Plan B kwa CHADEMA

Plan B kwa CHADEMA

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,866
Reaction score
4,252
Niliisoma vizuri sana makala ya Mzee Mwanakijiji kwenye gazeti la Tanzania Daima la jana au juzi. Makala yenye kusema anatoa karipio kali kwa Chadema kuhusu haya yanayoendelea sasa. kiukweli ukiisoma ile makala unaona kwa hakika kuwa si kwamba Chadema hawawezi kuingia madarakani, bali ccm hawana NIA ya kuachia madaraka. ccm wapo tayari kwa lolote ili kuona kuwa wanabakia madarakani. 2010 tuliona haya na Mungu mkubwa Hekima ilitawala na nchi haikuingia kwenye matatizo. 2015 mambo yanaweza kuwa tofauti sana maana mwamko kwa wananchi ni mkubwa sana juu ya mabadiliko na upuuzi unaoendelea na unaofanywa na walio madarakani.

Licha ya mwamko kuwa mkubwa vita dhidi ya mwamko nayo imepamba moto mno kuanzia serikalini, Mahakamani hadi Bungeni. Siye sote mashahidi. Chadema wanaandaa mkutano:
Leo wanajua Chadema si chama cha vurugu isipokuwa pale tu polisi wanapoingilia kutuzuia bila msingi na Mara nyingi kinyume na sheria. Hii ni credit kwa Chadema na ndiyo inayotuletea Leo mamilioni ya Watanzania. Mkakati hue hauwezi kubezwa. Umekuwa tested na umeonyesha matunda.5) sasa hive ninapoandika, tuko kwenye TOT ya viongozi wakufunzi watakaoenda kufundisha viongozi wa kanda wapatao 1,200, na wao watashuka kwenye majimbo na kufundisha viongozi wapatao 428 wa majimbo, na wao watashuka kwenye Kata kufundisha viongozi makundi yote takriban 30,000. Hii maana yake ni kuwa kuanzia Juni tuna uwezo wa kushika kwenye vijiji takriban 18,000 na vitongoji takriban 250,000, katika hatua hiyo sasa tutakuwa kweli Real Madrid na Barcelona, kwa kuwa tunaenda kuwakaba kule kule chini ambayo miaka yote walidhani hakuna chama chochote cha Upinzani kitafika huko.

Plan B ni ipi. Hatutaki vita wala umwagaji damu. Kadhalika hatutaki dhuluma. Hatutaki yatokee ya Kenya, Zimbabwe, wala yale ya Arab Spring kwani historia imetuonyesha kuwa tulipigana vita na hadi leo tunachechemea. Sie si kama wenzetu maana hatujaumbwa hivyo. Plan B ni kuweka nguvu ya ziada kwenye majimbo! Hili ni rahisi kuliko hata kuutaka huo urais. Urais utakuwa na faida gani kama chama hakitaweza kushinda majimbo ya kutosha ili kuleta ushindani usio na shaka Bungeni?

Mwisho tunawatakia Chadema kila la heri kwenye vikao vyao vya sasa na vya baadae.
 
Wadau napo hapa panahitaji michango yenu. Tusiache akili zetu zikasombwa na mkumbo wa vioja vya Bungeni. Tushirikishane mawazo kuongeza nguvu ya upinzani nchini.
 
Wadau napo hapa panahitaji michango yenu. Tusiache akili zetu zikasombwa na mkumbo wa vioja vya Bungeni. Tushirikishane mawazo kuongeza nguvu ya upinzani nchini.

Vioja vinachelewesha maendeleo. Taifa linajadili vioja...
 
CHADEMA watulie, wawaambie watanzania mapungufu ya mfumo wa uongozi/utawala na jinsi gani ya kuboresha
 
Kagua historia zote za Vurugu na Uvunjifu wa amani duniani, Utagundua source ya kubwa ni UDINI na KUKANDAMIZA DEMOKRASIA kunakofanywa na watawala.
 
400741_504897529557565_1750389005_n.jpg

Nina imani kwa usikivu huu tutavuna majimbo ya kutosha.
 
I repeat. Hii ni kwa chadema. Ninaona upuuzi unaoendelea Bungeni wa kupitisha hoja kizembe kwa wingi wa NDIOOOO. Hakika chadema kisipokuwa makini katika kuhakikisha kuwa majimbo mengi yanapatikana katka kupitisha au kukwamisha hoja Bungeni, itakuwa ni kilio na kusaga meno. Hata kama cdm wakaukwaa urais wakaacha idadi kubwa ya majimbo kwenda ccm bado itakuwa ni tatizo. Nguvu nyigi chadema izielekeze kwenye kunyakua majimbo ya kutosha sasa hata ifikapo 2015 pawe na neema.

Napatwa na jakamoyo ninapoona wapambanaji wakipata shida Bungeni kwa hoja zao makini kupeperushwa na maamuzi ya Spika. Ikiwezekana hata sasa waanze kuandaliwa vijana ambao watakuwa ndio wawakilishi wa chama wakati ukifika. Mods Cookie Buchanan naomba uzi wangu huu muurudishe jukwaa la siasa Main Forum ili upate wachangiaji. Tangu umetupwa huko suforum hakuna watu wanaenda humo. ccm hutetea yao na cdm kadhalika. Vijana na wawakilishi waandaliwe tangu sasa
 
Last edited by a moderator:
Ukichukua majimbo mengi kwa vyovyote utakuwa umechukuwa na uraisi pia kama ambavyo kupata madiwani wengi ni kupata uraisi pia. Cha muhimu ni kufungua matawi mengi vijijini kwa kadri iwezekanavyo na kuyaratibu kwa lengo la kupata madiwani wengi jambo litalosaidia kupata wabunge wengi na hatimaye kupata Raisi.
 
Wacha niwe muazi ktk hili 'Plan B' ya chadema ni kuhakikisha ccm inamuweka mgombea mkristo ili kupunguza maumivu yaliowapata katika kipindi hiki cha awamu ya nne.
Mfumo umetikiswa sana na utawala wa kikwete kwahiyo kama ccm ikimuweka muislamu 2015 basi Tanzania itawaka moto ukiongozwa na chadema.
 
Chadema bado safario ni ndefu,mnaweza mkafikiri wananchi wamehamasika bt hua hakuna watu wepesi wanadanganyika na kusahau matatizo yao kwa sekunde chache kama watz!!!mliobahatika kwenda shule na kufunguka akili hamasisha ndugu zako na jirani zako kila wakati,badilisha mtazamo wa baba yako na mama yako wakichukie chama cha mafisadi.Ukiona kijana wa leo anakomaa na sisiemu ujue ana maslahi binafsi au ni sababu tu ya ujinga.
 
Wacha niwe muazi ktk hili 'Plan B' ya chadema ni kuhakikisha ccm inamuweka mgombea mkristo ili kupunguza maumivu yaliowapata katika kipindi hiki cha awamu ya nne.
Mfumo umetikiswa sana na utawala wa kikwete kwahiyo kama ccm ikimuweka muislamu 2015 basi Tanzania itawaka moto ukiongozwa na chadema.
Tangu hapo watamweka huyo 'mkristo' by default lakini hoja za wananchi wala haziegemei huko. Wanatazama wamefanyiwa nini na hao wanaotaka kukitetea kiti cha urais

Chadema bado safario ni ndefu,mnaweza mkafikiri wananchi wamehamasika bt hua hakuna watu wepesi wanadanganyika na kusahau matatizo yao kwa sekunde chache kama watz!!!mliobahatika kwenda shule na kufunguka akili hamasisha ndugu zako na jirani zako kila wakati,badilisha mtazamo wa baba yako na mama yako wakichukie chama cha mafisadi.Ukiona kijana wa leo anakomaa na sisiemu ujue ana maslahi binafsi au ni sababu tu ya ujinga.
Ni kweli kuwa wananchi wanaweza badilika ndani ya saa 24 hasa nikichukulia kauli ya Membe katika hili. Bahati nzuri hata hao unaodhani hawajaenda shule wana mwamko wa ajabu sana kwa sasa. Labda tu wasiwe na mwamko wa kupiga kura.

Ukichukua majimbo mengi kwa vyovyote utakuwa umechukuwa na uraisi pia kama ambavyo kupata madiwani wengi ni kupata uraisi pia. Cha muhimu ni kufungua matawi mengi vijijini kwa kadri iwezekanavyo na kuyaratibu kwa lengo la kupata madiwani wengi jambo litalosaidia kupata wabunge wengi na hatimaye kupata Raisi.
Bahari nzuri Lissu kakiri Bungeni kuwa ccm wana mtandao huko ngazi wa vijiji na vitongoji. kwa kulitambua hilo inakuwa rahisi nao cdm kuchukua hatua mapema kufika ngazi hizo
 
Back
Top Bottom