Sizungumzii pasipoti halisi!
Baada ya pasipoti halisi kupoteza sifa kwasababu fulani fulani...
Mtu anaomba pasipoti mpya kwa jina feki (kwa kutumia affidavit) kwasababu hawezikutumia jina lake halisi alilopewa wakati amezaliwa.
Kwenye hiyo pasipoti mpya, alama za vidole ni zake na picha ni yake. Kisicho chake ni jina tu.
Na akienda airport anapita bila wasiwasi!
Ndiyo maana nikauliza kama huwa hawakagui alama mpya za vidole kwenye database yao?
Kwa maana ya kwamba, wakikagua wataziona finger prints zile zile zikiwa kwenye pasipoti ya jina jingine.
Kama mtu amebadilisha jina kisheria ni sawa. Lakini kuna "ubuyu" kwamba watu wanabadilisha sana pasipoti kwa mtindo huu!