Bosi natumaini una kiwanja,na kama una malengo ya kujenga natumaini hakuna kitu ambacho kitashindikana hapa chini ya jua. Ni wewe tu kujiamini ya kwamba unaweza. Watu wengi waliojenga walianza mdogo mdogo mpaka sasa wamemaliza nyumba zao.
Hatua za Ujenzi.
1. Ramani, tafuta ramani ambayo unaipenda
2. Msingi, hii ni hatua muhimu sana katika ujenzi na nilazima msingi ujengwe kwa umakini zaidi ili kuepuka matatizo hapo baadae maana msingi ukiwa mbovu hata nyumba haitakua imara. Mahitaji ya ujenzi wa msingi ni mchanga, kokoto, matofali, cement, nondo n.k Kwenye jedwali hapo chini nitakupa makadirio ya haraka ya nyumba yangu na bei zinazotembea eneo hili. Hila gharama zinaweza kuzidi au kupungua kutegemea eneo ulilopo, aina ya nyumba unayotaka kujenga, site ilivyokaa nk.
Bosi, hizo gharama chini wala si zisikutishe. Kama vipi unaweza ukanunua vitu kama tofali, mchanga na kokoto ukamwaga site huku ukiendelea kutafuta hela ya material zinginezo.
Bosi, Ukifanikiwa kujenga msingi unakuwa umepiga hatua muhimu sana.
Item
| Unit price
| Cost
|
Mchanga tripu 2
| 130000/=
| 260000
|
Kokoto tripu 2
| 300000
| 600000
|
Matofali 2000
| 1050
| 2100000
|
Nondo
|
| 1000000
|
Labour charge
|
| 1500000
|
Bending wire, misumari, mbao, transport n.k
|
| 1000000
|
Total
|
| 6460000
|
3. Kusimamisha boma,hapa ndio nyumba inaanza kuonekana. Kwa nyumba saizi ya kati unahitaji tofali kama 2000, nondo kwa ajili ya beam, kokoto n.k
4. Kuezeka na Kupaua, gharama itategemea na unataka kupaua kwa material gani. Ni kugumu kidogo kwakuwa ni lazima kufanyika awamu moja.
5. Kushimba mashimo ya maji taka, blundering, wiring, plumbing,kuweka milango na madirisha, plaster etc. hii ni hatua ambayo unaweza kwenda nayo mdogo mdogo.
6. Finishing, Hatua ya mwisho ya kuipamba nyumba yako kwa rangi, makabati, sink, tiles nk. Hapa itategemea wewe unataka nyumba yako iweje na mfuko wakati huo unasemaje. Uzuri unaweza kwenda mdogo.
Bosi nadhani nimekupa mwanga, ingawa kuna vitu vingi nimeviacha vinaelea hewani. Natumaini wanajamii wengine wanakuja kuchangia.