Kuna watu mie siwaelewi yaani wao wanadhani kupitia nyota za maceleb waliotutoka ndio na wao watatokea aidha kwa kua wanafanana na hao nyota au swagga zimeendana, hata ivyo wengi hua hawadumu, mfano baada ya kufa sharo millionea aliibuka jamaa akajiita chura millionea ata ivyo hasikiki tena.
Marehemu ngwea baada ya kifo chake akaibuka jamaa aliyedaiwa kufanana nae lakini nae sielewi anafaidika nini na kufanana na ngwea.
Pia baada ya kanumba kufariki kaibuka mtu mwingine anayetaka kutembelea nyota yake kisa wanafanana, hata ivyo sijaona kipya kwake kwenye filamu kiasi cha kumfananisha na late kanumba.
Na wengineo mnaowafahamu!