Nyumba inauzwa Kigamboni

Nyumba inauzwa Kigamboni

Doltyne

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2011
Posts
440
Reaction score
173
NYUMBA INAUZWA:
Ipo Kigamboni (Mikwambe). Kilometa 15 kutoka Ferry, Kilometa 13 kutoka Kongowe, Mita 100 tu Kutoka barabara ya lami iendayo kongowe. Ipo nje kabisa ya mradi. Kiwanja kina ukubwa wa 1200 Square Meters (kimepimwa lakini hakina hati ie surveyed plot), Nyumba ina ukubwa wa 138 Square meters, Imejengwa pembeni ya kiwanja kilicho tambarare kwahiyo kuna nafasi kubwa sana ya kujenga nyumba kubwa zaidi ndani ya kiwanja. Ina vyumba viwili vikubwa vya kulala, Haina Master bedroom, Ina Public toilet/bath kubwa, Ina jiko kubwa la kutosha, Open Plan Living/Diner. Imefanyiwa wiring, plumbing na finishing. Madirisha ni makubwa ya kutosha, (Mita 8*6 na mita 6*6), Ina tyles, Gypsum, Smooth walls, Rangi nk, Milango ya mbele na nyuma ni Secure doors isiyohitaji grills, Milango ya ndani yote ni mninga. Ina uwezekano wa kuongezeka ukubwa wa nyumba kwa kuongeza master bedroom pembeni. Ina Umeme Wa Solar (690 Watts solar system), Maji Ni ya kuchimba kisima.
Bei ni 90,000,000 Tshs TU (Maelewano yapo). PM au piga simu namba 0714881500
View attachment 75360View attachment 75361View attachment 75367View attachment 75362View attachment 75363View attachment 75364View attachment 75420View attachment 75366
 
Ndio. Mita 100 tu kutoka barabarani

OK Pazuri sema price ipo juu kidogo jaribu kuishusha weka 40-45m ndio reasonable,Unavyosema kimepimwa lakini hakina hati ina maana huyo anayemiliki amekipatapata vipi? Amerithi kutoka kwa babu bila hata maandishi? au kama alinunua hakuna hata maandishi na sahihi za shahidi na ofisa mtendaji?
 
OK Pazuri sema price ipo juu kidogo jaribu kuishusha weka 40-45m ndio reasonable,Unavyosema kimepimwa lakini hakina hati ina maana huyo anayemiliki amekipatapata vipi? Amerithi kutoka kwa babu bila hata maandishi? au kama alinunua hakuna hata maandishi na sahihi za shahidi na ofisa mtendaji?
Ushauri mzuri mkuu, ila inaelekea umepitiwa mbali kidogo na gharama za ujenzi na viwanja. 45 ni pesa ndogo sana kwa quality ya materials yaliyotumika kujenga hii nyumba. Ukipiga simu ntakueleza vema.
Kimepimwa maana yake kimeshakuwa survayed na kimeshawekwa mawe, Bado kupitisha mchoro manispaa then ndio hati (title deed) itolewe... Kwakuwa Napima mwenyewe, nahitaji kusubiri subiri majirani wapime tupeleke mchoro wa pamoja, ndio kupata Hati.
Otherwise maandishi ya mauziano ya kiwanja na umiliki yapo.
NB: Mimi ndio mmiliki.
 
Kitu kimesisimama sana na bei siyo mbaya ngoja nikuletee kichwa ....mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom