Ofisi ya DPP yatuhumiwa kupokea 30m/- kuzima kesi ya mauaji ya mwanafunzi

Simon Templar

Member
Mar 3, 2016
18
21
Kuna taarifa kwamba, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) imetuhumiwa kupokea Shs. 30 milioni ili kuzima kesi ya mauaji ya mwanafunzi Joel Chacha kabla haijafikishwa mahakamani.

Machi 21, 2016 baba wa marehemu, Peter Chacha, amemwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji George Masaju akilalamika kuhusu kesi hiyo yenye kumbukumbu ya polisi namba OB/IR/8304/2014 akilalamika kwamba kuna hujuma zinazotaka kufanywa na ofisi ya DPP kuizima kesi hiyo.

Barua hiyo inaeleza kwamba, ingawa tayari mtuhumiwa wa mauaji hayo, Andrew Sanga, yuko mahabusu baada ya kukamatwa Februari mwaka huu, kumekuwepo na taarifa kwamba ndugu wa mlalamikaji wamekuwa katika harakati za kukusanya fedha ili kuizima kesi hiyo.

"Mimi nilipata taarifa kutoka kwa msiri wangu aliyeko mkoani Mbeya kwamba kuna fedha kiasi cha Shs. 30 milioni zimechangwa na wazazi wa mtuhumiwa Andrew Sanga na zimepelekwa kwa mwanasheria wa serikali anayeshughulikia kesi hiyo," anasema Chacha katika barua yake kwenda kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chacha anasema kwamba, baada ya taarifa hizo aliamua kuja Dar es Salaam kutoka Mbeya ili kumuona DPP Biswalo Mganga kwa nia ya kujua mwenendo wa kesi pamoja na kumpatia taarifa hizo, lakini kwa mshangao wake, anasema Machi 21 alipokutana naye DPP alimwambia kwamba mtuhumiwa hana hatia na ameagiza aachiliwe.

"(DPP) alinijibu kwamba kesi hiyo amekwisha itolea uamuzi ya kwamba mtuhumiwa hana hatia hivyo ameelekeza aachiliwe huru," anasema Chacha kwenye barua hiyo.

Habari za kipolisi zinaeleza kwamba, marehemu Joel, ambaye wakati mauti yanamkuta alikuwa na miaka 18, alikuwa mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Feza Boys iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam, ambapo alikutwa amekufa katika mazingira ya kutatanisha wakati akiwa anaogelea katika ufukwe wa Coco Beach pamoja na mtuhumiwa.

Tukio hilo, kwa mujibu wa taarifa za kipolisi, lilitokea Jumapili, Septemba 7, 2014 majira ya saa 10 jioni na baada ya tukio hilo mtuhumiwa, ambaye aliondokea kuwa rafiki wa ghafla wa marehemu wakati akiwa likizo nyumbani kwao Mbeya, hakuwahi kutoa taarifa kwa wazazi wa marehemu wala shuleni kwake japokuwa maiti ilikuwa imechukuliwa na polisi siku hiyo na kwenda kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Mwanyamala.

Mbali ya hivyo, mtuhumiwa, ambaye simu yake ndiyo iliyotumiwa na marehemu kuwasiliana na ndugu zake mara ya mwisho saa 8:30 mchana kabla mauti hayajamkuta, alitoweka nchini Septemba 11, 2014 (siku nne baadaye) na haikujulikana mahali alikokwenda hadi mwaka 2015 wakati ilipobainika kwamba alikimbilia India kwa madai kwamba alikuwa anasoma.

Hata hivyo, taarifa ya daktari aliyeufanyia uchunguzi (post mortem) mwili wa marehemu ilieleza kwamba, kifo chake kilisababishwa na kuvunjwa shingo na siyo kuzama majini kama ilivyokuwa imeelezwa awali.

Nitarudi baadaye kuelezea undani wa tukio hili.
Barua DPP.jpg
 
Kuna taarifa kwamba, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) imetuhumiwa kupokea Shs. 30 milioni ili kuzima kesi ya mauaji ya mwanafunzi Joel Chacha kabla haijafikishwa mahakamani.

Machi 21, 2016 baba wa marehemu, Peter Chacha, amemwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji George Masaju akilalamika kuhusu kesi hiyo yenye kumbukumbu ya polisi namba OB/IR/8304/2014 akilalamika kwamba kuna hujuma zinazotaka kufanywa na ofisi ya DPP kuizima kesi hiyo.

Barua hiyo inaeleza kwamba, ingawa tayari mtuhumiwa wa mauaji hayo, Andrew Sanga, yuko mahabusu baada ya kukamatwa Februari mwaka huu, kumekuwepo na taarifa kwamba ndugu wa mlalamikaji wamekuwa katika harakati za kukusanya fedha ili kuizima kesi hiyo.

"Mimi nilipata taarifa kutoka kwa msiri wangu aliyeko mkoani Mbeya kwamba kuna fedha kiasi cha Shs. 30 milioni zimechangwa na wazazi wa mtuhumiwa Andrew Sanga na zimepelekwa kwa mwanasheria wa serikali anayeshughulikia kesi hiyo," anasema Chacha katika barua yake kwenda kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chacha anasema kwamba, baada ya taarifa hizo aliamua kuja Dar es Salaam kutoka Mbeya ili kumuona DPP Biswalo Mganga kwa nia ya kujua mwenendo wa kesi pamoja na kumpatia taarifa hizo, lakini kwa mshangao wake, anasema Machi 21 alipokutana naye DPP alimwambia kwamba mtuhumiwa hana hatia na ameagiza aachiliwe.

"(DPP) alinijibu kwamba kesi hiyo amekwisha itolea uamuzi ya kwamba mtuhumiwa hana hatia hivyo ameelekeza aachiliwe huru," anasema Chacha kwenye barua hiyo.

Habari za kipolisi zinaeleza kwamba, marehemu Joel, ambaye wakati mauti yanamkuta alikuwa na miaka 18, alikuwa mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Feza Boys iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam, ambapo alikutwa amekufa katika mazingira ya kutatanisha wakati akiwa anaogelea katika ufukwe wa Coco Beach pamoja na mtuhumiwa.

Tukio hilo, kwa mujibu wa taarifa za kipolisi, lilitokea Jumapili, Septemba 7, 2014 majira ya saa 10 jioni na baada ya tukio hilo mtuhumiwa, ambaye aliondokea kuwa rafiki wa ghafla wa marehemu wakati akiwa likizo nyumbani kwao Mbeya, hakuwahi kutoa taarifa kwa wazazi wa marehemu wala shuleni kwake japokuwa maiti ilikuwa imechukuliwa na polisi siku hiyo na kwenda kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Mwanyamala.

Mbali ya hivyo, mtuhumiwa, ambaye simu yake ndiyo iliyotumiwa na marehemu kuwasiliana na ndugu zake mara ya mwisho saa 8:30 mchana kabla mauti hayajamkuta, alitoweka nchini Septemba 11, 2014 (siku nne baadaye) na haikujulikana mahali alikokwenda hadi mwaka 2015 wakati ilipobainika kwamba alikimbilia India kwa madai kwamba alikuwa anasoma.

Hata hivyo, taarifa ya daktari aliyeufanyia uchunguzi (post mortem) mwili wa marehemu ilieleza kwamba, kifo chake kilisababishwa na kuvunjwa shingo na siyo kuzama majini kama ilivyokuwa imeelezwa awali.

Nitarudi baadaye kuelezea undani wa tukio hili.
View attachment 332191
mkuu unaporudi njoo na ushahidi wa uhusika wa dpp ili wakati anatumbuliwa kuwa na ushahidi wa moja kwa moja..

lkn pia uwe mwangalifu, inavyoonekana hao watu wanapesa so usije kujikuta nawe unapotea
 
Damu ya mtu haipotei hivi hivi Damu itamlilia muuwaji kila atkapokwenda na wanaomsaidia kukwepa sheria. Kila Mtu Duniani hapa huletwa na Mungu Kutimiza kusudio lake, Hivi hivi mtu anamkatisha maisha Mungu hata mwacha muuwaji na wanaomsaidia kukwepa. R.I.P Joel
 
So interesting,sina upande maana haya mambo ni complicated sana,ila kuvunjika shingo wakati wa kuogelea si jambo geni especially kama mtu ana dive-kuna mapathologist weledi sana kama Dr Mataka ,angekuwa involved anaweza tegua kitendawili cha cause of death
 
kumsomesha mtoto feza schools ni jambo lingine linahitaji uwe na mpunga wa kutosha

sidhani kama 30m itakuwa ni tatizo kwenu
pandeni dau mara mbili yao mpate haki yenu
 
mkuu unaporudi njoo na ushahidi wa uhusika wa dpp ili wakati anatumbuliwa kuwa na ushahidi wa moja kwa moja..

lkn pia uwe mwangalifu, inavyoonekana hao watu wanapesa so usije kujikuta nawe unapotea
Yeye hahitaji kuja na ushahidi wa kuhusika kwa DPP katika sakata hili. Anachotakiwa kuja nacho ni ushahidi wa mlalamikaji, maana mlalamikaji ndiye aliyesema DPP kamwambia kuwa ameifuta hiyo kesi...na kama barua iliyoambatanishwa hapo ni ya kweli, ina maana DPP ndiye atalazimika kutoa maelezo amejiridhisha vipi kwamba huyo mtuhumiwa hana hatia...endapo atatakiwa kufanya hivyo, maana yeye ni mtu mnene na anaweza akamwambia mlalamikaje to go to hell...hawashindwi hawa!
 
kumsomesha mtoto feza schools ni jambo lingine linahitaji uwe na mpunga wa kutosha

sidhani kama 30m itakuwa ni tatizo kwenu
pandeni dau mara mbili yao mpate haki yenu
Yaani haki igeuke kuwa biashara ya auction?
 
Hata akikaa lokapu hatanyongwa,waachane na hiyo kesi.

Wamsubiri akitoka nje wamalizane nae
 
So interesting,sina upande maana haya mambo ni complicated sana,ila kuvunjika shingo wakati wa kuogelea si jambo geni especially kama mtu ana dive-kuna mapathologist weledi sana kama Dr Mataka ,angekuwa involved anaweza tegua kitendawili cha cause of death
Kwa utaalamu wangu wa swiming, haiwezekani kwa asilimia 100 kuvunjika shingo kwa sababu tu ya diving. Labda kama utadive kwenye maji ya futi 2, ambalo ni jambo la ajabu. Majinya bahari yana buoyancy kubwa na density zaidi ya 1 yaani ktk g/cc. Hata kama utaweza kufika mita 10 ndani ya maji ambako ni vigumu maana tayari pressure inakuwa imefikia 2 atm.

Kwa maelezo ya mtoa mada sitaona ajabu. Hizo habari za kesi kufutwa zimekuwa zikisikika sana mitaani maana hata Ulimwengu aliwahi kusema wazi kwamba kuna majaji ambao wana bei. Kesi ya mauaji milioni kadhaa, na kesi inakwisha. Namuonea huruma muuaji. Hapo alipogusa ni namba nyingine. Visasi hadi kizazi cha tatu.
 
Nami si mwanasheria,lakini navyosikia,kwamba DPP aweza kufuta kesi yoyote,na asihojiwe popote,DUNIANI ila MBINGUNI tuu!..Je ni sawa? (Kumbuka mambo ya NOLLE PROSEQUI)..Hivyo huyu ndugu DPP imempendeza kutom-crucify mtuhumiwa..
 
Kwa utaalamu wangu wa swiming, haiwezekani kwa asilimia 100 kuvunjika shingo kwa sababu tu ya diving. Labda kama utadive kwenye maji ya futi 2, ambalo ni jambo la ajabu. Majinya bahari yana buoyancy kubwa na density zaidi ya 1 yaani ktk g/cc. Hata kama utaweza kufika mita 10 ndani ya maji ambako ni vigumu maana tayari pressure inakuwa imefikia 2 atm.

Kwa maelezo ya mtoa mada sitaona ajabu. Hizo habari za kesi kufutwa zimekuwa zikisikika sana mitaani maana hata Ulimwengu aliwahi kusema wazi kwamba kuna majaji ambao wana bei. Kesi ya mauaji milioni kadhaa, na kesi inakwisha. Namuonea huruma muuaji. Hapo alipogusa ni namba nyingine. Visasi hadi kizazi cha tatu.
Umeongea vizuri,kuzima "MYTHY" za kuvunjika shingo,kwa theory tamu kabisa ya Density,Buoyance and Pressure. Lakini hapo bold unamaanisha wakwetu kule kanda "maarumu"?
 
So interesting,sina upande maana haya mambo ni complicated sana,ila kuvunjika shingo wakati wa kuogelea si jambo geni especially kama mtu ana dive-kuna mapathologist weledi sana kama Dr Mataka ,angekuwa involved anaweza tegua kitendawili cha cause of death
Kweli hapo ni pagumu sana ila motive ya sanga kumuua marehemu ni nini hasa?Ila nadhani DPP anavyosema mtuhumiwa hana kesi ya kujibu inawezekana ni kutokana na upelelezi na si kwamba kuna rushwa ikizingatiwa mlalamikaji anasema zipo tetesi za rushwa.What a tragedy!Mi naamini inawezekana ni ajali ya kawaida.
 
Back
Top Bottom