Pesa za TASAF zagawiwa mtaani

Pesa za TASAF zagawiwa mtaani

Emaoi

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2013
Posts
307
Reaction score
235
Jamani naombeni kuuliza kuna watu wanagawa pesa mitaani wakidai ni pesa za TASAF kwa ajili ya kuwasaidia wasiojiweza yaani kaya maskini pesa hizo zimesambazwa kwenye maeneo ya vituo vya Iliboru na Sanawari na wamepewa vijana wengi waliokuwepo maeneo yale na kila mmoja alipata kiasi chake kuna waliopewa elfu 30 wengine elfu 40, 50 na wengine laki moja moja.

Jamani inakuwaje pesa za watu wasiojiweza kuja kugawanywa kwa vijana mitaani tena wanaokunywa viroba kupindukia kwanini wasingechunguza hizo familia maskini na kuwapatia msaada wa kiuhalali tena pesa zenyewe zimeletwa kwa kushtukiza.

Inakuwaje watu wanajitokeza unaona kabisa huyu ni mzima lakini bado unampa laki moja kama hayo majina ya wanaostahili kupata hizo pesa hawakuwepo karibu kwanini zisingerudishwa na kuandaliwa utaratibu upya?

Si bora wangezirudisha hizo pesa zifanyiwe kazi nyingine au ziende hata kwa watu wengine wenye shida? si kuna watu kila siku wanatangaza kwenye vyombo vya habari ITV, TBC wakiomba msaada wa kuwatibu ndugu zao kwenye hospitali za ndani na nje ya nchi yetu kwanini wasingepata mgao huo?

Kwa kweli utaratibu wa ugawaji wa pesa hizi haukuwa wa halali tena zinagawanywa chini ya ulinzi wa askari jamani hizi pesa zimezua mjadala hadi wengi wamefikia hatua ya kujiuliza ni rushwa ya uchaguzi mkuu ujao? au ni za matambiko? manake hazijawafikia wale walengwa ambao wamekusudiwa nini kinaendelea au kuna siri gani ndani ya huu mgao?
 
Kwa Mujibu wa Report Yao ni kwamba wamebakiza vijiji 35 tu kuwapa pesa vijiji vingine 52 washapata pesa zao.
 
Hizo ni pesa za uchaguzi kwenda kaya masikini lakini wenye uwezo wa kupiga kura. Hao aliopewa ni maskini pia kwani ndo maana wanakunywa viroba. Kama hujapata ni kwa sababu uko mbali na mwenyekiti wako wa chama kilichoagiza wagawiwe. Safari ijayo jipendekeze kama hukupata nipigie simu.
 
hizo pesa mkurugenzi wa tasaf kaamriwa azitoe ili kurubuni wapiga kura.

tasaf huwa wana utaratibu mzuri wa kutafuta miradi ambayo wahusika wanaweza kuifanya na kuwawezesha. mf kuna walipewa kuku wa kufuga, ng'ombe wa maziwa, nguruwe nk na ikawanufaisha wahusika.

huu utaratibu wa kugawa hela mkononi yawezekana wametumika kugawa rushwa kwa niaba ya ccm.

mtumishi wa umma hata uwe na uwezo vipi ukifuata think tank ya ccm utaingizwa kwenye matope tu na kuonekana na wewe hamnazo kabisa.
 
Dah ! Wanagawa kwa foleni au kwa kujuana?
 
hizo pesa mkurugenzi wa tasaf kaamriwa azitoe ili kurubuni wapiga kura.

tasaf huwa wana utaratibu mzuri wa kutafuta miradi ambayo wahusika wanaweza kuifanya na kuwawezesha. mf kuna walipewa kuku wa kufuga, ng'ombe wa maziwa, nguruwe nk na ikawanufaisha wahusika.

huu utaratibu wa kugawa hela mkononi yawezekana wametumika kugawa rushwa kwa niaba ya ccm.

mtumishi wa umma hata uwe na uwezo vipi ukifuata think tank ya ccm utaingizwa kwenye matope tu na kuonekana na wewe hamnazo kabisa.

Waneshachelewa waambiwe hata kama wataleta magunia kwa magunia hapa arusha wamenowa na imekula kwao,ccm haitakiwi hata na kibibi cha miaka 100
 
Huyo Mkurugenzi wa Tasaf,ajiandae kwani upinzani ukiingia madarakani atajibu ni kwanini aruhusu fedha za umma zigawiwe kwa mtindo huo wa kuhonga wapiga kura
 
Mleta mada ukinijibu mwasli haya nitakuelewesha kinacho endelea TASAF AWAMU YA TATU(3)
1)PRODUCTIVE SOCIAL SAFETY NET(PSSN)
2)PUBLIC WORKS PROGRAM
Ni vitu gani?
 
Back
Top Bottom