hapo hakuna kufaulu....alafu unakuta kigogo toka serikalini anaenda kutembelea mashule alafu anakuta hali hiyo huku huyo kigogo kaenda na gari la milion 250
nishawahi muuliza mwalimu kwenye shule za mfano huu, kwanini hao watoto wasio na viatu wasivae hata malapa, yeboyebo au hata masendeu, akasema hivyo hawaruhusu shuleni, wanaruhusu viatu au peku basi.
kuwa peku na kufaulu havihusiani kabisaa, nyie watoto mliokulia mjini hamuwezi kuelewa, mtu hajui watoto watakula nini kesho aanze kuhangaika na viatu?!!!
inakatisha tamaa na matumaini, KUNA WATU WANAVUTA LAKI YTATU KILA SIKU, NA NDIO HAO WAMETEULIWA MOJA YA MAJUKUMU NI KUAWEKA AKILA ZAO KUONDOKANA NA HALI HII, KINYUME CHAKE WANAZUA VURUGU TU, LEO TENA NIMESKIKIA WANAONGEZEWA SIKU SITINI MBELE.
Mnataka wale watoto wenu akitoka nyumbani asubuhi ana kibakuli kina viazi vya kukaanga na vipande vya nyama na kathoda halafu anaenda kusubiria basi la shule sio mwisho wa siku 00 na masikio......Hao ndio wenye uchungu wakitoboa hakuna kulemba!!!.....
Katika mazingira haya haya nimemaliza shule na sasa naendelea na elimu ya juu naamini nitafika..!! Hata hawa wakiamua watafika wanapopataka.. Penye nia pana njia haijalishi ni eneo gani