Nyumba inauzwa sh. 13 mil.

Nyumba inauzwa sh. 13 mil.

Nini hatima hatima ya huyo mpangaji?

Mpangaji taarifa anayo, akipatikana mnunuzi kodi iliyobaki atarudishiwa atafute sehemu nyingine ya kupanga, kama mnunuzi atataka aendelee kupangisha basi watanegotiate nae aendelee kupanga chini ya mmiliki huyo mpya.
 
Ni dakika 7 toka barabarani kwa gari au kwa mguu Sawia?
 
Ni dakika 7 toka barabarani kwa gari au kwa mguu Sawia?

Ni kwa mwendo wa kawaida wa miguu Mkuu Kambaku. Ukiwa na gari lako unaweza kufika hadi ndani nyumbani kwa dakika 1 au mbili kutoka kwenye barabara kuu ya lami.
 
Mbona unataka kuuza haraka namna hiyo mwenzetu?
Unanitia wasi wasi, isiwe nyumba si yako mmmm?
Maana nimeona mengi mie.
Mie nitanunua ila inabidi nifanye upelelezi miezi 3 kama hiyo nyumba ni yako.

Kwanza nione picha
Alafu niende hiyo sehem nikaone
Nifanye upelelezi wa hapo watu wanasemaje

Mkuu nauza haraka ili kuokoa biashara zangu kimtaji maana zimeyumba kidogo na sioni namna nyingine ya haraka. Nyumba ni yangu, nimepangisha mtu na familia yake, pato ninalopata hapo kwenye kodi ya pango ni kidogo sana kulingana na mazingira ya kule hivyo kwa sehemu kubwa nategemea biashara zangu zaidi kuliko hiyo nyumba. Haina tatizo wala mgogoro wowote.

Mkuu Somoe kwa nini utumie miezi yote hiyo 3 kupeleleza? Just try it muda wowote, ukweli utakaoupata hapo hata ukirudi mfululizo kwa miezi 6 ni ule ule tu kama ningekuwa siuzi. Ni matatizo tu ndo yamenilazimu niuze kwa hasara ili kuokoa biashara zangu. Kama unahitaji kuona tuwasiliane kwa simu.
 
Last edited by a moderator:
Nauza haraka nyumba yenye vyumba vitatu ambayo ipo kwenye eneo kubwa la mita 35 kwa 30 Chanika mwendo wa dk 7 toka barabara ya lami. Umeme upo. Bei sh. Mil. 13, haipungui. Unaweza kuikarabati nyumba, kuongeza ukubwa au kujenga nyingine hapo hapo. Kwa anayehitaji piga simu namba 0769 449485


Ni chanika ipi? unafika chanika mwisho?
 
Huyo mpangaji analipa kiasi gani ,nataka kujua kodi za huko zikoje hata nikinunua nijue italipa baada ya muda gani
 
Nyumba ipo karibu na kituo cha daladala cha Chanika mwisho. Pale dala dala za kutoka mjini zinapoishia na kugeuza kurudi mjini. Kila chumba hapo napangisha kwa elfu 15 kwa mwezi.
 
sawa tuwekee picha basi tuone mengine yatafatia
 
Wakuu picha zinasumbua sumbua kidogo maana nashindwa kuziattach hapa. Mtanisamehe I am poor in technology ila nitajitahidi.
 
nyumba inauzwa haraka? inamaanisha unamwahi mwenzako ambaye naye anataka kuiuza haraka,sasa hapo kuna kazi
 
nyumba inauzwa haraka? inamaanisha unamwahi mwenzako ambaye naye anataka kuiuza haraka,sasa hapo kuna kazi

Mkuu tayari nimeshatoa ufafanuzi kwa nini nauza nyumba yangu haraka. Pitia taratibu comments zilizopita kwenye post hii acha haraka mkuu. Kama hutajali chukua namba ya simu uombe kuonyeshwa hiyo nyumba yangu ninayoiuza haraka uliza muuzaji ni nani kisha fanya uchunguzi peke yako kama utaona mtu mwingine anayeiuza haraka zaidi yangu.
 
Ninawashukuru wote waliopiga simu kuonyesha kutaka kuinunua nyumba na kuahidi kuja kuangalia, wote mnakaribishwa sana hadi pale atakapopatikana mmoja wa kuinunua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom