jua mission statement
jua faida zao na hasara na nini wanafeli
jua mambo na ya kazi unayofanyia interview
jua skills zako, haswa cv yako pia
yaani usikose kujua wana branch ngapi, etc labda na wapi hawana mfano kimkoa, atm ngapi wapi na wapi, kwa nini wanahitaji zaidi au kwanini hili au lile
majibu mengine ni ya kimaisha umeona nini mazuri na manaya na yakufanyika kupanda juu na wateja kufurahi. wanatoa huduma zipi hata unaweza kumbuka advert kwa tv au redio ukijiona haujui
ukifika salimia usikae kabla hawajakuambia ukae, usikimbilie kujibu swali kama hujui ukaboronga bora kupose na kutumia sekunde kufikiria. vaa smart suti na tai usisahau au shati na tai. nyoa nywele, shevu onekana smart
usisahau jina la bosi mkuu wa benki hiyo, so ni kusoma nenda kwa website yao uchangamshe ubongo
weye unajiona utakuwa wapi miaka 5 ijayo? (lazima utataka kupanda madaraja au sio...nasema tu), ukipata malalmiko utasuluhishaje? ukipata mteja mbishi etc utafanyaje... kumbuka mteja hakikutukana haumtukani pia.
haya ni mie nisiejua ya benki zaidi ya kuweka pesa na kutoa,
goodluck