ONYO KWA CCM – SUDAN NI SOMO, SI HADITHI

ONYO KWA CCM – SUDAN NI SOMO, SI HADITHI

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
5,151
Reaction score
14,490
Wakuu salam nimetoa.

Sudan haikuanza kwa mabomu wala mapanga. Ilianza kwa serikali kupuuza maoni ya wananchi na kudhani nguvu ya dola inaweza kuzima kila kitu.
Wananchi walitaka nini?
1. Ushiriki wa kisiasa
2. Haki na usawa
3. Kusikilizwa

Serikali ikachagua nini?
1 Mabavu
2 Jeshi
3 Kufunga milango ya mazungumzo

Matokeo yake tunayaona leo.
Kosa kubwa la Sudan lilikuwa moja:
👉 Kuona kila mkosoaji kama adui wa taifa.
Hili ni kosa ambalo nchi nyingi Afrika zimefanya, na zote zimelipa gharama kubwa:
.Libya
.Sudan
.Ethiopia (sehemu)

Historia inaonyesha wazi:
Ukiziba njia za amani, wananchi hutafuta njia mbadala na mara nyingi si za amani.
Tanzania imejengwa juu ya:
.Maridhiano
.Uvumilivu
.Mazungumzo

Lakini ukweli usemwe: Amani haidumishwi kwa:
.vitisho
.ukamataji
.kuzima hoja

Amani inadumishwa kwa:
.haki
.kusikiliza
.kuheshimu tofauti

CCM ijitathmini mapema.
Sudan viongozi walichelewa kujitathmini, wakaambiwa “ni mambo madogo, yatapita”.
.Hayakupita.
.Yalikua.
.Yakawa taifa lililovunjika.
Hoja yangu ni moja tu:
👉 Chama chochote kinapojiona kikubwa kuliko wananchi, huanza safari ya hatari.
Amani ya Tanzania si mali ya CCM, wala si mali ya upinzani.
👉 ni mali ya Watanzania wote
 
Back
Top Bottom