Weka bei basi mkuu! Je, unavibali vya vizara ya afya pamoja na TFDA? kuna AC humo ndani? Pia naomba kujua yafuatayo:
- Ukitaja bei tafadhali sema hiyo hela ina cover vitu gani ( Rent, stocks, shelves, display cases, Pamoja na vibali?)
- Kodi yake kwa mwaka, Utatakiwa ku-provide tax clearance certificate kuonesha kwamba hudaiwi chochote
- Je. ulikuwa unaiendesha kwa mfumo gani, Sole proprietorship au kampuni?
- Sasa hivi kunasheria mpya ya ku-regulate maduka ya madawa, tafadhali tufahamishe duka lako lipo kwenye kundi gani. Duka la dawa muhimu au duka la...........( sikumbuki categories zake kwa usahihi, ila wewe unatakiwa utufahamishe maana uko kwenye hiyo industry tayari)
- Unawafanyakazi wangapi, na unawalipa kiasi gani kwa mwezi?
- Je una mtaalam yeyote aliyesomea pharmacy hapo dukani, na ningependa kujua kama atakuwa tayari kuendelea na management mpya.
- Gharama zinginezo ni zipi na ni kiasi gani kwa mwezi? mfano: ulinzi, usafi, maji, umeme etc
Ukinijibu hayo nitakupigia simu na hivyo kufanya mazungumzo yetu yawe mafupi mno. then tuna conclude deal fasta.