Ombi Langu Kwa UKAWA!

Ombi Langu Kwa UKAWA!

TEKNOLOJIA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2014
Posts
4,305
Reaction score
2,563
CCM ndio wamemshagua mgombea wao wa urais,Dr John Pombe Magufuli,Hakuna asiyemjua Magufuli kwa uchapa kazi wake,Watanzania wengi wanamkubali sana.
Nawashauri UKAWA,mtakapoanza kampeni za urais ni vyema mkalenga katika changamoto zinazowakabili wananchi kila siku. Kampeni yenu ijikite katika namna mtakavyompunguzia gharama za maisha mwananchi wa kawaida,kwa kumpunguzia mzigo wa kodi.Ishambulieni CCM kama mfumo wa ulioshindwa kuifikisha nchi pale ilipotarajiwa,na namna gani nchi inahitaji mfumo mpya utakaowaharakishia maendeleo wananchi na nchi kwa ujumla.
Udhaifu mkubwa wa Dr Magufuli upo katika haiba yake ya ubabe na ile ya kutoambilika,meli ya uvuvi inaweza ikawa case study nzuri sana katika kuonyesha hasara za kuwa na viongozi wa aina hiyo kwa taifa.
Achaneni kabisa na ufisadi,mkienda na mkakati huo mjue mtashindwa,Dr Magufuli hawezi kuchafuka kwa kashfa za ufisadi kwasababu wananchi wana imani naye sana.Kazi kubwa itakuwa huko kanda ya ziwa,UKAWA mjipange hasa.
 
Hapo kweli CCM imecheza na kuamua UKAWA wajipange kwa hoja mathubutu maana huyu jamaa ndo mwiba
 
Watanzania wana mzigo upi wa kodi? Au nyinyi ndo mnaoongoza watu kukataa kulipa kodi! Acha ujinga
 
Watanzania wana mzigo upi wa kodi? Au nyinyi ndo mnaoongoza watu kukataa kulipa kodi! Acha ujinga
Haiyumkini wewe huishi Tanzania au ndiyo mafisadi wenyewe. Si tu mzigo (wingi) wa kodi bali ukubwa wa kodi zenyewe ukilinganisha na kipato cha mwananchi wa kawaida.
 
Uchapa kazi upi? wa kujenga barabara ambazo baada ya miezi mitatu zinarudi kuwa vumbi tupu?

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...yo-inasambaratika-hata-kabla-ya-ufunguzi.html

CCM ndio wamemshagua mgombea wao wa urais,Dr John Pombe Magufuli,Hakuna asiyemjua Magufuli kwa uchapa kazi wake,Watanzania wengi wanamkubali sana.
Nawashauri UKAWA,mtakapoanza kampeni za urais ni vyema mkalenga katika changamoto zinazowakabili wananchi kila siku. Kampeni yenu ijikite katika namna mtakavyompunguzia gharama za maisha mwananchi wa kawaida,kwa kumpunguzia mzigo wa kodi.Ishambulieni CCM kama mfumo wa ulioshindwa kuifikisha nchi pale ilipotarajiwa,na namna gani nchi inahitaji mfumo mpya utakaowaharakishia maendeleo wananchi na nchi kwa ujumla.
Udhaifu mkubwa wa Dr Magufuli upo katika haiba yake ya ubabe na ile ya kutoambilika,meli ya uvuvi inaweza ikawa case study nzuri sana katika kuonyesha hasara za kuwa na viongozi wa aina hiyo kwa taifa.
Achaneni kabisa na ufisadi,mkienda na mkakati huo mjue mtashindwa,Dr Magufuli hawezi kuchafuka kwa kashfa za ufisadi kwasababu wananchi wana imani naye sana.Kazi kubwa itakuwa huko kanda ya ziwa,UKAWA mjipange hasa.
 
Tatizo LA ukawa hawana Dira
Kutokuichagua UKAWA sasa inamaanisha miaka 10 mingine ya mateso. Tutegemee kuvunjiwa nyumba zetu kwa wale tulio karibu na barabara maana upana wake utakuwa ukiongezwa kila mara.
 
Ukawa lazima watokee madirishani magufuri kiboko yao.
 
ukawa lazima watokee madirishani magufuri kiboko yao.

kwa taarifa yako ukiweka ushabiki pembeni magufuli urais sio size yake. Wala hana mvuto. Yeye anafaa kuwa mtendaji ndan ya serikali na sio kupewa urais. Hata jana alivyokuwa anaongea alionyesha kabisa uwezo huo hana. Pale alipitishwa tu baada ya kuhamua kumtoa membe ili wapenzi wa lowasa wafurahi baada ya lowasa kukatwa. Hamna rais material pale
 
UKAWAAAAAAAA.... mm mwana Lowassa nakuja...

CCM byee byeeeee.... mm kura yangu UKAWA... tukose wote.. CCM wamemwaga mboga, sie tunamwaga ugali
 
Ukawa lazima watokee madirishani magufuri kiboko yao.
Ana ukiboko gani huyo Magufuli?

Ikiwa Ukawa watacheza karata yao vizuri na wakatuletea mgombea ambaye ni kipenzi cha Umma ya watanzania, naamini Ukawa wataingia Ikulu kiulaini kabisa.

Yapo makombora machache ambayo naamini Ukawa wakiyaelekeza kwake huyo Magufuli ataanguka chali.

Baadhi ya makombora hayo ni kama yafuatayo.

1. Ilikuwaje yeye ndiye alikuwa kinara wa uuzaji wa nyumba za serikali kwa watawala wa CCM na kwa ndugu zao hadi wakawauzia hata 'magirlfriends' wao ndiye tumkabidhi madaraka makubwa ya nchi, je kama alidiriki kutuuzia nyumba za serikali hadi hivi sasa watumishi wa serikali wanakosa makazi, hivi akiwa Rais wa nchi si ndiyo ataiuza kabisa nchi yetu?

2. Aombwe Magufuli aelezee ni kwa vipi yeye 'alizitafuna' zaidi ya shilingi zaidi ya bilioni 250 ambazo katika ripoti ya CAG imeonyesha zilipotea kwenye wizara yake ya ujenzi?

3. Atolee pia maelezo ni kwa vipi kiongozi mwenye kupenda 'kuropoka' kama alivyowaambia wakazi wa Dar kuwa yeyote atakayekosa nauli waliyoiongeza kwenye kivuko cha kwenda Kigamboni apige mbizi, ni kwa vipi watanzania wampigie kura kiongozi 'mropokaji' wa aina yake?

Nawe waweza ongeza mapungufu makubwa ya mteule huyo wa CCM.
 
Mimi sidhan kama mwaka huu sisi UKAWA tunapaswa kufanya kampeni za kushambulia, kwa tathimini zangu zinatuangusha, tunahtaji kampeni za kuwaambia Watanzania tunafanya nini kwao

Kwa Mfano wakati ule Dr slaa aliposema atashusha cement mpk tsh 5000 ilimpa credit sana na uaminifu na mvuto

Masikini hawa Watanzania hawahtaji Tuhuma, japo sisemi zisisemwe lakn mtu mwenye njaa anataka mara nyingi kujua atashiba vipi sio nani kamsababishia njaa

Ivo ukawa lazima wajifunze hiki kitu, Jambo jingine MGOMBEA wa UKAWA ajue kujieleza kwa Lugha nyepesi, unajua kuna ligha nyepesi ambazo ukiongea kila mwananchi atakuelewa

SISI ukawa tunatumia sana lugha ngumu kwa mfano lugha za takwimu na hesabu, kwa mfano mtu anasema fulan alipokuwa waziri alisababishia wizara hasara za tilion mia mbili, au sarafu imeshuka kwasababu hatuzalishi bidhaa za kuuza nje, au bank kiu imebakiwa na fedha za kigeni chache, au deni la Taifa ni lak 8, kwa kila Mtanzania Nk nk

Hizo lugha na mtu wa kijijini kwa bibi wapi na wapi hata maana ya fedha za kigeni hajui

Tunahtaji mtu anaeweza kusema tu, tunaenda madarakani cement tutashusha mpka elfu 5. Tutaleta komputa kila shule, tutahakikisha kila mtoto anaenda shule anasoma bure. Huu ni mfano wa lugha nyepesi

Tofauti na jambo hilohilo kuliweka katika lugha labda kama hii, tutaifanya form four kuwa elimu ya chini na ya lazima 👈 hii watakao kuelewa ni wasomi tu alieko kijijini Hawezi jua tekniko au mfumo, yeye anataka aambiwe last product sio mchakato

Ukawa hii itawaokoa.
 
Yaani watanzania mmesahau mateso ya ccm......ina magufuli sio ccm au???? mfumo wa ufisadi aliouasisi mkapa akiwa na magufuli katika baraza lake la mawaziri kuuza nyumba za serikali wanaleta wawekezaji na kuuza nchi kwa miaka 100,Magufuli alishauri nn na hao ndio wamemleta kwa kishindo hao ccm ambao mnawachukuia.....hakika watanzania tumelaaniwa!!!!
 
Back
Top Bottom