Pesa za RADA pamoja na Pesa za BUNGE

Asante

JF-Expert Member
Dec 18, 2009
2,086
1,081
PESA YA RADA
ZAIDI ya shilingi bilioni 72 zilizorudishwa kutoka kwenye “chenji” ya rada zimeelekezwa kwenye kusaidia malengo ya Wizara ya Elimu na Ufundi katika kiwango cha elimu ya msingi.Hususani manunuzi ya vitabu na madawati katika shule za msingi Tanzania Bara.


Pesa hizo zililejeshwa kutoka kwenye malipo ya ziada yalifanywa na serikali kinyume na utaratibu kwa kampuni ya BAE Systems ya Uingereza katika manunuzi ya rada.


Akizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Zitto Kabwe alitaka kujua, "Pesa ya rada ilirejeshwa lini? Ilibadilishwa lini toka kwenye paundi kwenda kwenye shilingi za kitanzania?"

PESA YA BUNGE
April 11 2016 Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, John Pombe Magufuli amepokea taarifa ya taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa ‘Takukuru’ na hundi ya shilingi bilioni sita zilizotolewa na Ofisi ya Bunge baada kutekeleza kwa vitendo kauli ya kubana matumizi yasio na Tija ili fedha hizo zikanunulie madawati kwa ajili ya wanafunzi.

Rais Magufuli ameipongeza ofisi ya Bunge kwa kubana matumizi na kufanikiwa kuokoa shilingi Bilioni 6, ambazo zitatumika kutengeneza madawati ya wanafunzi wa shule na amezitaka ofisi na taasisi nyingine za serikali kuiga mfano huo, ameagiza fedha hizo zipelekwe Idara ya Magereza na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili vyombo hivyo vifanye kazi ya kutengeneza madawati yanayotarajiwa kuwa zaidi ya 120,000 ambayo yatasambazwa katika shule ili kukabiliana na tatizo la wanafunzi wanaokaa chini kwa kukosa madawati.

Hundi Kifani ya fedha hizo imekabidhiwa kwa Mheshimiwa Rais na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Akson, ambaye amesema Ofisi ya Bunge imetekeleza wito wa serikali wa kubana matumizi ambapo kiasi hicho cha shilingi Bilioni 6 kimepatikana kwa kipindi kifupi cha takribani nusu mwaka.​

TANGAZO LA TAMISEMI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. George Simbachawene amewataka Watendaji wa Mamlaka zilizo chini ya Ofisi ya Rais -Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa katika kipindi kijacho cha miezi sita, tatizo la upungufu wa madawati kwa wanafunzi shuleni liwe limemalizwa.​

============

1. Pesa za rada zilitengeneza madawati mangapi, shule zipi zilipokea hayo madawati na vitabu.

2. Pesa za bunge tumeambiwa inatosha kutengeneza madawati 120,000, je madawati hayo yatapatikana?

3. Simbachwene ametua agizo kila halmashauri iwe imetengeneza madawati ya kutosha na asiwepo mwanafuzi wa kukaa chini, ametoa agizo bila ya halmashauri hizo kupewa pesa za kufanyia kazi.

Halmashauri wameanza kutengeneza madawati kwa kuzuia pesa za likizo na matibabu kwa watumishi wake, itakuwaje kama madawati ya bunge yatatengenezwa kwa idadi ya 120,000 hayo madawati yatapelekwa wapi?
 
Mkuu asante kwa uchambuzi mzuri wa matamko tofuti ya serikali kuhusu fedha zilizookolewa kushughulikia tatizo la madawati.
Uchambuzi wako huu mzuri umezua maswali mengi:-
1. Ni kweli fedha za rada zilitengeneza madawati na kununua vitabu? Thamani ya fedha ilifanana na manunuzi?
2. Fedha za bunge kama kweli zitatengeneza madawati kwann waziri Simbachawene anaziagiza halimashauri kutengeneza madawati? Waziri huyu hajui kuwa fedha za rada zilifanya (kama ilifanyika) kazi hiyo? Hajui kuwa kuna fedha A bunge zinatengeneza madawati?


Nina mashaka. Yawezekana viongozi wetu hutoa kauli hewa ambazo ni tamu ili kufurahisha wanaosikiliza ama kutazama. Lkn fedha huelekezwa ktk kazi nyingine.
 
Wote wanaotoa matamko yasiyo na uhalisia ni waropokaji! Wangekuwa na strategies za kumaliza tatizo wangepeleka agenda ALAT ili kila halmashauri itoe presentation na kujipanga kujua watapata wapi pesa na muda gani kuweza kumaliza tatizo hilo! Akisema miezi 6 bila kuangalia ukubwa wa tatizo na kipato cha halmashauri ni upuuzi!! Waache kuropoka na kutoa matamko , wako chooni!!
 
Mkuu asante kwa uchambuzi mzuri wa matamko tofuti ya serikali kuhusu fedha zilizookolewa kushughulikia tatizo la madawati.
Uchambuzi wako huu mzuri umezua maswali mengi:-
1. Ni kweli fedha za rada zilitengeneza madawati na kununua vitabu? Thamani ya fedha ilifanana na manunuzi?
2. Fedha za bunge kama kweli zitatengeneza madawati kwann waziri Simbachawene anaziagiza halimashauri kutengeneza madawati? Waziri huyu hajui kuwa fedha za rada zilifanya (kama ilifanyika) kazi hiyo? Hajui kuwa kuna fedha A bunge zinatengeneza madawati?


Nina mashaka. Yawezekana viongozi wetu hutoa kauli hewa ambazo ni tamu ili kufurahisha wanaosikiliza ama kutazama. Lkn fedha huelekezwa ktk kazi nyingine.

Inashangaza sana mkuu, leo serikali inatoa miezi sita kwa halmashauri kila mtoto awe amekalia dawati, mbaya zaidi halmashauri nyingi hazina senti tano na vyanzo vyao vya mapato ni hafifu sana kukusanya mapesa yakutosheleza kazi hiyo. Pia kumbuka mwaka jana serikali ilitoa kauli kama hizo za kujenga maabara kwa shule za sekondari bila kutoa fungu lolote kwa kazi hizo.

Nafikiri kuna hila fulani inatengenezwa, fikiria kila kiongozi anazungumzia madawati pesa zinapatikana lakini zinapotezwa kimiujiza, halmashauri ndio wanabebeshwa mzigo, kuna jambo lisilo la kawaida linaumbwa na likishaumbika litaonekana tu.
 
Akizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Zitto Kabwe alitaka kujua, "Pesa ya rada ilirejeshwa lini? Ilibadilishwa lini toka kwenye paundi kwenda kwenye shilingi za kitanzania?"

Muulizeni Membe, alikuwa anazishupalia kweli kweli. Lazima atajua ziliko. Mapesa manono yale. Alisema zitaenda kununulia vitabu.
 
Kweli hawa jamaa pumzi imekata.Ubongo wao sasa unakosa oxygen ya kutosha hivyo akili zao hazifanyi kazi sawa sawa.Kweli pumzi ni muhimu sana.Kingunge aliona mbali.

Subiri watakuja na hoja kuwa elimu bure imepelekea ongezeko la wanafunzi mashuleni hivyo hali hii imeongeza uhitaji wa madawati mashuleni.

Hata hivyo, waulize data za madawati yote yaliyotengenezwa kwa kipindi chote hicho ukilinganisha na jumla ya pesa zote zilizotengwa katika kipindi hicho uone kama watakupa.
 
Kuna mambo mawili yanaleta mgongano hapa:
1. Hivi likizo ni zawadi ya mtu au haki?
2. Hivi unapo wachangisha wafanyakazi wa Halmashauri, tuseme walikosea kuomba kazi halmashauri? Wana uhusiano gani na hao watoto huko shuleni? Ndo wazazi wao? Hiyo haki ipo wapi au ni dhambi mtu kupokea mshahara wake wa haki?
Nasema, wapo viongozi waliogeuka "Wapayukaji" zaidi ya kasuku. Ukitaka kujua walichaguliwa chini ya viwango, waangalie kwenye semi zao. Analolisema bwamkubwa kwao hakuna kujiuliza.
 
Back
Top Bottom