi kwa uchapaji kazi wake na Sera zake kwamba zinatekelezeka kila kukicha..
Ukweli ni kwamba chama cha mapinduzi kinaendelea kudidimiza demokrasia nchini kwa kutumia mbinu ovu za rushwa,mabavu na hila dhidi ya vyama vya upinzani katika chaguzi mbalimbali.
Pia ccm na dola vimefanikiwa kuvitumia baadhi ya vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake kama mamluki kugawa kura za upinzani kama njia ya mafanikio yao..

Wananchi tunaona yanayoendelea ndani ya ccm na dola katika kuminya demokrasia na haki ya wananchi katika kuamua nani awe kiongozi wao.
 
Kama unashiriki Uchaguzi Ina maana umekubali Sheria zinazoongoza Uchaguzi huo otherwise ni Kelele za kuwafariji wafuuasi wenu.

Unajua Tume si huru kwanini unashiriki?

Inanikumbusha Miaka Kama 23 iliyopita Simba ilicheza na Yanga na baada ya Kipindi cha kwanza kuisha wakasema Refa wa Pambano lile tangu Mwanzo hawamkubali hivyo hawakubali achezeshe Pambano
 
Ccm imeoza, hao walioipa ushindi ni mamiozo tu!!
Haijapewa Mkuu,imejipa yenyewe.,si unawajua ni mabingwa wa kura za 'maruhan'?inawapigisha kura mpaka marehem wetu.,kwa sasa jinsi wanavyoipeleka nchi kwa kubutua ni dhahiri shahiri hawakushinda kihalali,BARA NA PWANI KOTE WALIANGUKIA PUA 15.
 
CCM ni chama kikongwe sana lakini hatua kilichonayo ya ubabaishaji hasa uibaji wa kura ni uthibitisho tosha kuwa wananchitulisha kichoka bali twatawaliwa kwa ubabe tu na si vinginevyo
 
ccm hawapati ushindi bali kwa kuwa wamekamata vyombo vya dola na serikali wanaamrisha watangazwe washindi, kuna tofauti kubwa sana.

Hii ndio inasababisha tushindwe tunawaza kuibiwa kura kila wakati! kama vipi na sisi tuibe
 
CCM ni chama kikongwe sana lakini hatua kilichonayo ya ubabaishaji hasa uibaji wa kura ni uthibitisho tosha kuwa wananchitulisha kichoka bali twatawaliwa kwa ubabe tu na si vinginevyo

Mi nachojua hawaibi Kura! Kwenye Uchaguzi Mawakala wa Upinzani wako kibao!
Tatizo ni wapiga Kura wetu wachacheeeeee
 
Huwezi kuiba kura kwa kuwa NEC ni waajiriwa wa serikali ya ccm, ili kushinda uchaguzi lazima tuwe na tume huru.

Mi naona hapo bado sana wananchi ndio wanaamua!
Wenzetu Wakenye walipata Tume Huru tena wakaiweka wenyewe lakini ni Sarakasi tupu
hawaiamini hata kidogo, Waafrika sijui nani ameroga
 
Mi naona hapo bado sana wananchi ndio wanaamua!
Wenzetu Wakenye walipata Tume Huru tena wakaiweka wenyewe lakini ni Sarakasi tupu
hawaiamini hata kidogo, Waafrika sijui nani ameroga
Suala la zanzibar na Jecha bado lawama utamsingizia mwananchi? Kenya wameweza hata kama kuna lawama ni za upande wa walioshindwa kihalali maana hawakubali kushindwa ndio maana unaona Kenya wanabadilishana madaraka kutoka chama kingine kuja kingine, wasingekuwa na tume huru KANU isingeondoka madarakani kama ilivyo ccm.
 
...maelezo na yawe mengi kadiri awezavyo, kama DPP asingeamua kuondoa ile kesi iliyokuwa inawakabili wale vijana wa 'tallying' bila shaka tungelijua kosa lao lilikuwa ni nini!
 
I may be poor lakini kuwaita wapiga kura unaotaka wakupe ulaji uoza is more than what is called brightness. Lugha mbaya za wapinzani ndio zinawafanya muishie kunawa kila mara.
 
Back
Top Bottom