Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,445
- 7,813
Timu ya ligi kuu, Coastal Union leo inacheza mechi ya marejeo na timu kutoka daraja la kwanza inayojaribu tena kurudi ligi kuu, Pamba ya Mwanza. Mechi iliyopita walitoka sare ya magoli 2-2 na mshindi yeyote wa mechi ya leo anaweka mguu ligi kuu.
========
00' Mpira unaanza hapa uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga
10' ⚽ Pamba inaandika bao la kwanza baada ya mpira maridadi wa Fadhili Juma kuguswa na beki wa Coastal na kumpoteza mlinda mlango.
29' Mwamuzi ameipa penati Coastal faida ya mkwaju wa penati baada ya Majaliwa wa Pamba kumuweka chini mchezaji wa Coastal Union
31: ⚽ AbdulRahman Sopu anaiwekea Coastal bao la kusawazisha kupitia mkwaju wa penati
49' Edward wa Pamba anapewa kadi ya njano
42' Refa anafunika tuta la pili, mpira uligonga giganja cha mchezaji wa Pamba
43' Mlinda mlango Samuel Simon anapangua mkwaju wa Sopu na Coastal inashindwa kutumia faida.
68' Mabadiliko Coastal Union, Hamadi majimengi anachukua nafasi ya Issa
71' Coastal wanapata freekick kwenye mstari wa 18 wa Pamba
72' ⚽ Abdul Sopu anaweka bao la pili kwa upande wa Coastal
89' ⚽ Mlinda Mlango wa Pamba anajifungua baada ya kujaribu kuudaka badala yake ukamgonga na kutinga nyavuni
90' Kipenga kinapigwa kuashiria tamati ya mchezo, Coastal inafanikiwa kusalia Ligi Kuu Tanzania Bara huku Pamba ya Mwanza nayo inasalia ligi daraja la kwanza.
========
00' Mpira unaanza hapa uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga
10' ⚽ Pamba inaandika bao la kwanza baada ya mpira maridadi wa Fadhili Juma kuguswa na beki wa Coastal na kumpoteza mlinda mlango.
29' Mwamuzi ameipa penati Coastal faida ya mkwaju wa penati baada ya Majaliwa wa Pamba kumuweka chini mchezaji wa Coastal Union
31: ⚽ AbdulRahman Sopu anaiwekea Coastal bao la kusawazisha kupitia mkwaju wa penati
49' Edward wa Pamba anapewa kadi ya njano
42' Refa anafunika tuta la pili, mpira uligonga giganja cha mchezaji wa Pamba
43' Mlinda mlango Samuel Simon anapangua mkwaju wa Sopu na Coastal inashindwa kutumia faida.
68' Mabadiliko Coastal Union, Hamadi majimengi anachukua nafasi ya Issa
71' Coastal wanapata freekick kwenye mstari wa 18 wa Pamba
72' ⚽ Abdul Sopu anaweka bao la pili kwa upande wa Coastal
89' ⚽ Mlinda Mlango wa Pamba anajifungua baada ya kujaribu kuudaka badala yake ukamgonga na kutinga nyavuni
90' Kipenga kinapigwa kuashiria tamati ya mchezo, Coastal inafanikiwa kusalia Ligi Kuu Tanzania Bara huku Pamba ya Mwanza nayo inasalia ligi daraja la kwanza.