Ole Sendeka walaumu wapiga kura wako ndio waliokuadhibu sio Lowassa

mwembemdogo

JF-Expert Member
Feb 28, 2016
2,282
1,251
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
 
Yes nadhani amesikia ndiyo wanaenda kumwaribia mipango Jpm!!!! Kwani hata bunge la budget ni mbunge gani kasimamia wapiga Kura kwa dhati? ole amesahau alipokuwa akigonga meza wafanye uharifu??? 2014-2015? hakumbuki?
 
Zimwi la lLowassa linawamaliza ccm. Lowassa yeye katulia anahudhuria matamasha tu na mialiko wala hafanyi siasa wao kila siku Lowassa.

Vijana wa ccm humu wakilala wakiamka ni Lowassa, wanachama wa ccm wakilala wakiamka ni Lowassa.

Kama Lowassa katulia tu wanahaha namna hii tena kipindi kifupi hiki baada ya uchaguzi, je atakaporudi kwenye active politics itakuaje si tutawazika?
 
Mpaka Ole Sendeka anaondoka Simanjiro, Paracetamol na Panadol zilikuwa bidhaa adimu sana huko jimboni kwake.
 
Aisee,Nafuu hata hawajamchagua,anajali ng'ombe zake wapate maji huku wananchi wake wakiteseka kuyapata hayo maji kwa kutandikwa na wamasai.
 
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
Olesendeka anavuna alichopanda
 
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
Ukiona anamtaja sana basi ujue katendwa na Lowasa maana haiwi kila mda umseme tuuu
 
Hahaha aliingiza watu wengi pale afgem ila kwenye kura wakamtosa!akasema fukuza wote hao watu mia8 wakatimuliwa kazi.hehehe
 
Huyu jamaa kapewa cheo cha asante kwa kutohama chama kumfuata Lowasa, sasa anatumia fadhila hizo vibaya sana, siku Lowasa akienda simanjiro na kuwaambia wanasimanjiro wamjibu sendeka atajuta kuanzisha vita ya maneno na Lowasa, Lowasa hawezi kumjibu huyu jamaa mpayukaji bali wana simanjiro ndio watamjibu, Kashindwa na Ole Milya mtoto mdogo wa kumzaa itakuwa Lowasa jina kubwa mtu mwenye hekima tele?
 
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
Sendeka akimpa nondo za ukweli mgombea wako unaumia? Kama unaumia mwambie aache ulaghai wa kisiasa vinginevyo kila akitaka kulaghai wananchi nondo za ukweli ajue zitamkabili mpaka atakaposema poo!!.
 
Huyu jamaa kapewa cheo cha asante kwa kutohama chama kumfuata Lowasa, sasa anatumia fadhila hizo vibaya sana, siku Lowasa akienda simanjiro na kuwaambia wanasimanjiro wamjibu sendeka atajuta kuanzisha vita ya maneno na Lowasa, Lowasa hawezi kumjibu huyu jamaa mpayukaji bali wana simanjiro ndio watamjibu, Kashindwa na Ole Milya mtoto mdogo wa kumzaa itakuwa Lowasa jina kubwa mtu mwenye hekima tele?
Kwahiyo Lowassa kakutuma umjibie?
 
Mpunilevel sijatumwa Na Lowassa nimeona nimkumbushe Huyo Bw.Sendeka nahisi hamjui aliyemroga ni wapiga kura wake
 
Kwahiyo Lowassa kakutuma umjibie?
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Philip Mangula, amekosoa kauli ya Msemaji wa chama hicho, Christopher ole Sendeka ya kupambana na vyama vya upinzani kwenye majukwaa. Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Tamasha la Kigoda cha Mwalimu Nyerere lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema siasa ina wakati na mahali pake.“Hata msemaji wetu alikosea kusema CCM ingeenda kupambana nao huko huko barabarani. Hatuwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu haijengi badala yake inabomoa, wakati huu ni wakati wa kujenga nchi.“Siasa ina muda na wakati wake…tulifanya siasa za majukwaani wakati wa kampeni na uchaguzi na ule ulikua wakati wake lakini hivi sasa kuna Bunge ambalo linajadili suala muhimu la bajeti ya Serikali halafu mtu badala ya kukaa bungeni atoe mchango wa kujenga na kuboresha anataka kwenda kusimama kwenye majukwaa, suala ambalo halitasaidia kitu,” alisema Mangula.
 
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
Alijichafua sana wakati wa bunge la katiba yeye alidhani anajijenga.
 
Nimeona nichangie mada juu ya tabia aliyoianzisha msemaji wa CCM Bw.Ole Sendeka ya kumfuata fuata Mh.Lowassa katika usemaji wake.Bw.Ole Sendeka unatakiwa ukumbuke kuwa wapiga kura wa Simanjiro uliowatelekeza ukiwa mbunge ndio waliokuadhibu kwa kukunyima ubunge.

Kumbuka ukiwa mbunge ulijikita kujifanya msemaji sana bungeni badala ya kuwa mpeleka maendeleo jimboni kwako.Inashangaza kuona kila ukipanda jukwaani wewe in Lowassa, Lowassa, Lowassa.Kakukosea nini Bw.Lowassa?,kama ni CCM keshatoka kwanini unamfuatafuata?

Wewe nenda Simanjiro kawaombe radhi wapiga kura wako ila sidhani kama watakusikia wamepata mbunge kijana uliyemtafutia visa vingi lakini hukufanikiwa.
Umesahau pia kumwambia mdomo wake ndio ulio mponza. Maana nakumbuka pale Mererani aliwaambia wasipo mpa kura ana ng'ombe watampigia kura. Akiwa na maana wapiga kura wengi hawana akili lazima watampa kura. Kumbe alisahau msimamo wa Wamaasai sasa ana cheo ambacho hakipo kikatiba kama wanvyotaka kurithishana uenyekiti wa chama bila kufuata katiba inaswmaje.
Wakati juo huo wapiga debe wa Lumumba wakiwaandama wapinzani kujusu uchaguzi wa kufuata katiba.
Ni mfalme gani alikuwa mbabe kama Herode. Je ufalme wake ulidumu milele?
 
Back
Top Bottom